https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, June 30, 2017

Mwanafunzi wa TEKU mkoani Mbeya ang’arishwa na Milioni 20 za Biko

Na Mwandishi Wetu, Mbeya
WAENDESHAJI wa bahati nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’, leo wamemkabidhi Sh Milioni 20 mshindi wao wa droo ya 18, Linda Mhewa, ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji University (TEKU), kilichopo jijini Mbeya.
Mshindi wa droo ya 18 ya Biko, Linda Mhewa, akiwa anazishangaa fedha zake kiasi cha Sh Milioni 20 alizokabidhiwa na waendeshaji wa bahati nasibu hiyo ya Biko Tanzania, leo jijini Mbeya.
 Mwanafunzi huyo ambaye ni msichana wa pili kufanikiwa kuzoa mamilioni ya Biko kupitia bahati nasibu ya Biko, aling’ara katika droo ya Jumatano iliyopita, ikiwa ni mwendelezo wa bahati nasibu hiyo kumwaga mamilioni kwa kupitia mchezo wao unaotoa zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja, bila kusahau droo kubwa ya Jumatano na Jumapili ya Sh Milioni 20.
Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Paul William Ntinika mwenye suti, akimpongeza mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Linda Mhewa, aliyeibuka kidedea katika droo ya 18 iliyochezeshwa Jumatano iliyopita. Makabidhiano hayo yamefanyika leo jijini Mbeya. Kushoto aliyeshika kipaza sauti ni Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven. Kulia ni Afisa wa Benki ya NMB, jijini Mbeya. Picha na Mpigapicha wetu Mbeya.

Thursday, June 29, 2017

 Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Congo, Ferre Gola, (wa pili kulia) Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Ltd, Teddy Mapunda (kulia) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru mchanganyiko, Anna Mshana, kwa pamoja wakipaka rangi katika ukuta wa chumba cha darasa la Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, wakati walipofika shuleni hapo kwa ajili ya kujionea mazingira ya shule hiyo, baada ya kuomba kusaidiwa mahitaji hayo, ambapo msaada huo umetokana na mauzo ya meza za Onyesho maalumu la mwanamuziki huyo linalofanyika leo Alhamisi kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO)

Wednesday, June 28, 2017

Waziri Mavunde ataka watu watumie Biko kukuza uchumi wao


Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mh Anthony Mavunde, kulia akiwa na mshindi wa droo ya 17 ya Biko, Evodi Mlingi, baada ya kukabidhiwa fedha zake jana mjini Dodoma. Waziri Mavunde amepongeza mshindi huyo na kumtaka azitumie fedha zake kwa uangalifu ili afanikiwe kiuchumi.



Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mheshimiwa Anthony Mavunde, amewataka Watanzania hususan wakazi na wananchi wa Dodoma kunufaika kiuchumi kwa kuutumia vyema uwapo wa mchezo wa bahati nasibu wa Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’.


Mh Mavunde ameyasema hayo jana wakati wa makabidhiano ya Sh Milioni 20 kutoka kwa mshindi wa droo ya 17 ya Biko, Evodi Mlingi, ambaye ni fundi cherehani mwenye maskani yake mjini Dodoma, akitangazwa mshindi katika droo ya 17.
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mh Anthony Mavunde kulia akiwa na wananchi wake wa Dodoma Mjini walioshinda Sh Milioni 20 za Biko kila mmoja. Evodi Mlingi katikati amekabidhiwa fedha zake jana wakati kushoto ni Ramadhan Juma Hussein aliyeshinda Milioni 20 hivi karibuni ambapo tayari ameshapokea fedha zake kutoka Biko.

Monday, June 26, 2017

Tanga watakiwa kuongeza uzalishaji


 MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku pichani, amewataka wananchi heri ya sikukuu ya Eid El Fitri huku akiwataka kujiandaa na ujio wa fursa ya mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga kwa kuongeza uzalishaji.
 
Alhaji Mussa aliyasea hayo wakati akizungumza na mtandano huu ambapo alisema mradi huo ni mkubwa ambao utahusisha watu wengi hivyo wananchi wanapaswa kujipanga ili kuweza kuendana na fursa hiyo muhimu kwa ajili ya kujiongezea kipato halisi.
Alisema lazima wakazi wa mkoa huo watambue kuwa wakati mradi huo ni mkubwa ambao unaweza kuchangia ukuaji wa kipato chao hivyo wajiandae kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwemo mama ntilie waweze kuendesha shughuli zao kisasa.

Milioni 20 nyingine za Biko zaenda tena Dodoma

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KATIKA hali inayoonyesha ya kuchachamaa na kuchangamkia fursa, droo ya 17 ya Bahati ya Nasibu ya Biko ‘ijue Nguvu ya Buku, imefanyika jana jijini Dar es Salaam, huku fundi charahani wa Mjini Dododoma, Evodi Mlingi, kuibuka kidedea na kujinyakulia jumla ya Sh Milioni 20 zinazotolewa na Biko.
Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akizungumza na simu ya mshindi wa Sh Milioni 20 kutoka Dodoma, Evodi Mlingi aliyepatikana baada ya kuchezesha droo ya 17 ya Bahati Nasibu ya Biko. Kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki.

Droo ya kumtafuta mshindi huyo wa Sh Milioni 20 imeendeshwa na Balozi wa Biko, Kajala Masanja kwa kushirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema Mlingi ni mshindi wa pili wa anayetokea Dodoma mjini kujinyakulia Sh Milioni 20, akitanguliwa na Ramadhan Juma Hussein, aliyekabidhiwa fedha zake wiki iliyopita.

Friday, June 23, 2017

Kijiji cha Shujaaz chafunguliwa katika mashindano ya EAC 2017 Mjini Moshi

Mwakilishi wa Taasisi ya Wel tel Story ,watayarishaji wa Mradi wa Shujaaz,Alan Lucky akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani ) kuhusu kufunguliwa kwa kijiji cha Shujaaz katika Mashindano ya vijana ya Afrika Mashariki maarufu kama East Africa Cup 2017 yanayofanyika katika shule ya Sekondari Moshi Ufundi .
Baadhi ya Wageni wakijiandikisha kabla ya kuingia katika kijiji hicho ambako kumekuwa kukitolewa mafunzo mbalimbali hasa ya Kilimo .

Muuza simu Dodoma ajazwa Milioni 20 za Biko

MILIONI 20 NYINGINE KUPATA MWINGINE JUMAPILI HII
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MFANYABIASHARA wa simu za mikononi mjini Dodoma, Ramadhan Juma Hussein, jana amejazwa Sh milioni 20 zake alizoshinda kutoka kwa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko, aliyoshinda katika droo ya 16, iliyochezeshwa Jumatano iliyopita.
Mshindi wa droo ya 16 ya Sh Milioni 20 kutoka Biko, Ramadhan Juma Hussein katikati akiwa amebeba fedha zake alizokabidhiwa jana na waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko mjini Dodoma katika benki ya NMB. Kulia ni Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven.
Kupokea kwa pesa zake kumekuja baada ya kuwa miongoni mwa Watanzania lukuki wanaocheza bahati nasibu ya Biko kuwania zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni 1,000,000, pamoja na donge nono la Sh Milioni 20 linalotoka Jumatano na Jumapili.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kulia akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 20 mshindi wao wa Dodoma, Ramadhan Juma Hussein. Wengine wanaoshuhudia ni familia ya Ramadhan wakati wa makabidhiano hayo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika katika benki ya NMB mjini Dodoma, Juma anasema kwamba pesa hizo atazitumia vizuri katika kukuza biashara zake kama alivyokuwa akimuomba Mungu aweze kushinda mamilioni ya Biko.

Wednesday, June 21, 2017

Milioni 20 za Biko zaenda kwa Ramadhan wa Dodoma

Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akiwa kwenye tukio la kumtafuta mshindi wa Sh Milioni 20 wa droo ya 16 ya Biko, ambapo bwana Ramadhan Hussein wa Dodoma aliibuka kidedea na kuzoa kiasi hicho cha pesa kutoka Biko. Kushoto ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki.



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
DONGE nono la Sh Milioni 20 la bahati nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’, droo ya 16, leo limeenda kwa mshindi wao Ramadhan Juma Hussein, mwenye maskani yake mjini Dodoma, ikiwa ni mara ya kwanza kwa Makao Makuu ya Nchi ya Tanzania kupata mshindi wake katika droo kubwa inayofanyika Jumatano na Jumapili.

Ushindi wa Ramadhan umekuja siku chache baada ya kukabidhiwa fedha zake mshindi wa Handeni, mkoani Tanga, Yahaya Ally Khamis, aliyekabidhiwa pesa mapema wiki hii.
Akizungumza katika droo hiyo leo mchana, Balozi wa Biko, Kajala Masanja alimpongeza Ramadhan kwa kuibuka na ushindi mnono wa Sh Milioni 20, huku akiwataka Watanzania wote kucheza kwa wingi na mara nyingi ili wazoe mamilioni ya Biko.

“Naomba kutangaza kwamba mshindi wetu wa Jumatano hii wa Sh Milioni 20 ni Ramadhan anayetokea mjini Dodoma, ambaye pia amekiri kucheza Biko mara kwa mara pamoja kuwahi kushinda zawadi za papo kwa hapo ambao zinatoka kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja zinatoka kila dakika kwa wale wanaocheza bahati nasibu yetu.

Mchezo huu unachezwa kwa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kwenye mitandao ya simu ya Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel, ambao huingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu 2456, baada ya kufanya muamala kuanzia Sh 1,000 na kuendelea na kupata nafasi ya kuwania zawadi za papo kwa hapo bila kusahau kuingia kwenye droo kubwa ya Sh Milioni 20,” Alisema Kajala.

Tuesday, June 20, 2017

Biko yampatia Milioni 20 mshindi wa Handeni

Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, kushoto akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 20 Yahaya Ally Khamis, dakika chache kabla ya kuelekea katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni walipomkabidhi pia kiasi cha fedha taslimu Sh Milioni 20 kama mshindi wa droo ya 15 ya Biko iliyochezeshwa Jumapili iliyopita. Wengine ni majirani na wadau wa Khamis, wilayani Handeni wakishuhudia wakati anakabidhiwa hundi hiyo.

Na Mwandishi Wetu, Handeni
WAENDESHAJI wa bahati nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’ jana wamemkabidhi jumla ya Sh Milioni 20 mshindi wao Yahaya Ally Khamis, aliyeibuka na ushindi katika droo ya 15, iliyochezeshwa juzi Jumapili, huku akitokea wilayani Handeni, mkoani Tanga. Makabidhiano hayo yamefanyika wilayani hapa katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni, mkoani Tanga, tayari kwa kuziingiza katika matumizi ya kumkwamua kiuchumi.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, akimkabidhi Sh Milioni 20 mshindi wao wa Handeni, mkoani Tanga, Yahaya Ally Khamis kulia. Makabidhiano hayo yalifanyika katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni mkoani Tanga jana. Kushoto ni afisa wa NMB, wilayani Handeni akishuhudia makabidhiano hayo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema mchezo wao ni rahisi kucheza na kushinda, tofauti na michezo mingine inayotumia akili nyingi pamoja na uzoefu wa kufuatilia mambo mengi ya kukuletea ushindi. Alisema Biko ili mtu ashinde ni kufanya muamala kwenye simu yake ya Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money kwa kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba ya kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ikiwa ni 2456, huku mchezaji akiwa haulizwi swali lolote kwenye simu yake.

Sunday, June 18, 2017

Mkulima wa Handeni Tanga ajinyakulia Sh Milioni 20 za Biko


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MAMBO yamezidi kunoga katika bahati nasibu ya ‘SMS’ ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’, baada ya mkulima kutoka wilayani Handeni, mkoani Tanga, Yahaya Ally Khamis, kuibuka kidedea kwa kuzoa Jumla ya Sh Milioni 20 kutoka kwenye bahati nasibu hiyo inayozidi kushika kasi nchini Tanzania, ikiwa ni droo yake ya 15 tangu kuanzishwa kwake.
Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania, Humud Abdulhussein kushoto, akiagana na Balozi wa Biko, Kajala Masanja mara baada ya kumaliza kuchezesha droo ya 15 leo jijini Dar es Salaam, ambapo mkulima wa wilayani Handeni, mkoani Tanga, Yahaya Ally Khamis aliibuka kidedea kwa kuzoa jumla ya Sh Milioni 20.

Bahati nasibu hiyo imechezeshwa leo  jijini Dar es Salaam na Balozi wa Biko, Kajala Masanja kwa kushirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein.

Akizungumza katika droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwamba bahati nasibu yao imezidi kupanua mbawa zake kwa kutua wilayani Handeni, mkoani Tanga kwa mshindi wao Yahaya ambaye ana umri wa miaka 50 anayejishughulisha na kilimo.
Alisema ni faraja yao kuona mchezo wao umekuwa ukitoa washindi katika sehemu mbalimbali za Tanzania, akiamini kuwa ni mwendelezo wa kuhakikisha kwamba kila mtu anaibuka na mamilioni ya Biko.

Friday, June 16, 2017

Magreth Sinyangwa wa Kilosa Morogoro apokea Milioni 20 za Biko

.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kulia akiwa katika makabidhiano ya Sh Milioni 20 kwa mshindi wao wa Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa aliyeibuka kidedea katika droo kubwa iliyofanyika Jumatano iliyopita. Kushoto ni mume wa Magreth, Bahati Ramadhani na mwingine ni Ofisa wa NMB Tawi la Kilosa, akiwa kwenye makabidhiano hayo.


Na Mwandishi Wetu, Morogoro
MJASIRIAMALI mwanamke mwenye umri wa miaka 26, Magreth Sinyangwa amekabidhiwa jumla ya Sh Milioni 20 za ushindi wa bahati nasibu ya Biko, aliyoupata katika droo kubwa iliyochezeshwa juzi Jumatano, jijini Dar es Salaam, huku akiwa mwanamke wa kwanza kuibuka na ushindi huo.

Sinyangwa amekabidhiwa fedha hizo Kilosa katika benki ya NMB, mkoani Morogoro na Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, ambaye pamoja na mambo mengine, alimpongeza mshindi huyo na kumtaka azitumie fedha zake kwa uangalifu pamoja na kuboresha maisha yake ya kila siku.
Mshindi wa donge nono la Sh Milioni 20 kutoka Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa akiwa ameshika fedha zake baada ya kukabidhiwa kutoka kwa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Heaven alisema ni wakati wa kutajirika kwa kutumia vyema bahati nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’ iliyozidi kuchanja mbuga na kutoa mamilioni ya Sh kwa washindi wa droo kubwa zinazofanyika Jumatano na Jumapili, sanjari na zawadi za papo kwa hapo.

Wednesday, June 14, 2017

Magreth Sinyangwa wa Kilosa Morogoro azoa Milioni 20 za Biko


Balozi wa Biko Kajala Masanja na mwakilishi wa Bodi Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein, wakihakiki namba ya mshindi wa Sh Milioni 20 kutoka Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Sinyangwa na kumpigia ili kumjulisha juu ya ushindi wake.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MOTO wa bahati nasibu ya Biko ama ‘Ijue Nguvu ya Buku’, umezidi kuchanja mbuga baada ya droo yake ya 14 kufanyika leo jijini Dar es Salaam, huku mkazi wa Kilosa Morogoro, Magreth Sinyangwa, akiwa mwanamke wa kwanza kuzoa jumla ya Sh Milioni 20 zinazotolewa na waendeshaji wa bahati nasibu hiyo inayotikisa hapa nchini.


Droo hiyo iliyompelekea utajiri mshindi huyo wa Morogoro, imechezeshwa na Balozi wa Biko Tanzania, Kajala Masanja na kushuhudiwa pia na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein.
Balozi wa Biko Kajala Masanja akiagana na mwakilishi wa Bodi Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein, mara baada ya kumaliza kuchezesha droo ya 14 ya Sh Milioni 20 iliyochezeshwa leo jijini Dar es Salaam, huku Magreth Sinyangwa akiwa mwanamke wa kwanza kuibuka na mamilioni hayo ya Biko tangu kuanzishwa kwa bahati nasibu hiyo hususan kwa droo kubwa za Sh Milioni 10 hadi 20.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema moto wa Biko umezidi kuchanja mbuga baada ya kumpata mshindi wao wa Sh Milioni 20, huku kwa mara ya kwanza wakimpata mshindi ambaye ni mwanamke tangu kuanzishwa kwa bahati nasibu yao.


Alisema washindi hao ni wale wanaocheza bahati nasibu yao kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kufanya miamala kwenye simu zao za M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money, ambapo watatakiwa kuingia kwenye lipa bili au lipa kwa M-Pesa na kuingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na namba ya kumbukumbu 2456 tayari kwa kucheza.


“Baada ya kuingiza namba ya kumbukumbu pia atatakiwa kuweka kiasi cha kucheza ambacho kinaanzia Sh 1000 na kuendelea ambapo kiasi cha Sh 1000 kitampatia nafasi mbili ambazo ni ushindi wa papo kwa hapo pamoja na donge nono la Sh Milioni 20 kwa Jumapili ijayo kama tulivyompata mwingine kwa droo tuliyochezesha jana.

Tuesday, June 13, 2017

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo akagua majengo ya shule ya msingi Hondogo

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akizungumza jambo mara baada ya kuzuru kwa ziara ya kikazi katika Shule ya Msingi Hondogo iliyopo Kata ya Kibamba.

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo Leo June 13, 2016 amefanya ziara ya kikazi kwa kutembelea shule ya Msingi Hondogo iliyopo katika Kata ya Kibamba Jijini Dar es salaam kujionea hali ya Miundombinu ikiwemo majengo ya shule na ufanisi wa utoaji elimu katika Shule hiyo.

Mara baada ya kuzuru katika Shule hiyo Mkurugenzi Kayombo amebaini kuwapo na ubovu wa madarasa hivyo kuamua kujenga madarasa mengine mapya matano kwa ajili ya wanafunzi kujisomea kwa uhuru na amani shuleni hapo.

Amani: Milioni 20 za bahati nasibu ya Biko zitanikomboa

Mshindi wa Sh Milioni 20 wa Bahati Nasibu ya Biko 'Ijue Nguvu ya Buku', Amani Kabuku, akiwa katika furaha baada ya kukabidhiwa fedha zake katika benki ya NMB, jijini Dar es Salaam jana. 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MSHINDI wa Milioni 20 wa bahati nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’ wa  droo ya 13, Amani Kabuku, jana amekabidhiwa fedha zake huku akisema kuwa zawadi hiyo ya donge nono itamkomboa kiuchumi, licha ya umri mdogo aliokuwa nao, akiwa na miaka 23 tu.


Makabidhiano hayo ya Biko na Kabuku ambaye pia anatokea katika familia ya mwanahabari nguri nchini Tanzania, Generali Ulimwengu, yalifanyika katika benki ya NMB jijini Dar es Salaam, sambamba na kumpatia elimu ya kifedha saa chache kabla ya kufungua akaunti kwa ajili ya kuingiza fedha zake alizoshinda katika droo hiyo ya aina yake.
Mshindi  wa Sh Milioni 20 wa droo ya 13 ya Biko 'Ijue Nguvu ya Buku', Amani Kabuku, katikati akiwa amepakatia fedha zake baada ya kukabidhiwa jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven na kushoto ni afisa wa NMB aliyekamilisha mchakato wa kufungua akaunti ya mshindi huyo na kuingiza pesa zake. 

Akizungumza kwa furaha kubwa, mshindi huyo alisema ndio kwanza amemaliza kidato cha sita na kuibukia kwenye fedha hizo za Biko, hivyo anaamini zitamkomboa kiuchumi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba maisha yake yanakuwa mazuri.

Monday, June 12, 2017

Kompyuta nane za Bayport zatua mkoani Tanga

Na Mwandishi Wetu, Tanga
TAASISI ya Kifedha ya Bayport Financial Services, imekabidhi kompyuta nane katika wilaya za Handeni, Korogwe, Muheza na Pangani zote za mkoani Tanga, ikiwa ni mwendelezo wa msaada wa kompyuta 205 zenye thamani ya Sh Milioni 500 kwa ajili ya ofisi za serikali nchini Tanzania, huku mpango huo ukiasisiwa mwishoni mwa mwaka jana.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, William Mwakufwe aliyeshika sehemu ya kompyuta akiwa na Mratibu wa Masoko wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa wa pili kutoka kulia pamoja na Meneja wa Bayport Handeni, Candy Masunzu. Kushoto ni Afisa Utumishi wa Wilaya ya Handeni, Noel Abel katika tukio la kupewa msaada wa kompyuta mbili kutoka Bayport wiki iliyopita wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Utaratibu wa makabidhiano ya kompyuta hizo ulianza Handeni Jumatatu ya Juni 5, huku wilaya ya Korogwe wakipokea Juni 6, Muheza Juni 7 kabla yakumalizia Pangani Juni 8, ambapo kila wilaya ilipokea kompyuta mbili kwa ajili ya kupunguza changamoto ya vifaa vya kiutendaji katika ofisi za umma.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Korogwe, George Nyalonga mwenye koti jeusi naye akipokea kompyuta mbili kutoka Bayport wiki iliyopita.

Akizungumza mjini Tanga katika makabidhiano hayo, Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, alisema ni furaha yao kuona mpango wao wa kutoa kompyuta kwa ofisi za umma unaendelea vizuri kwa Mkoa wa Tanga kufikiwa na msaada huo.

Sunday, June 11, 2017

Mkazi wa Mbezi Makonde jijini Dar es Salaam aibuka na Milioni 20 za Biko

Balozi wa Biko Tanzania, Kajala Masanja kulia akiwa kwenye majukumu ya kumtafuta mshindi wa droo ya 13 ya Biko ambapo kijana mwenye miaka 23 mkazi wa Mbezi Makonde, jijini Dar es Salaam, Amani Kabuku, alifanikiwa kuibuka na zawadi nono ya Sh Milioni 20. Kushoto ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
DROO ya 13 ya Biko waendeshaji wa mchezo wa kubahatisha Tanzania maarufu kama ‘Ijue Nguvu ya Buku’, imefanyika leo asubuhi, huku mkazi wa Mbezi jijini Dar es Salaa, Amani Kabuku, mwenye miaka 23, akifanikiwa kuibuka na ushindi mnono wa Sh milioni 20.

Mshindi huyo ameibuka katika droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es Salaam na Balozi wa Biko, Kajala Masanja, kwa kushirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.

Akizungumza katika droo hiyo leo asubuhi, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage, alisema ni wakati wa kutajirika kwa kupitia mchezo wao wa Biko uliozidi kujizolea umaarufu katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake nchini Tanzania.
Kajala Masanja kulia akizungumza huku akionyesha namba ya mshindi wa Sh Milioni 20 kutoka Mbezi Makonde, jijini Dar es Salaam baada ya kutangazwa mshindi katika droo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, huku akishuhudiwa na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.
Alisema anaamini washindi wao wanaoendelea kujipatia fedha mbalimbali kupitia mchezo wao, huku akiwataka Watanzania waendelee kucheza kwa kufanya miamala ya fedha kwenye simu zao za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money kwa kuanzia Sh 1,000, ambapo namna ya kucheza ni kuweka namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu 2456.

Friday, June 09, 2017

Mshindi wa Milioni 20 Arusha akabidhiwa mzigo wake

Na Mwandishi Wetu, Arusha
WAENDESHAJI wa Bahati Nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku, jana wamemkabidhi zawadi yake jumla ya Sh Milioni 20 mshindi wao wa Arusha, Oscar Haule, huku wakijigamba kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwakwamua washiriki wao kwa kuwapa fedha zao haraka ili waziingize katika majukumu yao ya kiuchumi.
Mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko Oscar Haule mwenye fulana nyekundu akipokea hundi yake ya ushindi kutoka kwa Balozi wa Biko, Kajala Masanja. 
Mbali na kumpa zawadi hiyo ya fedha taslimu mshindi huyo, Biko pia wametangaza kutoa jumla ya Sh Milioni 500 kwa washindi wao waliocheza Biko mwezi Mei.
 
Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mkurugenzi wa Biko Tanzania, Charles Mgeta, alisema wanaamini kuwa kiasi cha pesa walichompa mshindi wao atazitumia vizuri katika kujiletea maendeleo kama ilivyokuwa dhamira ya kucheza Biko na kufikia kutoa Sh Milioni 500 kwa washindi wa mwezi Mei.
Mkurugenzi Mtendaji wa Biko Tanzania, Charles Mgeta kulia akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa Milioni 20 wa Biko droo ya Jumatano Oscar Haule wa jijini Arusha mwenye fulana nyekundu.

“Tunampongeza Haule kwa kushinda donge nono la Sh Milioni 20 kutoka Biko katika droo iliyochezeshwa juzi Jumatano, sambamba na kuwapongeza wote wanaocheza mchezo huu kwa njia ya ujumbe wa maandishi kwa simu zao za Tigo, Vodacom na Airtel kwa kufanya miamala kwenye simu zao kwa kuingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu ikiwa ni 2456,” Alisema Mgeta.

Mvua haijazuia kompyuta za Bayport kusambazwa mikoani

Mratibu wa Masoko wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa akimkabidhi kompyuta mbili Kaimu Mkurugenzi wa Mbulu, mkoani Manyara, Deogratias Kashasha.


Na Mwandishi Wetu, Mbulu
KWA miezi kadhaa sasa mvua imeendelea kunyesha katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, hali inayoonyesha kukidhi kiu ya watu wengi waliokuwa wakiiomba inyeshe katika maeneo yao.

Hata hivyo, licha ya mvua hiyo kunyesha, lakini baadhi ya maeneo imekuwa na matokeo mabaya kutokana na kuezua nyumba, kuharibu miundo mbinu muhimu ikiwamo ya barabara.

Matokeo hayo yameibua changamoto mpya hususan za kufikika kwa urahisi katika maeneo hayo yanayoendelea kukumbwa na mvua kubwa. Mbali na mvua hiyo kunyesha, hata hivyo uwajibikaji unaendelea kufanyika kwa sekta na watu mbalimbali kuendelea na maisha yao ya kila siku ili wakuze uchumi.
Zoezi la kutoa msaada wa kompyuta lilivyokuwa linaendelea katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.


Licha ya maeneo mengi kukumbwa na mvua, lakini Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services imeendelea na usambazaji wa kompyuta katika ofisi za serikali mikoani kama ilivyozindua utaratibu huo mwishoni mwa mwaka jana.

Bayport ambayo ni Taasisi ya Kifedha inayojihusisha na mikopo ya fedha, mwaka jana ilianzisha mpango wa kusambaza kompyuta kwenye ofisi za serikali ambapo tukio la uzinduzi lilihudhuliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki. Jumla ya kompyuta ambazo Bayport iliamua kuzisambaza kwa serikali ni 205, ambapo tayari maeneo mbalimbali wamefikiwa na kompyuta hizo kwa ajili ya kupunguza changamoto ya vifaa vya ofisi.

Akizungumza katika usambazaji wa kompyuta kwenye mikoa ya Singida, Manyara, Iringa, Songwe na Ruvuma, Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, anasema licha ya mvua kubwa kupiga, lakini wameendelea na zoezi lao la kuhakikisha wanafikisha msaada wa kompyuta.

Wednesday, June 07, 2017

Mkazi wa Arusha Oscar Haule aibuka na Milioni 20 za Biko

Balozi wa Biko Tanzania Kajala Masanja akionyesha namba ya ushindi wa Sh Milioni 20 aliyopata mkazi wa Arusha, Oscar Haule, katika droo iliyochezeshwa leo jijini Dar es Salaam.



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

DROO ya 12 ya Bahati Nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’ imechezeshwa leo asubuhi, huku ikimpata mshindi wake wa nonge nono la Sh Milioni 20 ikiwa ni maalum kwa Jumatano hiyo kutoa mshindi wa Sh Milioni 20 ambapo mkazi wa Arusha, Oscar Haule kuibuka kidedea kwa kuzoa mamilioni hayo.


Donge nono hilo limekwenda kwa mshindi huyo wa Arusha, ikiwa ni mwendelezo wa kutoa mamilioni katika zawadi mbalimbali za bahati nasibu huyo inayoanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja kwa zawadi za hapo hapo huku droo kubwa ya Jumatano na Jumapili hii pia itatoa Sh Milioni 20 kama Jumatano mbili zilizopita.
Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akichezesha droo ya 12 ya Bahati Nasibu ya Biko, ambapo mkazi wa Arusha, Oscar Haule alitangazwa mshindi wa donge nono la Sh Milioni 20. Kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid.

Akizungumza leo asubuhi katika uchezeshaji wa droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwamba ni wakati wa kushinda mamilioni ya Biko kwa kuchezesha bahati nasibu yao rahisi na yenye nafasi kubwa ya ushindi wa zawadi za papo kwa hapo na zile za wiki zinazotoa mamilioni kwa droo ya Jumatano na Jumapili.


Alisema hadi sasa zaidi ya washindi 55,000 wameshinda zawadi kutoka Biko, huku wakiamini kuwa Biko ni chanzo cha mapato na kinachoweza kubadilisha maisha ya washindi wao wanaoamua kujitokeza kwa wingi kuwania mamilioni kwa kupitia mchezo huo.
Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akichezesha droo ya 12 ya Bahati Nasibu ya Biko, ambapo mkazi wa Arusha, Oscar Haule alitangazwa mshindi wa donge nono la Sh Milioni 20. Kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid.

Monday, June 05, 2017

TPDC yaibuka mshindi wa tuzo ya Banda Bora sekta ya Nishati na Mazingira

Waziri wa Malisili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe kushoto akimkabidhi  Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale tuzo ya mshindi wa banda bora la sekta ya nishati na mazingira katika maonyesho ya Kimataifa ya Biashara wakati alipokwenda kuyafunga kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella.
 Waziri wa Malisili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe kushoto akifurahia jambo na  Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale mara baada ya kumkabidhi tuzo ya mshindi wa banda bora la sekta ya nishati na mazingira katika maonyesho ya Kimataifa ya Biashara wakati alipokwenda kuyafunga kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella.

Dau nono la Milioni 10 za Biko laenda kwa Junior Pesambili wa Makete

Jumatano hii mwingine kuzoa Milioni 20 kwa droo ya 12, cheza sasa ushinde
Balozi wa Biko Tanzania, Kajala Masanja, kulia akionyesha namba ya ushindi wa Sh Milioni ya mshindi wao wa Lupela, Makete,mkoani Njombe, Junior Ashery Pesambili aliyepatikana katika droo ya jana Jumapili. Kushoto ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
DAU nono la Sh Milioni 10 linalotolewa kama zawadi ya droo kubwa ya Mchezo wa Kubahatisha wa Biko limeenda kwa Junior Ashery Pesambili wa Lupela, Makete, mkoani Njombe, ikiwa ni mwendelezo wa kugawa fedha kwa washindi wake ikitokana na matokeo ya droo ya 11 iliyochezeshwa jana Jumapili.
Balozi wa Biko Kajala Masanja akifurahia namba ya mshindi wa Sh Milioni 10 kutoka Makete, mkoani Njombe, droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es Salaam.

Droo hiyo iliyochezeshwa jana iliendeshwa na Balozi wa Biko Kajala Masanja, akishirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid. Akizungumza katika droo hiyo jana, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage, alisema wamedhamiria kugawa mamilioni kwa washindi wao wanaocheza mchezo wa Biko uliozidi kushika kasi katika kona mbalimbali nchini Tanzania.

Thursday, June 01, 2017

Grace Kisetu, Mkuu wa Idara ya Ijenzi wa Nguvu Pamoja wa TGNP Mtandao, akizungumza na washiriki katika warsha ya Uongozi wa Kijinsia kwa Madiwani wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Zijue mbuga za wanyama unazoweza kutembelea bure mwishoni mwa wiki hii

Na Jumia Travel Tanzania
Siku ya Jumatatu ya Juni 5 itakuwa ni maadhimisho ya ‘Siku ya Mazingira Duniani’ ambayo huadhimishwa na mataifa tofauti duniani ikiwa imebeba kauli mbiu ya ‘Kuwaunganisha Watu na Mazingira Asilia.’ 
Mapema wiki hii Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, Mh. January Makamba  alitoa taarifa kwa umma kuwa kwa hapa nchini maadhimisho ya siku hiyo kitaifa yatafanyika kijijini Butiama mkoani Mara, mahali alipozaliwa mwasisi wa taifa la Tanzania, Hayati Mwl. Julius Nyerere, ikiwa ni kuenzi jitihada zake za kulinda na kuhifadhi mazingira.

Milioni 20 za Biko zatua kwa Huruma Mkongwa wa Arusha


Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akisalimiana na Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Bakari Maggid kabla ya kuanza kuchezesha droo ya 10 ya Jumatano ya Sh Milioni 20 ambapo mkazi mwingine wa Arusha, Huruma  Mkongwa aliibuka kidedea.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
DROO ya kwanza ya Sh Milioni 20 na ya kumi kufanywa na waendeshaji wa bahati Nasibu ya Biko hatimae imepata mwenyewe baada ya kutangazwa mshindi wake ambaye ni Huruma Mkongwa wa jijini Arusha, akiibuka kidedea katika droo iliyochezeshwa jana, jijini Dar es Salaam.

Droo hiyo ni ongezeko la Sh Milioni 10 ambapo hapo awali droo zote zilikuwa zikihusisha kiasi hicho cha pesa kabla ya kuongezwa katika droo ya Jumatano ambapo waliongeza Milioni 10 nyingine hivyo kufikia Sh Milioni 20 na hivyo kutua kwa Mkongwa.
Balozi wa Biko Kajala Masanja akimtangaza mshindi wa Sh Milioni 20 Huruma Mkongwa kutoka mkoani Arusha baada ya kumaliza kuchezeshwa droo hiyo ya 10 ya Biko. Kushoto ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Bakari Maggid.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa kuchezesha droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema Jumatano ya Sh Milioni 20 imekuwa tamu baada ya fedha hizo za zawadi ya juu kabisa kutoka kwenda kwa  Mkongwa ambapo anakuwa mshindi wa kwanza kuzoa kiasi hicho cha pesa kutoka kwenye bahati nasibu yao inayotikisa nchini.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...