https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, August 11, 2013

Tamasha kubwa la burudani la Fiesta kuzinduliwa mkoani Kigoma Agosti 17 mwaka huu na kudondoshwa shoo ya aina yake


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
TAMASHA la burudani la kila mwaka linalojulikana kama Fiesta, limepangwa kuanza kutimua vumbi Agosti 17 mwaka huu, huku likianzia mkoani Kigoma na wasanii mbalimbali kutarajiwa kupanda jukwaani.
Mkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, pichani.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, ambao ndio waandaaji wa tamasha hilo, alisema tamasha hilo litafanyika Kigoma kwa mara ya kwanza.

Alisema lengo la kupeleka tamasha hilo mkoani Kigoma ni kupanua wigo wa kiburudani, sambamba na kutafuta fursa kwa Watanzania wote, hasa mkoani Kigoma kwenye changamoto lukuki.

“Kigoma kuna fursa nyingi lakini zinashindwa kuonekana, hivyo hili ni jambo ambalo sisi Clouds tumeamua kuanzia Fiesta huko kwa ajili ya kushirikiana na wadau kusaka maendeleo ya wananchi wote.

“Ukiacha Fiesta, lakini pia tutakuwa na ule mpango wa semina za ‘Twenzetu’, huku tukiamini kuwa mambo yatakuwa mazuri kwa kuhakikisha kuwa watu wanafanya harakati za kimaisha,” alisema.

Mara baada ya kuzinduliwa rasmi mkoani humo, tamasha la Fiesta litaendelea katika mikoa kdhaa ya Morogoro, Mwanza, Shinyanga, Tanga, Arusha, Iringa, Mbeya na kwingineko.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...