https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, August 21, 2013

Tamasha la Fiesta kuendelea Agosti 23 Ijumaa hii mkoani Tabora



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
TAMASHA la muziki nchini linalojulikana kama Fiesta 2013, linatatarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu mkoani Tabora kwa ajili ya kuwapatia burudani za aina yake.
Linah, mkali wa Bongo Fleva
Khufanyika kwa tamasha hilo ni wiki moja tangu ilipozinduliwa rasmi Jumamosi iliyopita ya Agosti 17 mwaka huu katika Uwanja wa Tanganyika, mkoani Kigoma.
AMkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, pichani.
kizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Kampuni ya Clouds Media Group ambao ndio wandaaji wa Tamasha hilo, Ruge Mutahaba, alisema kuwa wakazi na wananchi wa Tabora wana kila sababu ya kulisubiri tamasha hilo kwa shangwe.


Ahmad Ally 'Madee'
Alisema kuwa hakuna tamasha kubwa linalochanganya wasanii wengi kwa pamoja, hivyo wadau wao wajiandae kupata burudani kabambe kutoka kwao.

“Sisi kama waandaaji tumejipanga imara kuhakikisha kuwa wasanii wote wanafanya mambo makubwa katika jukwaa ili kuwapatia vitu vya aina yake wadau na mashabiki wao.

“Hii ni ziara ndefu inayofanyika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, ikiwa na wasanii wengi, akiwamo Barnabas, Linah, Chege, Mwana FA, AY, Stamina na wengineo,” alisema.

Baada ya kumaliza ziara zao katika mikoa mbalimbali ya Tanznaia Bara, tamasha hilo litatia nanga katika jiji la Dar es Salaam, ambapo hushirikisha msanii wa Kimataifa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...