https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 30, 2011

Wakali wa Ulaya walivyotoana jasho







MICHUANO ya klabu Bingwa Ulaya iliendelea tena Jumanne na Jumatano katika viwanja mbalimbali barani Ulaya.

Katika mechi za Jumanne Manchester United ikiwa nyumbani ilitoka sare ya mabao 3-3 na Basel FC ya Uswisi.
Dany Welbeck alipachika mabao mawili ya haraka dakika ya 16 na 16……………., lakini Fabian Frei alifunga bao kipindi cha pili kabla ya kaka yake, Alexander Frei akufunga mengine mawili na kuwaweka mbele, lakini Ashelay Young alisawazishia United.

Mechi nyingine ilikuwa ni kati ya Bayern Munich dhidi ya Man City katika Uwanja wa Allianz Arena, ambapo mabao mawili ya Mario Gomez yaliilaza City.
Trabzonspor walitoka sare ya bao 1 – 1na  Lille, Real Madrid wakiwa nyumbani waliichapa Ajax mabao 3 – 0 yakifungwa na Ronaldo, Kaka na Karim Benzema.

Otelul Galati wa walifungwa na Benfica nyumbani bao 0-1,  Napoli          waliishinda mabao 2 – 0 dhidi ya Villarreal,
Lyon wakaibanjua 2 - 0 Dinamo Zagreb na Inter Milan waliifunga CSKA Moscow 2 – 3.

Kwenye mechi za Jumatano Chelsea walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Valencia, bao la Chelsea lilkuwa la kwanza likifungwa na Frank Lampard kabla ya  Soldado kusawazisha kwa penalty.
Arsenal ambao msimu huu wamekuwa hawapewi nafasi kubwa kutokana na kuanza vibaya kwenye Ligi ya England, wameichapa Olympiacos mabao 2-1, bao la kwanza lilifungwa na Alex  Oxlade-Chamberlain dakika ya 7 na la pili lilipatikana dakika ya …………………………….. Andre Santos (19),  David Fuster aliipatia timu yake bao la kufutia machozi dakika ya 26.

Shakhtar Donetsk walitoka sare na 1 – 1 Apoel Nicosia, Marseille          waliichapa mabao 3 - 0   Borussia Dortmund, Bayer Leverkusen ilishinda 2 – 0 dhidi ya Genk na Zenit St Petersburg waliizamisha FC Porto mabao3 – 1.

BATE walikula kichapa cha mabao 5 –0 kutoka kwa Barcelona, mchezaji wa BATE alianza kujifunga dakika za mwanzo, Messi aliweka nyavuni mara mbili, Pedro na Villa kila mmoja akifunga moja.
AC Milan waliifunga 2 - 0    Plzen, Ibrahimovic na Cassano waliipatia ushindi huo klabu hiyo yenye makazi yake San Siro.

Sumalee mdheee wa Hakunagaaa


HAKUNAAGA zaidi yangu mi na wewe, hakunaaga zaidi yangu mi na wewe, hakunaaga zaidi yangu mi na wewe, hakunaaga zaidi yangu mi na wewe, hakunaaa, hakunaga, hakunaaa hakunaga.
Hiko ni kiitikio cha wimbo mpya wa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Suma Lee, uitwao Hakunaga, kibao ambacho kimepigwa katika mahadhi ya kwaito.
Wimbo huo tayari umeanza kuwabamba mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva na kupata Air Time katika vituo mbalimbali vya redio, huku video ya wimbo huo ukifanya vizuri pia.



Sumalee akiwa katika picha tofauti...
Sasa mkali huyo anatamba na wimbo wake wa 'Hakunaga'
Msanii huyo alianza masuala ya muziki kwa mara ya kwanza mwaka 2000 na moja kwa moja akaingia studio na kutoa wimbo ulioitwa Sivuti na Mama, akiwa na kundi la Parklane lililokuwa na makazi yake mjini Tanga.
Hakuweza kufanya muziki kabla ya hapo kwa kuwa familia yake haikuwa tayari kumuacha ajiingize katika masuala hayo, lakini muda ulipofika yeye mwenyewe aliamua liwalo na liwe.
Ingawa hakuwahi kufanya muziki kabla ya hapo, lakini aliweza kuingia studio, ambapo mwaka huo waliweza kutoa wimbo mwingine uitwao Aisha, wakati huo C Pwaa alikuwa amejiunga na kundi hilo la Parklane.



Baada ya Parklane kusambaratika, wasanii waliounda kundi hilo kila mmoja alijishughulisha na muziki binafsi.
Suma Lee, ambaye jina lake halisi ni Ismail Thabit, aliyezaliwa Tanga katika Hospitali ya Mkoa ya Bombo, mwaka 2006 alitoka kivyake na kibao kiitwacho Chungwa.
Wimbo huo uliweza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio, huku ikishika katika chati za vituo hivyo vya redio hapa nchini na nje ya mipaka yetu.
Suma alitoa albamu ambapo wimbo huo wa Chungwa ndio ulibeba jina la albamu, zikiwemo nyimbo nyingine kama Rafiki, Chaguo Lake, Gomba na Ba na Ma.
Kutoka kwa kibao cha Hakunaga ni maandalizi ya albamu yake mpya baada ya ile ya kwanza ya Chungwa.
Albamu hiyo mpya itakayoitwa Hesabu za Mapenzi itakuwa na nyimbo 15, ukiwemo wimbo mkali uliofanya vizuri mwaka 2009 uitwao Ndani One Week.
Katika albamu hiyo mpya kutakuwa na nyimbo kama
Nikueleze, Uk Dubai, Aunt na Hakunaga pamoja na Ndani One Week ambazo tayari ameshaziachia.
Suma Lee amekuwa na utaratibu wa aina ya pekee tofauti na wasanii wengine, kwani huchukua muda mrefu hadi kutoa ‘single’ moja hadi nyingine.
Singo ya mwisho Suma Lee kutoa ilikuwa ni Ndani ya One Week, ambayo ilikuwa mwaka 2009 na kufanya vizuri, hivyo ni takribani miaka miwili imepita ndio ametoa Hakunaga.
Akitoa sababu za kuchelewa kutoa singo baada ya kutoa moja, amesema huo ni utaratibu wake, kwani akifanya haraka mashabiki wake watamchoka kama wanavyochokwa wengine.
“Wimbo wangu mmoja ukiusikiliza leo, ndivyo utakuwa na utamu ule ule utakapousikia tena baada ya miaka 10 kupita,” anasema nyota huyo.
Tangu msanii huyo aanze muziki kwa mara ya kwanza mwaka 2000 hadi leo 2011 ni miaka 10 imepita, lakini bado ameonyesha uwezo aliokuwa nao zamani.
Ni miaka 10 sasa tangu aanze sanaa, lakini bado uwezo wake wa kutunga mashairi na kuimba ni wa kipekee na ndiyo maana anaweza akakaa miaka miwili bila ya kutoa wimbo na akija kutoa unakuwa mkali.
Kwa sasa Suma Lee ana mpango wa kutafuta vijana wenye sauti za ukweli na wenye uwezo wa kuimba na kuweza kuinua vipaji vyao.
‘Project’ hiyo ya kuibua vipaji na kuviendeleza ameipa jina la Voice of Suma, ikilenga wale wasanii wadogo wenye sauti nzuri na uwezo wa kuimba kama yeye.

Mjuwe Marlaw kifaa cha Besta





Marlaw akiwa na Bestaaaa


BABA mwimbaji, mama mwimbaji – tazama familia hii, kama atapatikana mtoto itakuwaje?
Swali kama hilo pia unaweza kujiuliza kuhusu Beyonce Knowles na mumewe Shawn Carter ‘Jay-Z’.
Lakini, katika jukwaa la muziki wa Tanzania, hasa wa kizazi kipya, naizungumzia familia iliyoanzishwa na Marima Lawrence na Besta Rugeiyamu.
Wawili hao ni wanandoa na pia ni waimbaji mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, wakati mume akijulikana vyema na mashabiki wake kama Marlaw na mke akitambulika kwa jina la Besta.
Unadhani akipatikana mtoto kwenye familia hiyo atarithi kitu gani? Kwa haraka utasema ni muziki, na kuzitazama kama familia ya Will Smith na mkewe Jada Pinkett – ambao watoto wao, Jayden na Willow, wanatesa kwenye muziki na filamu kama ilivyo kwa wazazi wao.
Mkali huyo alitupasha kuwa yote juu ya ndoa yake na masuala mazima ya muziki.
Tanzania inamtambua Marlaw kutokana na kujishirikisha na sanaa ya muziki, lakini malengo ya mwimbaji huyo ni kuufikisha mbali muziki wake, ikiwa pamoja na kutambulika katika bara zima la Afrika.
Wakati akiwa na fikira hizo, Marlaw anatambua ujio wa waimbaji wapya ambao wanaongeza ushindani katika tasnia hiyo hapa nchini.
“Kuongezeka kwa wasanii kunazidisha ushindani na kuibua changamoto mpya katika muziki,” anasema.
Muziki umekuwa ni sehemu ya maisha kwa msanii huyo, tofauti na ilivyokua mwanzo wakati anaanza kufanya kazi hiyo.
Marlaw, ambaye alikuwa msanii kutoka Tanzania House Of Talent (THT), alijiunga katika jumba hilo la vipaji kwa ajili ya kujiongeza ujuzi zaidi baada ya kuachia kibao chake cha Bembeleza mwaka 2007.
Marlaw alijifunza mambo mengi THT, ukiachilia uimbaji, pia aliweza kujifunza namna ya ‘kuperform’  na bendi ‘live’.
Baada ya kuachia Bembeleza, msanii huyu alikaa kimya kwa muda akijipanga upya na kuachia nyimbo nyingine kibao kama Rita, Daima na Milele, Bado Umenuna aliyomshirikisha Chid Benzi na Pii Pii (Missing my Baby).
Marlaw anatamba katika soko la muziki na albamu zake mbili ya kwanza ikiwa ni Bembeleza na ya pili ni Bidii.
Albamu ya Bembeleza iliitoa Septemba (2007) ikiwa na nyimbo (12), ambazo ni Bembeleza, Rita, Bado Umenuna, Daima na Milele, Busu la Pink, Si mimi.
Wakati ile ya Bidii iliyoitoa Septemba (2009) ilikuwa na nyimbo 12 pia,  zikiwemo Pii Pii (Missing my Baby), Sorry Sana, Be Happy na Tanzania.
 Msanii huyo alikutana na mkewe, Besta kwenye muziki wakawa na uhusiano, huku wakiendelea na tasnia hiyo hadi walipoamua kufunga ndoa ili kuwa mke na mume.
Akizungumzia juu Serikali kusaidia sanaa hiyo ya muziki, Marlaw anasema kuwa iko tayari kusaidia na ndio maana imeanza na msaada wa studio ya ‘mastering’, kitu ambacho ni muhimu sana kwa kazi zetu.
Pia alizungumzia muziki wa nje na ule wa kwetu akisema muziki wa nje una maendeleo mazuri, kwa kuwa wana mifumo madhubuti kwenye pande zote za haki ya sanaa kuanzia usambazaji wa kazi, haki miliki na hata matumizi ya sanaa kiujumla.
Kwa sasa unapomzungumzia Marlaw ni kama unauzunguzia muziki, kwa sababu chakula chake anakipata kutokana na kufanya muziki, makazi yake anayolala yanatokana na ujira anaopata kwenye muziki, lakini kubwa kwenye mapenzi – mkewe ni mwimbaji.


Sinta kubali mama weeee, ehee





 Sinta akiwa katika pozi bomba mbayaaaaaaaaaa. Huyu kweli ni malkia na anastahili kuitwa mrembo.
Chini ni ujumbe wake mzito kwa mashabiki wake wooote kwenye mtandao wa facebook na yaliyofuata ni maoni na ushauri wa marafiki zake haooo.

Kikweli handenikwetu.blogsport.com inatamani kuona wawili hao wanacheza movie hiyo ambayo kwa mujibu wa meneja wa Sinta, Richard Mathew, wawili hao wanaelekea makubaliano.

Christine Sintah
hi Sintah's fans,baada ya miaka 9 siongei na hatupikiki chungu kimoja na Nature unafikiri, ninaweza kusamehe yaliyotokea na kufanya nae kazi ya movie na ikaenda platinum?pse comment KISTAARABU
LikeUnlike · · Wednesday at 7:41am via BlackBerry · Privacy:Shared with: Christine's friends

     
            Emilian Lyimo samehe mtoto mbona hata mm ulinisamehe tupilia mbali issue tofauti
            Wednesday at 9:17am · LikeUnlike
            Mary Misoji Ng'oboko Kusamehe ni muhimu mamy katika maisha maana kwanza utakua umeutua mzigo fulani mkubwa moyoni... hata maandiko ya mungu yanatusisitiza msamaha....Kama ni kazi tu fanyeni ila ule ukaribu kama zamani usiwepo... ukaribu wenu ni wakati wa kazi t

            Wednesday at 9:17am · LikeUnlike
            Martin Josephat Kwanza mtakapo fanikiwa ukiigiza hiyo Movie mtakuwa mmewasaidia wale wote ambao wanavibifu visivyo na maana na kujiona wanachofanya ni ujinga tu na mwisho wa siku wenda mambo kama hayo yakapungua na kama si kuisha kaisa!
            Wednesday at 9:21am · LikeUnlike · 1 personLoading...

            Fadhil Ally
            SINTAH samehe kama binadam na sio sababu ya mapenzi au kazi coz kama mapenzi yalishakufa na kama makosa wote mlifanya n kumbuka NATURE ni celebrity than you, so swala kusameheana ni swala la kibinadam na sio u celebrity, mapenzi au ela, bad...o ujamaliza maisha u never know what wil happen 2mr...... Sisi wazawa wa TEMEKE atuna kinyogo coz tupo fasta kusahau na kusamehe, so NAAMINI nature ashasamehe yupo busy na kazi zake kama ulivyo wewe, achana na washamba wa maisha wanaokupa mawazo ya kitoto waambie sijui nini kesho kitatokea mbele then watajua binadam ni nani,See More
            Wednesday at 9:21am · LikeUnlike

            Verdiana Mathias Mimi nafikiri msamaha wa kwl unatoka ndani ya nafsi ya m2,haitaji mawazo ya wa2 wa pembeni,jee km wa2 wote wakisema ucmsamehe so hutomsamehe?lbd uliza km jee ufanye nae kazi,lkn dini ye2 inasema samehe 7mara70 hamna mkamilifu duniani
            Wednesday at 9:22am · LikeUnlike

            Nelson Karabwe Mie nadhani hilo niwazo zuri sana Sinta.Kweli kusamehe ni jambo muhim sana kusamehe jambo jema Sinta,MPE ISSUE BRO.Wala sikosa kuuliza wadau kwani humu ndani sio tangazo kama gazetini.
            Wednesday at 9:23am · LikeUnlike

            Idd Minani Hey sinta forgive and forget there u will release ur self from anger and strases dont try to rise the dead u have to let it go
            Wednesday at 9:29am · LikeUnlike

            Olivia Sanare-mwanaharakati Hehehehehe siku ya kwanza kukutana nae alikuja kwetu usikuuu,HAKUNA KUMSAMEHE ANATAFUTA PAKUANDIKIA MISTARI MINGINE TWIN HANA NYIMBO CKU HIZI.
            Wednesday at 9:31am · LikeUnlike · 1 personLoading...

            Sarah Albert Sintah dear samehe ufanye kazi, yaliyopita c ndwele mama
            Wednesday at 9:34am · LikeUnlike

            Bobson'dozen Julius itapendeza sana coz mlikua mnapendezana sana akuna mahusiano yaliyotokea kupendwa kama yenu coz yalikua ya kwanza ya msanii kudat na msanii
            Wednesday at 9:36am · LikeUnlike
 

         Kaka Ommy kama kuna aliekushauri juu ya hili mpe pongezi sana na kama ni akili zako ongera nyingi,ilo ni la kulifanyia kazi mazima sio mda wa mabiifu huu ni amani na kusaka hela tu
            Wednesday at 9:40am · LikeUnlike · 2 peopleLoading...

            Vicent Mgunda Igosha Huwezi jua kesho wenda akaoa mtoto wako samehe tu ilikuwa utoto sintah
            Wednesday at 9:47am · LikeUnlike

            Okot P'Bitek iTAKUWA POA SANA CAUSE KILA M2 ATAMUHESHIM MWENZIE SAHAU FANYA KAZ YALIYOPITA YAMEPITA!
            Wednesday at 9:52am · LikeUnlike

            Aysha Nyange Kiukwe sintah mi cdhani km cns dat tym mpk leo huongei nae kunachochote kimekuathir au laah' bc jua ht ukimsamehe it will b da same nothing change.. Ckiliza moyo wako zn fanya maamuz my dia.. Wt evr ur decition is' it will b u mamaa....
            Wednesday at 9:56am · LikeUnlike

            Bakari Hemed km uwez kusamehe itakua ngumu kupata msamaa, jifunze kupitisha msamaa km maji kwenye mto.
            Wednesday at 10:15am · LikeUnlike

            Faraji Said Kemea pepo lakinyongo linalokusumbua.
            Wednesday at 10:16am · LikeUnlike

            Chris Kaoneka Mjomba Oliver Nakumbuka the First time huo wimbo unapigwa Nilikuwa na Mjomba Tina kwenye Gari alilia sana...! Venture alimtumia sms akamwambia kuna wimbo sikiliza...! Umenikumbusha Mbali sana...! Hahaha...! Tinah Samehe tu Mjomba...! Yameisha fanya kazi iwe tu ina hela ndefu...!
            Wednesday at 10:20am · LikeUnlike

            Samson Simbeye jaman kuna gazeti1 la udaku limetoka leo lasema kwamba hao watu now wapo pamoja na tofauti zao zimeshaisha so tueleweje?
            Wednesday at 10:25am · LikeUnlike

            Saida Salum My dear just follow your heart.
            Wednesday at 10:28am · LikeUnlike

            Ezekiel Noah Leo tumia status hii kujua maadui zako na ambao hawakutakii mema,utaona wanafiki wote wasiokupenda watakwambia usimsamehe na kukumbushia machungu achana nao kwani hata huku kwetu wapo wapotezee. samehe fanya kazi na Kibra itakujengea heshima na utaonekana umekomaa!hebu angalia comment za fans wengi wanapenda umsamehe nina imani utafanya hivyo.
            Wednesday at 10:31am · LikeUnlike

            Jacqueline Mwibule samehe my dia km Mungu husamehe kwanini wewe????wala hakukupunguzii kitu bali kinakuongezea amani zaidi...so u shld 4get..
            Wednesday at 10:38am · LikeUnlike

            Adam Tibaigana Sinta kumbuka kila Binadamu ana mapungufu yake na pia Binadamu tumeumbwa kusahau mfano Sinta ukienda kilioni ukakuta mtu aliefiwa na mama yake anavyolia na khali aliyonayo kwa mawazo ya halaka huwezi amini kuwa mtu huyo ipo siku atakuja kusahau nakucheka. Hivyo sahau yaliyopita kwani kumbuka wakati yanatokea yale fikiria na umri muliokuwa nao ujana ndo ulichukua nafasi yake. SINTA FANYA KAZI NAE SAHAU YALIYOPITA.
            Wednesday at 10:44am · LikeUnlike

            Emmanuel Kimori Msamehe sintah,maandiko yanarema samehe mara 70,wewe msamehe bure. Mungu ndie wa kukulipa wewe kwa msamaha utakaoutoa c binaadamu.
            Wednesday at 11:00am · LikeUnlike

            Johari Luwembas Madua ndio kwa nini usiweze kusamehe ni dalili ya uungwana dadito
            Wednesday at 11:15am · LikeUnlike

            Ruben Mwakilima A
            Kama ni siku njema basi imefika maana HIYO NDIO KAULI NZURI ZAIDI KUISKIA IKIMAANISHA MUDA WA MABADILIKO, TIME TO CHANGE BECAUSE HAKUNA ADUI WA MILELE NA HAKUNA BINGWA WA MILELE NA HAKUNA ASIYE SAMEHE MILELE NA HAKUNA ASIYEKOSEA MILELE.... ...u nani usitake samehe? Mangapi UMEKOSEA MPAKA LEO KWA WENZIO NA BINADAMU YOYOTE? Wakati huu dada PESA NA UTU PAMOJA NA UBINADAMU MBELE... fanya Kazi NAYE (NATURE) na HEBU KAA NAYE OBE TABLE ONE SEAT NA MSHIKE MKONO ILI KAZI IWE POUA INGAWAJE USIFANYE AKAZANI UMEJIPENDEKEZA ILA MAELEWANO NA MAKUBALIANO MAANA NASI WABONGO HATUNA DOGO.... DHAMBI PIA KAMA UNAMCHUKIA MTU KWA MUDA MREFU SANA.... rudisha kiwango kwa UBAO MPYAAA MAANA PIA ITAUZA SANA HIYO... ujue ukweli ukimpenda sana DADAA AKAKUACHA "INAUMA SANA" alf Kama MZURI NDIO LAAAAAAAAAH ,WE JIANGALIE UTAGUNDUA ROHO INAUMAJE,LOVE HEALS ALSO... not only FOR PARTNERS BUT LOVE FOR ALL HEALSSee More
            Wednesday at 11:23am · LikeUnlike

            Mgaza Kossey kiukweli muda ule uliopita ulikuwa unaboa kila siku sinta sinta...may be unaweza kuanza upya na watu wakakupa shavu kiaina tofauti na zamani...jaribu kuanza upya hujachelewa!!
            Wednesday at 11:37am · LikeUnlike

            Fadhil Ally Uliyoyataka yameshaandikwa kwenye gazeti tayari, @sintah
            Wednesday at 11:41am · LikeUnlike

            Fadhil Ally Uliyoyataka yameshaandikwa kwenye gazeti tayari, @sintah
            Wednesday at 11:41am · LikeUnlike

            Fadhil Ally Uliyoyataka yameshaandikwa kwenye gazeti tayari, @sintah

            Isha Salum yaah....inawezekana mamtooo..ilikua zaman na sio ss.yaliyopita c ndwele angalien ya mbele..but kikaz tu. na c vingnevyo..sawasawa
            Wednesday at 11:45am · LikeUnlike

            Fadhil Ally Uliyoyataka yameshaandikwa kwenye gazeti tayari, @sintah
            Wednesday at 12:13pm · LikeUnlike

            Pamela Betabula mpz samehe yaliyopita kwanza hope umeshasahau yote maana ni muda sasa unajua ukisameheana na mtu unakuwa na amani sana fanya hiyo movie mpz itauza kishenzi
            Wednesday at 12:55pm · LikeUnlike · 1 personLoading...

            Leah Mafwenga uwiiii umenkumbusha mbali sana Christine Sintah jamani Rozana mhh angalia moyo wako unakuambia nini coz kusamehe kupo wangu
            Wednesday at 1:15pm · LikeUnlike

            Moses Killagane Dah yani nimekumbuka mbali sana enzi za SITAKI DEMU na INANIUMA SANA oooh my god.....heshimu maamuzi ya moyo wako si kuamua watakavyo watu wakati bado unaunia@sintah.
            Wednesday at 1:29pm · LikeUnlike

            Nancy Frank Samehe mara saba sabini kwani yule kaua itakua vizuri na utakua umefanya jambo la mbolea
            Wednesday at 2:00pm · LikeUnlike

            Sharifa Shafii ‎4gv and 4gt
            Wednesday at 2:12pm · LikeUnlike

            Albert Mganga Fanya kazi we mtoto achana na hizo maki2 coz deal kusaka mahela
            Wednesday at 2:32pm · LikeUnlike

            Albert Mganga Fanya kazi we mtoto achana na hizo maki2 coz deal kusaka mahela
            Wednesday at 2:45pm · LikeUnlike

            Kanju Ally mbona itakuwa full lmaisha nikusameheana tu na maisha mengine yanaendelea,hiyo k2 itabamba niaje me mwenywe lazima niitafute ni watch hiyo movie.
            Wednesday at 3:34pm · LikeUnlike

            Aniceth Tryphone Ngaiza Ynwa Yap unaweza nyote mmeshakua sasa mnajua nn kilitokea
            Wednesday at 4:29pm · LikeUnlike

            Sweetlips Bigkiss Sinta nakuomba ucheze hiyo movie kwani mimi ndiyo mmoja wapo wa watu tulioshirikiana na LAMATA kutoa mawazo hayo ya wewe kucheza movie na J. NATURE. N a mm ndiyo Location Manager wenu.
            Wednesday at 5:29pm · LikeUnlike

            Mwajuma Ndege Du hii kari nimekumbuka mbali sana tina but sshv umekua mamy yaliopita sindwele tugange yajayo itakua bomba wangu fanya kweli mdogo wangu mungu atakusimamia
            Wednesday at 5:40pm · LikeUnlike

            Lema Peter samehe tu yaliyopita si ndwele ganga yanayokuja
            Wednesday at 6:47pm · LikeUnlike

            Idd Minani
            Just let it go sinter have life countinue and move one with ur life never let past hold ur future people came to u and live u because his not joine in to ur body u must let him go and free ur mynd sinter his not part of ur body paty and it... ease to forgert abou him forgive and dont forget what hapen because that is memory ever single human have memory to remember if is good or bad that is how is it and that is fact u wont change See More
            Wednesday at 9:39pm · LikeUnlike

            George Kidubo what for bana hzo story za kzaman fanya ishu zngine za ukwel
            Wednesday at 9:48pm · LikeUnlike

            Kambi Mbwana Hakuna tatizo juu ya hilo, hivyo mnaweza kufanya kazi bila wasiwasi wowote.Naamini itakuwa ni film nzuri kupita kiasi, czwote mna vipaji na idadi kubwa ya mashabiki Tanzania. Sameheaneni, maana ndio ubinadamu huo.
            Wednesday at 11:08pm · LikeUnlike

            Leticia Thomas Pole mamii yaliyopita yamepita sahau fanya kazi
            Yesterday at 2:38am · LikeUnlike

            Leticia Thomas Pole mamii yaliyopita yamepita sahau fanya kazi
            Yesterday at 2:39am · LikeUnlike

            Irene Mkwizu Inawezekana kabisa my dear. Msamehe bure.
            Yesterday at 10:26am · LikeUnlike
          .
            Geko Jackson Kama kweli mkifanya kazi pamoja,hiyo movie ita hit sana bongo kwa sababu uhalisia utakuwepo
            4 minutes ago · Like

Wimbo wa kazi ya dukani





 Dogo Mfaume huyu akiwa katika pozi


Haiiii ya ya ya ya yaaaa ohoooo
Ohoooo yayaya ohoooo
Hii kazi yangu ya dukani mimi naona inalipa
Nikizingatia zitaweza filisika
Baba kabla ya kufa, alinipa usia
Mwanangu kazi ya kufanya fungua duka
Eheeeee funguu duka
Na ukizingatia hutaweza filisika
Sasa wanakijiji wamepanga wanitimuwe
Jamani ndugu zangu nipeni ushauri wa bure
Niache kuuza duka au nifuge nguruwe
Hiyo haiwezekanii
Hiyo ni tofauti tambi na mboga ya majani
Kama wanamuziki Yondo na Marijan
Yote mimi najua sababu demu wa Fulani
Yeye akija kwangu dukani
Analeta sana matani
Hii yote najua sababu demu wa fulani
Yeye analeta sana matanii
Anajiona yeye ndio bora
Mali hazina thamani
Kumbe hana lolote anataka kunilaghai
My Dogo mafi me Peace&Love
Yani namaanisha upendo na amani
Kaka mkanye mkeo atalala kwenye majani
Eheeeee kazi ya dukani mieeeeee
Naona inaniweka matatani


Kiitikio

Kazi yangu ya dukanii eheee inaniweka matatani
Ehee kazi yangu ya dukaniii ohooo inaniweka matatani
Eheee wanaonirudisha nyuma wengi wao majirani
Majiraniiii, wanaonirudisha nyuma wengi wao majiraniii
Majiranii, wanaonirudisha nyuma wengi wao majirani

Ubeti 2

Aiiiiiiii yayayayayayayayayaayayayaa ohooo
Ohoooooo, yayayaa ohooo
Yani kila kukicha mi naona masiara
Baada ya miezi sita sitakuwa na biashara
Sasa nimekata mtaji wangu wa sigara
Ilikuwa juzi mimi na bwana Sele
Alipokuja dukani nimkopeshe mchele
Anataka kilo mbili watoto wake wakale
Nitafanya nini mimi nitafanya nini
Naogopa kugombana na majirani
Nikitazama duka langu linakata
Siku zote hakuna ninachopata
Haina kulia mi nabaki tu kucheka
Kwani tayari duka lishafilisika
Na hivi sasa, nimeshachoka
Hivi sasaaa nimeshachoka
Zege nabeba, kokoteni nasukuma
Debe napiga shamba la mtu nalima
Yamenijaa moyoni nashindwa hata kusema
Ningekuwa nyoka sumu ningezitema
Marafiki wameshiriki, kunifilisi
Mpaka sasa wote mimi nawaona nuksi
Wameleta mikosi juu ya mikosi
Na kazi yangu ya dukani imeniweka matatani
Nikikumbuka mi napatwa na simanzi
Maumivu ya moyo hayapoi kwa ganzi
Hayaaa ohooo yayayaaaaa ohooo

Kiitikio

Kazi yangu ya dukanii eheee inaniweka matatani
Ehee kazi yangu ya dukaniii ohooo inaniweka matatani
Eheee wanaonirudisha nyuma wengi wao majirani
Majiraniiii, wanaonirudisha nyuma wengi wao majiraniii
Majiranii, wanaonirudisha nyuma wengi wao majirani

Yapu yapu yapu yapu pruduce welter
Hii ni sauti ya mwanao
Yule yule Dogo Mfaume
Angalia haooo, watakufilisi
Wasikope kimbizaaaa haooo
Haruna Moshi Boban
Professional Players
Wapi Juma Nyoso
Yanini utumbo utupwee
Wakati wenyewe twalia ndizi
Ahaaa producer maneno yako haya
Mkurugenzi Peter

Bongo fleva zindukeni usingizini





Msanii wa Bongo Fleva, Bob Junior akiwa katika pozi. Huyu ni miongoni mwa wasanii wanaofanya vema mno katika ulingo huo wa muziki wa vijana na unaopendwa mno.

 
TANZANIA inaweza kupiga hatua kama wote wanaojihusisha katika sanaa watahamasika na kufanya sanaa ya ndani na si kupapukia zile za tamaduni za wenzao, wakiwamo Wamarekani.

Nawazungumzia wakina Jeniffer Lopez, Rihannah, Mac Anthon, Jay Z na wakali wengine wa huko wanaokula raha nyingi kutokana na kazi zao kukubalika duniani kote.

Wasanii wanaowika nchini kama watajaribu kuingiza muziki wa Tanzania zaidi, hasa ngoma zao za makabila, kama vile Wazigua, Wasambaa, Wamakonde huwenda mambo yakawa mazuri.

Vijana wale wanaoona hawawezi kuishi bila kufanya sanaa, hapana shaka huu ni wakati wao kuingia zaidi kulitumikia Taifa lao kwa kuhakikisha sauti zao zinaitangaza nchi yao .

Nasema hivyo huku nikifahamu kasumba ya Watanzania kwa siku za hivi karibuni kutoipenda zaidi nchi yao . Hata wasanii wetu nao wamo kwenye mkumbo huo.

Wananchi sasa hawana cha kufaidika kutoka kwa wasanii. Kila msanii anaona ni vema kuimba muziki wa Kimarekani, eti anajua hiyo ndio njia yake ya kuwika kimataifa.

Kwa bahati mbaya wanashindwa kutambua kuwa hiyo siyo njia ya kumfanya Ludacriss awatambuwe. Mimi ni miongoni mwa waandishi wachache waliofanikiwa kusikiliza wasanii nyota wa Kimarekani, akiwamo Ludacriss aliyekuja hivi karibuni.

Msanii huyo alisema kuwa Bongo fleva haijui ni kitu gani duniani. Hata hivyo msanii Shaggy naye alisema maneno kama hayo, kuashiria kuwa kazi bado ipo.

Vipi wanaweza kufika huko walipokuwa wenzao? Hayo ni maswali ambayo majibu yake ni mepesi kuliko maswali. Yani kuuliza vipi wasanii wa Tanzania wanaweza kufanikiwa ni ngumu kuliko majibu yake.

Utashangaa, ila utaelewa ninachomaanisha. Angalia, japo kuwa Shaggy hautambui muziki wa Tanzania , hasa huo wa Bongo Fleva, ila aliposhuhudia Wasukuma, Wanyamwezi wanacheza ngoma zao za asili katika Uwanja wa Bujora, aliinuka na kucheza.

Alishangaa kwa mengi kutokana na wakazi hao wa jiji la Mwanza walivyoweza kudumisha ngoma za asili. Ni kutokana na hilo , nathubutu kusema Shaggy, amerudi kwao na wazo la ngoma za kabila ya Wasukuma na Wanyamwezi na sio Bongo fleva.

Hata kama hutaki ila huo ndio ukweli. Huu ni wakati wa wasanii na wadau wote tukazinduka na kufanya kazi zetu kwa minajiri ya kukuza utamaduni wetu maana ndio wenye soko.

Shabiki wa muziki wa Hip Hop ya Kimarekani hawezi kupoteza muda wake kukaa na kumuangalia msanii wa Tanzania . Ana kitu gani kipya? Si bora ananunuwe CD ya wasanii wao wa huko wenye soko hata wale waliotangulia mbele ya haki?

Hakuna kufichana hapa. Ni bora tuambiane ili tujifunze. Sio siri, nilikuwapo jijini Mwanza, wakati Shaggy ametembelea huko hasa kwenye tamasha la Fiesta 2011.

Sijamuona akitikisa hata kichwa chake kuonyesha kwamba amekoshwa na msanii kama vile Prof Jay, Fid Q, Roma, Mataruma, Barnabas na wengineo waliokuwapo uwanjani pale.

Shoo hii ilifanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, Juni 25 na kuhudhuliwa na mashabiki wengi mno.

Wakati pale ameshindwa kuguswa na muziki huo wa ‘mikono juu’, muda mchache uliopita alipagawishwa na ngoma za makabila, hivyo kuonyesha kuwa ngoma za makabila zinaweza kuwaletea mafanikio vijana hao na kukuza utamaduni wan chi.

Kwa bahati mbaya Watanzania siku hizi kama tumerogwa. Ukisema ukweli huna thamani machoni mwao wala midomoni mwao. San asana watakusema kwa mabaya, hata kama lengo lako halikuwa baya.

Hakuna haja ya kulambana kisogo hapa. Kwa wale waliokuwapo kwenye tasniaa ya sanaa, waingize japo ngoma za makabila yao waone utamu wao.

Hata kama sio kwa albamu nzima, ila wanaweza kuimba hata nyimbo moja au mbili, ili wanapofanikiwa kupata shoo za kimataifa, waimbe mbele ya watu walioingia kwa ajili yake.

Waswahili wamesema kila muomba chumvi, huombea chungu chake. Kwa msanii wa Tanzania kuzidi kutumbia katika muziki wa nje ni kujimaliza mwenyewe.

Kila kitu kinawezekana kinachotakiwa hapo ni kutimiza wajibu wetu. Angalia Makhirikiri kutoka Botswana . Hawa wasanii wanaimba muziki na ngoma za kwao. Lakini wanawika na kuvuma mno.

Hivyo hata hawa wanaoimba Tanzania lazima wafuate nyayo za wengine, hasa wale wanaoimba ngoma za asili yao , namzungumzia, Costar Siboka, Wanne Star na wengineo.

Huo ndio ukweli, maana waswahili wamesema ‘kijua ndio hichi, msipounika mtaula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua’.

Jumamosi Njema

0712 053949
0753 806087

Thursday, September 29, 2011

Masikini Sinta weeeeeeeeee







 Juma Nature juu akiafutiwa na mwanadada Sinta wakati picha ya chini na Nature na mke wake. Na hapo ndipo pabaya, maana sidhani ndoa yake itadumu endapo uhusiano huo utaanza upya.

NYOTA wa filamu aliyewahi kutamba katika kundi la Kaole Sanaa Group, Christina Manongi, maarufu kama Sinta, yupo kwenye wakati mgumu akifikiria zaidi uhusiano wake mpya na Juma Kassim, Juma Nature, aliyewahi kuwa na uhusiano naye.

Hata hivyo mwanadada huyo hajaweka wazi uhusiano huo na Nature, zaidi ya kusema kuwa anafikiria kama anaweza kufanya naye kazi ya sanaa, hususan filamu na muziki.

Sinta, anayefanya kazi katika kampuni ya mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji, ameweka wazi hisia hizo na kuonyesha kuwa anaumwa na kichwa kwa kumuwaza mkali huyo wa ‘Wanaume Halisi’, licha ya kusema kuwa haamini kama anaweza kufanya naye kazi bila kinyongo chochote.

Licha ya kupendana wakati huo, wawili hao waliingia kwenye mkwaruzo mkubwa uliosabibisha Nature atunge vibao viwili vya kumsema mwanadada huyo.

Nyimbo hizo ni ‘Sitaki Demu’ na ‘Inaniuma Sana’, akiweka bayana hasira zake juu ya binti huyo aliyetingisha vikali katika vyombo vya habari kutokana na urembo wake.

Vibao hivyo vilifanya vema mno katika vituo vya redio na kuzidi kumuweka juu mkali huyo mwenye bahati kubwa.

Mara baada ya mwanadada huyo kuweka hisia zake kwa baadhi ya marafiki zake, wengi walionyesha wakimuuanga mkono kwa wazo lake na kumtaka asahau na kumpokea tena Nature, kama anataka kufanya naye kazia huaku akiambiwa kuwa itafanya vema.

Sinta alikuwa kimya kwa muda mrefu tangu alipogombana na Nature, kitu kinachowafanya baadhi ya watu washikwe na hamu ya kuwaona wawili hao wakiwa pamoja.

Wednesday, September 28, 2011

Unafiki wa wadau wa michezo ni hatari kwa Taifa

Kambi Mbwana, akishiriki katika matukio muhimu ya Vodacom Tanzania, ambao ndio wadau wakubwa wanaodhamini ligi ya Tanzania Bara. Kushoto ni Rukia Mtibwa na Matina Nkurlu, mtaalamu wa habari wa Vodacom Tanzania.
Picha juu nis: Mkuu wa kitengo cha Udhamini wa Vodacom Tanzania Tanzania, George Rwehumbiza.
                                    Pichani; Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim.
Picha ya Yanga na Simba wakiwa uwanjani.

Waandishi wa habari wakiwa kazini, hawa ni wadau wakubwa wanaostahili kuthaminiwa na kupigania maendeleo ya michezo Tanzania.
                                          Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage
Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Lloyd Nchunga
.
Mohamed Mharizo akiwa na Zaituni Kibwana. Hawa ni wadau wakubwa wa michezo wakiandikia magazeti ya New Habari (2006) Ltd, Mtanzania, Dimba, Rai, Bingwa na The African. Kwa  ushirikiano wa wote wanaweza kuendeleza michezo Tanzania. Mungu ibariki Tanzania.

UNAFIKI WA WADAU WA MICHEZO NI HATARI KWA TAIFA

HUWA najiuliza uwapi umuhimu wa mtu kujiita mdau wa michezo, hali ya kuwa ni timu moja tu, kama sio Simba basi Yanga, ndio anayoipenda na kuiheshimu kuliko nyingine yoyote nchini?
 
Yupo wazi akose ibada au kufanya kazi yake kwa sababu ya kukimbilia mechi hiyo ya Simba na Yanga, timu kongwe zisizostahili kuigwa hata kidogo kwa matatizo yao lukuki, wanayofanya miaka nenda rudi.
 
Hali ni mbaya zaidi ya ubaya. Ila ndio hao hao wanajiita wadau wa michezo, wakati hawana nia ya kuhudhulia mchezo wa aina nyingine yoyote ukiacha huo mpira wa miguu, tena wa Simba na Yanga.
 
Nakuwa mnyonge na kushukuru Mungu. Nasema hivyo maana nchi hii inaharibiwa na mfumo huo mbovu. Mashabiki hao ndio wenye nguvu na ushawishi mkubwa majumbani mwao na wote kuelemea kwa timu vigogo.
 
Na ndio wenye nguvu pia maofisini mwao. Kwa bahati mbaya au nzuri, neon la udau wa michezo linafikiriwa vingine. Angalia, licha ya Simba na Yanga kujimudu kimaisha na kiuchumi, bado Kampuni ya Bia Tanzania TBL kupitia bia yao ya Kilimanjaro, wanaidhamini klabu hizo.
 
Tena ni udhamini mkubwa mno. Kwa miaka mitano hii, Simba na Yanga zitafaidi fedha nyingi mno, bila kusahau mengineyo yenye tija na mguso kwa wakongwe hao, kama vile magari, vifaa vya michezo, fedha za kuendesha mikutano yao ya mwaka na nyinginezo.
 
Hayo ndio matatizo ya wadau wetu wa michezo. Kwani licha ya klabu hizo kujimudu, ila wanaongezewa ulaji. Wakati huo wenzao wanaambulia fedha ndogo zinazotolewa na wadhamini wakuu wa ligi hiyo.
 
Vodacom ambao ndio wadhamini wa ligi hiyo, wanatoa fedha za safari kwa timu zote 14 kuanzia Yanga ambao ndio mabingwa watetezi na timu ya Oljoro FC, waliopanda daraja msimu huu.
 
Ni mfumo mbaya mno. Kwani aliyekuwa nao anazidi kuongezewa na wengine wakibaki kama walivyo. Hayo ndio matatizo makubwa. Kwa mtindo huo huwezi kuifananisha Villa Squad na Yanga au Simba.
 
Kwa mfumo huu wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) Villa Squad haiwezi kuwika wala kubaki msimu ujao. Hapo kwenyewe haina kitu, vipi ipangiwe mechi mbili kwa siku tatu? Itoke Mwanza iende Bukoba itaweza?
 
Kikweli haiwezi. Lakini Simba wao wanaweza kufanya hilo vizuri, maana akiba kubwa wanayo. Kwanza wanazo kupitia wadhamini wakuu Vodacom na ukiongeza hao TBL kupitia bia yao ya Kilimanjaro.
 
Sina nia ya kulaumu, maana hayo ndio matatizo yetu. Na hao hao baadaye hukaa kwenye vikao vyao na kujiita wadau wa michezo. Nani kasema? Wadau wa aina hiyo ni sumu kwa maendeleo ya michezo.
 
Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuangalia mazoezi ya timu ya Taifa ya ngumi, yaliyokuwa yakifanyika katika Uwanja wa Ndani wa Taifa, jijini Dar es Salaam .
 
Nilishangaa kama sio kushikwa na uchungu. Wachezaji hao wanaojiandaa na mashindano ya ‘All African Game’, yanayotarajiwa kufanyika nchini Msumbiji, baadaye mwaka huu, hawana vifaa vya michezo.
 
Walikuwa wakilalamika hali hiyo ila hawakusikilizwa. Waliachwa kama watoto yatima. Inatia uchungu. Sasa hao wanaojiita wadau wa michezo wako wapi? Kwanini tusiwaite wadau wa mpira wa miguu?
 
Kwanini? Kuna ubaya gani sasa kuitwa wadau wa Simba na Yanga? Jamani, hakuna haja ya kufichana tunapotaka kuzungumzia mambo ya maana katika Taifa hili linalokwenda kwa kusua sua.
 
Tuweke maslahi ya Taifa kwanza kabla ya siasa zenu. Mnatumia vibaya vyombo vya habari na kuwapasha habari za uongo wananchi wenu. Ndio, kwani watu hao wanaojiita wadau huita wanahabari ili wapewe sapoti hiyo.
 
Nadhani hayo ni mambo yanayotakiwa yaangaliwe upya kwa maslahi ya michezo yetu hapa nchini. Najua timu kubwa ni suala lisiloweza kuzuilika, ikiwamo hiyo Simba na Yanga.
 
Hata Ulaya mambo hayo yapo. Zipo timu kubwa zinazogusa hisia za wengi, ikiwamo Manchester United, Chelsea , Liverpool , Arsenal na nyinginezo, ila pia wadau wao ni tofauti na wetu.
 
Kuna ubaya gani wadau hao kuzipa ‘sapoti’ na timu changa mfano wa Coastal Union , Moro United, Villa Squad, Oljoro na nyinginezo?
 
Si tunataka maendeleo sisi kwa mpira wa miguu? Si mnajiita wadau wa michezo nyinyi, kuna haja gani ya kuelemea Simba na Yanga? Haya ni maswali tunayotakiwa tujiulize sisi sote kwa maendeleo ya Taifa.
 
Kwa mtindo huo michezo haiwezi kupiga hatua kamwe. Tutaendelea kulalama tu kwakuwa hatuna mfumo mzuri. Tuambiane tu. Nadhani hata wadhamini Vodacom nao wanatakiwa walijuwe hili.
 
Licha ya kuiweka ligi hiyo kwenye presha kubwa ila bado mambo ni magumu. Kasoro nyingi, ikiwamo kuchelewa kwa fedha za kujikimu na kugharamia safari zao, ni sababu moja wapo ya kuharibu mfumo wao wa ligi yenye ushindani.
 
Hapo ndipo pabaya, kwani hilo sio tatizo kwa Simba na Yanga. Kwanza wana akiba kubwa ya wanachama na mashabiki wenye nazo huku pia wakiwa na udhamini mnono, wakiwamo TBL.
 
Nadhani tuliangalie hilo kwa mapana zaidi. Tujifunze kuweka mikakati yenye tija na mguso kwa maendeleo ya michezo hapa nchini. Najua inakuwa ngumu kusema ukweli ila hakuna haja ya kuogopana.
 
Huo ndio ukweli. Kinachotakiwa ni kuona ligi inakuwa na nguvu na ushindani, kitu kitakachowafanya wachezaji wapate nafasi kubwa zaidi, hasa kucheza soka la kulipwa duniani, ikiwamo Barani Ulaya.
 
Ni ligi yenye nguvu na ushindani ndiyo inayoweza kuiweka timu ya Taifa, Taifa Stars katika hali nzuri. Wachezaji wataonekana kimataifa. Huo ni mpango na mkakati wenye tija kwa wote.
 
Kwanini tupore haki za watu? Kwanini tujiite wadau wakati sisi ni mashabiki wa Simba na Yanga pekee? Kama wewe upo kwenye kitengo kikubwa, angalia jinsi gani unaweza kuinua mchezo wa masumbwi.
 
Kama wewe ni Meneja wa Kampuni, jua ipo michezo mingi na klabu nyingi zinazoweza kufanikiwa kwa kupitia wewe. Hatutaki sifa za kijinga kwa kusaini hundi kwa Simba na Yanga. Wao sio kila kitu katika nchi hii.
 
Zipo timu nyingi zinazohitaji msaada huo. Katika ligi iliyomalizika huku Yanga akiwa bingwa, zipo timu zilizoshuka daraja kwasababu ya ukata. Miongoni mwa timu hizo ni Majimaji ya mjini Songea na Ashanti United.
 
Walikuwa na wachezaji wazuri, ila tatizo ni ukata. Kama kula yao ni tabu hawawezi kuifunga Simba na Yanga wanaoweka kambi sehemu nzuri na kula vizuri.
 
Huu ni wakati wa kuangalia upya nyendo zetu kwa faida ya michezo. Tuwe na fikra pevu. Kila mtu awe makini. Bila hivyo tutaendelea kuwa wadau wa Simba na Yanga, licha ya kushindwa kufanya vizuri nyanja za kimataifa.
 
Kila siku ni Simba na Yanga tu hali ya kuwa zipo timu nyingi na zenye uwezo wa kufanya mapinduzi katika mpira wa miguu nchini. Ukiacha Azam FC, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar na nyingine za jeshi, klabu nyingine wana njaa kubwa.
 
Hazina uwezo kifedha wala wadhamini. Wao wenyewe ndio kila kitu. Viongozi wachache wasiokuwa na chochote wanapeana mchango kwa ajili ya timu yao .
 
Watu kama hao hawawezi kuzibania Simba na Yanga wenye kila kitu cha kujivunia. Huo ndio ukweli wa mambo wadau. Tuwe makini katika hilo kwa maendeleo ya michezo kwa ujumla.
 
Yapo makampuni mengi mno. Zipo taasisi kubwa na wafanyabiashara wenye nguvu, hivyo huu ni wakati wao wa kuingia zaidi michezoni. Nasema michezoni, maana ni mjumuiko wa michezo mingi, bila kuangalia mpira wa miguu pekee.
 
Hilo ndio jambo la busara kufanywa na hao wanaojiita wadau wa michezo kwa faida ya kizazi cha Tanzania , maana hakuna ubishi kuwa michezo ni ajira na inaweza kuingiza sifa kwa Taifa letu.
 
Naomba kutoa hoja.
 
0712 053949
0753 806087

Tatizo la maji Kilwa lapatiwa ufumbuzi






                                                       
Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu juu na Mustafa Sabodo, mfanyabiashara chini.


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MFANYABIASHARA maarufu Mustafa Sabodo na Mtanzania anayeishi nchini Marekani, Faraja Ukondwa, wameahidi kuchimba visima vya maji safi na salama 133, wilayani Kilwa, hivyo kupunguza tatizo la uhaba wa maji linaloyakumbuka maeneeo mengi mjini humo.

Hayo yamesemwa na mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), jijini Dar es Salaam jana, alipokuwa akizungumza na Mtanzania kuhusiana na kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wake.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mangungu mmoja wa wabunge machachari waliopita katika uchaguzi wa mwaka jana, alisema kwa kupitia msaada huo, wananchi wa Kilwa watanufaika na maji hayo, mara baada ya visima 30 kutoka kwa Sabodo na visima 100 msaada wa Ukondwa, kukamilika.

Alisema kero ya ukosefu wa maji ni kubwa katika maeneo hayo, hivyo kujitokeza kwa watu hao ni dalili njema za kuanza kufanyia kazi matatizo yanayowakabili wananchi wote na wakazi wa Kilwa.

“Nimekuwa katika presha kubwa kutafuta namna ninavyoweza kusaidia maendeleo katika jimbo langu na maeneo yote ya Kilwa, hivyo kujitokeza kwa wafanyabiashara hao kutapunguza matatizo hayo.

“Naamini wananchi wote watafaidika na maji hayo, hivyo ni jukumu la kila mwenye uwezo wake kushirikiana kwa karibu kutafuta namna tunavyoweza kuwakomboa watu wa Kilwa wenye utajiri mkubwa, japo kuwa wanaishi katika umaskini wa kutupwa,” alisema Mangungu.

Kwa mujibu wa Mangungu, yupo kwenye hatua za mwisho za kufanya ziara katika maeneo yote ya jimbo lake, akiwa na nia ya kuangalia jinsi ya kuweza kukabili changamoto kwenye eneo lake.

Mawazo mgando yanawasumbua wasanii wetu

Wasanii wa Tanzania wanatakiwa wafuate nyayo za wenzao kama hawa wa Dikakapa Traditional Dance wenye maskani yao nchini Botswana.

Juu kabisa msanii Rehema Chalamila, maarufu kwa jina la Ray C akiwa katika pozi.



 Juma Nature akiwa jukwaani. Msanii kama huyu anatakiwa awe makini ili aweze kufikia malengo ya kuwa nyota kama wengine wanavyowika duniani.




 
 

NIMEKUWA makini mno kufuatilia maisha ya wasanii wetu nchini na kujua mambo mengi yanayowahusu kila uchwao. Nafanya hivi maana ni mdau na mwenye kupenda zaidi kazi zao kila siku ya Mungu.
 
Katika hilo , mengi nimeyaona na kuyaacha kama yalivyo. Najua kabla ya kuyaacha yapite, huwa kwenye wakati mgumu kusumbua akili yangu nikitaka wafanye lile na kuaacha hili, hata hivyo mwisho wa siku wao ndio wahusika wakuu.
 
Hata hivyo katika hili siwezi kuliacha mara baada ya kuling’amua siku chache baada ya kumaliza uchunguzi wangu kwa wasanii mbalimbali hasa wa muziki wa Bongo Fleva, wanaotamba kwa muda zaidi ya bigijii.
 
Huo ndio ukweli, maana ni makosa na yanatakuwa yafanyiwe kazi kwa faida yao , ukizingatia kuwa supu inanywewa ikiwa ya moto. Sasa naanza. Wasanii wa Bongo fleva wana kasumba kuwa boashara wanayoweza kuifanya ni kuuza nguo.
 
Yani mara baada ya kupata kajina kadogo, hutafuta flemu ya duka na kufungua sehemu ya kuuza nguo. Ni biashara nzuri pia, ila inaishia hapo hapo au nini malengo yao ? Hivi biashara ni kuuza nguo peke yao ?
 
Mbona biashara ni nyingi mno zinazoweza kufanywa na vijana hao wanaona sanaa ndio maisha yao na hawawezi kuishi bila kuwa kwenye kundi hilo ? Hapa lazima tufanye jambo.
 
Ni wasanii wengi wanaofanya kazi hiyo japo kuwa maduka hayo hufa maara baada ya wao kupotea katika ramani ya sanaa, hivyo kuonyesha kuwa hawakuwa na malengo ya aina yoyote katika kufungua biashara hiyo, zaidi ya kupoteza muda.
 
Sitaki nionekane tofauti hapo, maana haya ni mawazo yangu nikitaka wasanii hao wafike mbali zaidi kuliko kupoteza muda wao. Kwa bahati mbaya aina yao ya sanaa ni ya siku tatu na kupotea kabisa.
 
Maisha yao huwa magumu mno wanapofilisika kisanaa hivyo kusumbua ndugu na marafiki zao, wakitaka wapewe msaada kimaisha. Ni wengi japo kuwa ni ngumu kuwataja maana hawakawii kupayuka wakisema wameharibiwa majina yao .
 
Hapa hakuna kufichana, japo kuwa tunaheshimiana, ukizingatia kuwa nia ni kuwafanya wasanii hao wafike mbali zaidi. Ipo haja ya wasanii hao kukaa chini na kuangalia biashara za kufanya, ikiwamo zile zenye tofauti na mavazi.
 
Nasema hivyo kwasababu biashara zipo nyingi kama wamejipanga na kuumiza vichwa vyao kwa ajili ya  maisha yao . Angalia msanii Judithi Wambura maarufu kama Lady Jay D. Huyu ni msanii aliyefika mbali zaidi kibiashara.
 
Ameweza kufungua vitega uchumi vyake zaidi ya vitatu na kumuingizia kipato kikubwa. Nzuri zaidi, bendi yake nayo inaendelea kufanya vema na kulinda jina la heshima yake. Labda ni kwasababu Jay D yupo na mtu makini, Gadna G Habash.
 
Habash aliweza kuacha kazi yake ya utangazaji Clouds FM kwa nia ya kuambatana na mke wake huyo mwenye uwezo mkubwa kisanaa. Sawa, ila nadhani hata mwanadada huyo pia anashaulika, kitu kinachompatia maendeleo.
 
Vipi hawa wengine? Je, hawana watu wa kuwaongoza kwa faida yao ? Jibu wapo wengi tu, ila mawazo yao nahisi ni ya kupelekena katika majumba ya starehe wakikata kilaji kwa raha zao, maana wanasema maisha yenyewe kimini.
 
Haya ni mawazo mgando. Nasema hivyo maana pesa inayotoka bila kuingia kamwe haiwezi kukaa muda mrefu. Nadhani huu ni wakati wa wasanii hao kukaa na kuangalia aina yao ya maisha kwa faida yao wenyewe.
 
Napenda kuona wasanii hao wakipiga hatua kubwa kimaisha, maana majina yao ni tofauti na maisha yao baada ya muda mchache. Kwanini kila msanii aone biashara ni ya kuuza nguo. Tena duka moja, lililozunguukwa na mangine?
 
Huo ni upungufu mkubwa. Jina la Ahmad Ally Madee ni kubwa ndio, ila linaweza kumuingizia fedha nyingi kwa kubuni biashara yenye tija. Wapo wengi, ila sidhani kama inaweza kuwa chachu yao ya kupiga hatua na kuishi maisha mazuri, kama watafungua vijibiashara vya kupoteza muda, kama wanavyofanya sasa.
 
Wakati ndio huu. Kaeni chini muangalie aina yenu ya maisha. Uvivu wa kufikiria usiwafanye mfe maskini, hali ya kuwa mngekuwa matajiri hata kama kuna kasumba ya kuibiwa kazi zenu, maana hao mnaowata wadosi hawawezi kuingia hadi kwenye biashara zenu.
 
Zindukeni kwa faida yenu wenyewe.
0712 053949
0753 806087



LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...