Msanii wa nyota wa filamu Tanzania, Kajala Masanja kulia, akichezesha droo ya pili ya kuwania Sh Milioni 10 ya mchezo wa Bahati Nasibu ya Biko 'Nguvu ya Buku' iliyochezeshwa jijini Dar es Salaam ambapo mshindi wake Nicholaus Mlasu kutoka Ukonga Mombasa, Ilala alinyakua kitita hicho na kuhudhuriwa na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Jehud Ngolo mwenye kitabu mkoni. Katikati ni mshindi wa Biko wa wiki iliyopita, Christopher Mgaya. Picha na Mpiga Picha Wetu.

Na Mandishi Wetu, Dar es Salaam
DROO ya pili ya wiki kutafutwa mshindi wa shindano la Bahati Nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’ ya kuwania Sh Milioni 10 imefanyika leo asubuhi huku mkazi wa Ukonga Mombasa, Ilala, jijini Dar es Salaam, ameibuka na ushindi huo na kuwa mtu wa pili kufaidika na mamilioni ya Biko, baada ya Christopher Mgaya kushinda wikiiliyopita na kukabidhiwa mamilioni yake.
Picha nyingine Kajala Masanja akimtangaza mshindi wa Biko wa wiki hii Nicholaus Mlasu kunyakua Sh Milioni 10 za Biko katika droo hiyo.

Mshindi huyo amepatikana katika droo iliyochezeshwa jana na Balozi wa Biko, Kajala Masanja pamoja na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Jehud Ngolo pamoja na Mgaya mshindi wa wiki iliyopita.
Kajala Masanja na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania kwenye notebook mkononi pamoja na mshindi wa wiki iliyopita, Chiristopher Mgaya wakiisoma namba ya mshindi wa wiki hii ambaye bwana Nicholaus Mlasu alitangazwa mshindi.

Akizungumza katika droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwamba ni furaha yao kubwa kuona wamempata mshindi mwingine aliyeshinda Sh Milioni 10 kutoka kwenye shindano lao linalofanyika kila mwisho wa wiki.

Alisema bahati nasibu ya Biko imezidi kujizolea umaarufu mkubwa kwa siku chache kutokana na urahisi wake wa kucheza pamoja na kutumia muda mdogo kulipa washindi wake, hususan wa zawazi za papo kwa papo zinazopatikana baada ya kucheza kwa kufanya miamala ya kifedha kwa simu za Vodacom, Tigo na Airtel Money.

“Ni rahisi kucheza Biko kwa sababu mtu anafanya muamala kwenye simu yake kuanzia Sh 1000 ambapo kwanza katika kipengele cha lipa bili, atakwenda kuingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 kisha ataweka 2456 kama namba yetu ya kumbukumbu.