https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, March 31, 2015

Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal afungua mkutano wa Baraza la Vyuo Vikuu Afrika Mashariki

Picha ya juuu na chini ni Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua rasmi mkutano Mkuu wa Sita wa majadiliano wa Baraza la Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki (IUCEA) wenye lengo la kukuza maendeleo endelevu ya mifumo ya Elimu ya Juu na Maendeleo ya Kiuchumi, uliofanyika leo Machi 31, 2015 kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo baada ya kufunguliwa rasmi leo kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakati akiondoka kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere, baada ya kuufungua ramsi, leo Machi 31, 2015.Picha zote na Ofisi ya Makamu wa Rais (OMR)



Monday, March 30, 2015

UN yatangaza neema zaidi kwa Tanzania

DSC_0065
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Fedha,  Dk. Servacius Likwelile (katikati) akiwasili katika ukumbi wa mikutano kwenye hoteli ya Hyatt Regency akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Hoseana Lunogelo (kulia) pamoja na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez kwa ajili ya kuzindua rasmi ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2014 Tanzania, uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Nyuma yao ni Mkurugenzi wa Programu kutoka Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF), Dk. Tausi Kida.

Na Mwandishi wetu
UMOJA wa Mataifa umesema kwamba utaendelea kuisaidia serikali ya Tanzania katika kutanzua changamoto za maendeleo zinazoikumba nchi hii.
Kauli hiyo imetolewa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja huo (UNDP), Alvaro Rodgriguez  wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2014 mwishoni mwa wiki.

Ripoti hiyo imeandaliwa na Taasisi ya utafiti wa masuala ya kiuchumi na jamii- ya ESRF kwa ufadhili wa UNDP na inagusia changamoto za Maendeleo .
Katika hotuba yake amesema kwamba Umoja wa Mataifa unaona juhudi za serikali katika kuwakwamua wananchi katika umaskini na kutokana na  hali hiyo wataendelea kusaidia mipango mbalimbali ya maendeleo pamoja na utafiti wenye kulenga kutoa suluhu kwa changamoto za maendeleo ya wananchi.
DSC_0207
Mshehereshaji wa uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2014 Tanzania, Taji Liundi akiitambulisha meza kuu kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria uzinduzi huo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Ripoti hiyo ambayo inazungumza: "mabadiliko ya kiuchumi kwa maendeleo ya watu" imesheheni mipango mbalimbali ya maendeleo na shida zake na namna ya kukabiliana na shida hizo.

Katika utafiti huo imeelezwa kuwa pamoja na uchumi wa Tanzania kukua kwa  kasi umaskini bado ni kero kubwa  kutokana na kukosekana kwa uhusiano kati ya ukuaji wa kiuchumi na kufutwa kwa umaskini miongoni mwa wananchi wa kawaida. Kuanzia mwaka 2001 uchumi wa Tanzania umekuwa ukikua kwa zaidi ya asilimia 6.

Saturday, March 28, 2015

Simba na Azam fc zapigwa faini nzito



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KIKAO cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania  kilichoketi jumanne ya tarehe 24, Machi 2015 jijini Dar es salaam, kimepitia taarifa mbalimbali za michezo iliyochezwa na kutoa adhabu kwa wachezaji na vilabu vya Ligi Kuu ya Vodacom.


Katika mechi namba 107 iliyowakutanisha wenyeji Ndanda FC dhidi ya Coastal Unioni, klabu ya Ndanda imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Kuu ya Vodacom  kutokana na washabiki wake kumrushia chupa za maji mwamuzi msaidizi Anold Bugado.

Mechi namba 108 iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, (Stand United dhidi Simba SC), wenyeji timu ya Stand United imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(8) kutokana na timu yake kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika ishirini.

Mchezo namba 117 uliozikutanisha Simba SC dhidi ya Yanga SC kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, timu ya  Simba imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(9) kwa kukataa kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.

Nayo klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 42(11) baada ya timu yake kuonyeshwa kadi zaidi ya tano kwenye mchezo dhidi ya Simba SC, huku mshambualiji wake Dany Mrwanda  akipigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(12) kwa kutopeana mikono na wachezaji wa timu hiyo.

Thursday, March 26, 2015

Mdau wa maendeleo Kambi Mbwana aandika kitabu cha ‘Dira na Tumaini Jipya Handeni’

Picha juu na chini ni mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Bingwa, Dimba na Mtanzania kutoka Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, Sharifa Mmasi pichani akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni kilichoandikwa na Kambi Mbwana, ambaye ni Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu linalofanyika kila mwisho wa mwaka wilayani Handeni, mkoani Tanga. Picha na Mpigapicha wetu.
 
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWANDISHI wa Habari za Michezo ambaye pia ni Mratibu Mkuu wa Tamasha la Utamaduni la Handeni Kwetu, Kambi Mbwana, ameandika kitabu chake kinachojulikana kama ‘Dira na Tumaini Jipya Handeni’, kilichoanza kupatikana mapema wiki hii jijini Dar es Salaam na wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Kitabu hicho kimeelezea kero na changamoto mbalimbali za wananchi wa Handeni, kama vile shida ya maji, elimu na migogoro ya ardhi kwa ajili ya kushirikisha mawazo ya viongozi wa serikali, wadau na wananchi ili kukabiliana na tatizo hilo wilayani humo na mikoa ya jirani ambapo changamoto hizo zinashabihiana kwa kiasi kikubwa.
Sharifa Mmasi akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni, kilichoandikwa na Kambi Mbwana.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mbwana alisema kwamba kuandika kitabu hicho kuna lengo kubwa la kuelimisha jamii kwa ajili ya kutafuta fursa ya kimaendeleo katika wakati huu ambao wananchi wengi wamekuwa wakilia bila kupata msaada wowote.

“Naijua vizuri wilaya yangu ya Handeni na mkoa wa Tanga kwa ujumla, hivyo nimeamua nitumie kipaji change katika kuandika kitabu hiki ambacho kimeweza kuanika mambo mengi yenye tija kwa serikali na wananchi kwa ujumla, hivyo naomba waniunge mkono kwa kuhakikisha kwamba wanapata kitabu hiki popote kitakapokuwapo.

Kinapatikana kwa bei ndogo mno ya Sh 3500 kwa kuwa sikuwa na lengo la kutajirika kwa kupitia kitabu hiki bali kutoa mawazo yangu na kuelimisha jamii yangu inayonizunguuka, hivyo ni wakatai wa Watanzania wote, bila kusahau wakazi na wananchi wa Handeni kupata nafasi ya kusoma mawazo yangu kwa ajili ya kutafuta namna ya kufika mbali kiuchumi na kiutamaduni, ukizingatia kuwa kitabu kimegusia mambo kadhaa ambayo ni muhimu,” alisema Mbwana.

Kwa mujibu wa Mbwana, maeneo yanapopatikana kitabu hicho kwa jijini Dar es Salaam ni pamoja na ambapo ni Kinondoni Kwa Manyanya, kwenye kituo cha basi kwa muuza magazeti aliyekuwa pembeni ya ghorofa la Mwaulanga, Sinza Kijiweni kwenye studio inayoangaliana na lango la New Habari 2006 Ltd, upande wa wanaokwenda mjini, huku studio hiyo ikiwa karibu na duka la vifaa vya ujenzi. Maeneo mengine ni muuza magazeti wa Kimara Mwisho kwenye kituo cha basi cha wanaokwenda mjini, huku Buguruni kikipatikana katika studio ya upigaji wa picha karibu na Hoteli ya New Popex, Buguruni, jijini Dar es Salaam.

Aidha Mbwana alisema kwa wanaotaka kuwasiliana naye juu ya kitabu hicho cha Dira na Tumaini Jipya Handeni wanaweza kumpata kwa +255 712053949 au barua pepe; kambimbwana@yahoo.com.

Wednesday, March 25, 2015

Pan Africa na Changanyikeni FC kuwania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa ya Mkoa

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BAADA ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na timu za FFU na Zakhem kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao, kesho 20/03/2015 utapigwa mchezo mmoja wa kusaka nafasi ya kuungana na mabingwa hao kushiriki michuano ya ligi ya mikoa.

Mchezo huo wa mtoano utakaopigwa katika uwanja wa Mizinga Kigamboni, utazikutanisha timu za Pan Africa dhidi ya Changanyikeni ambazo zimemaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi yao.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam, DRFA, baada ya kumpata mshindi katika mchezo huo, majina ya timu hizo tatu yatapelekwa shirikisho la soka la Tanzania TFF.
Aidha kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Kenny Mwaisabula,imewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja mbalimbali kushuhudua michuano ya ligi mkoa wa Dar es salam tangu ilipoanza kutimua vumbi.

Pan Africa na Changanyikeni FC kuwania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa ya Mkoa

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BAADA ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na timu za FFU na Zakhem kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao, kesho 20/03/2015 utapigwa mchezo mmoja wa kusaka nafasi ya kuungana na mabingwa hao kushiriki michuano ya ligi ya mikoa.

Mchezo huo wa mtoano utakaopigwa katika uwanja wa Mizinga Kigamboni, utazikutanisha timu za Pan Africa dhidi ya Changanyikeni ambazo zimemaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi yao.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam, DRFA, baada ya kumpata mshindi katika mchezo huo, majina ya timu hizo tatu yatapelekwa shirikisho la soka la Tanzania TFF.
Aidha kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Kenny Mwaisabula,imewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja mbalimbali kushuhudua michuano ya ligi mkoa wa Dar es salam tangu ilipoanza kutimua vumbi.

Pan Africa na Changanyikeni FC kuwania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa ya Mkoa

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BAADA ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na timu za FFU na Zakhem kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao, kesho 20/03/2015 utapigwa mchezo mmoja wa kusaka nafasi ya kuungana na mabingwa hao kushiriki michuano ya ligi ya mikoa.

Mchezo huo wa mtoano utakaopigwa katika uwanja wa Mizinga Kigamboni, utazikutanisha timu za Pan Africa dhidi ya Changanyikeni ambazo zimemaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi yao.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam, DRFA, baada ya kumpata mshindi katika mchezo huo, majina ya timu hizo tatu yatapelekwa shirikisho la soka la Tanzania TFF.
Aidha kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Kenny Mwaisabula,imewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja mbalimbali kushuhudua michuano ya ligi mkoa wa Dar es salam tangu ilipoanza kutimua vumbi.

Pan Africa na Changanyikeni FC kuwania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa ya Mkoa

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BAADA ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na timu za FFU na Zakhem kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao, kesho 20/03/2015 utapigwa mchezo mmoja wa kusaka nafasi ya kuungana na mabingwa hao kushiriki michuano ya ligi ya mikoa.

Mchezo huo wa mtoano utakaopigwa katika uwanja wa Mizinga Kigamboni, utazikutanisha timu za Pan Africa dhidi ya Changanyikeni ambazo zimemaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi yao.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam, DRFA, baada ya kumpata mshindi katika mchezo huo, majina ya timu hizo tatu yatapelekwa shirikisho la soka la Tanzania TFF.
Aidha kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Kenny Mwaisabula,imewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja mbalimbali kushuhudua michuano ya ligi mkoa wa Dar es salam tangu ilipoanza kutimua vumbi.

Pan Africa na Changanyikeni FC kuwania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa ya Mkoa

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BAADA ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na timu za FFU na Zakhem kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao, kesho 20/03/2015 utapigwa mchezo mmoja wa kusaka nafasi ya kuungana na mabingwa hao kushiriki michuano ya ligi ya mikoa.

Mchezo huo wa mtoano utakaopigwa katika uwanja wa Mizinga Kigamboni,utazikutanisha timu za Pan Africa dhidi ya Changanyikeni ambazo zimemaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi yao.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam, DRFA, baada ya kumpata mshindi katika mchezo huo, majina ya timu hizo tatu yatapelekwa shirikisho la soka la Tanzania TFF.
Aidha kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Kenny Mwaisabula,imewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja mbalimbali kushuhudua michuano ya ligi mkoa wa Dar es salam tangu ilipoanza kutimua vumbi.

Tuesday, March 24, 2015

Mbunge Al-Shaimaa:Wahalifu wa albino wahukumiwe hadharani

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MBUNGE wa Viti Maalum (CCM), Al Shaimaa Kweigyir, ameitaka serikali kuhakikisha kwamba hukumu za watu wanaokutwa na hatia dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), zinafanyika kwa uwazi, sambamba na kutocheleweshwa ili kulinda roho za Watanzania wanaoendelea kuangamia.
Picha mbalimbali zikimuonyesha mbunge wa Viti Maalumu, Al-Shaymaa Kweigyir, akiomba mwongozo wa Spika bungeni jana mjini Dodoma, kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya watuhumiwa wa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). Picha zote na Mpigapicha wetu, Dodoma..

Al-Shaimaa aliyasema hayo bungeni jana akitoa maelezo binafsi kwa kupitia Kanuni ya Kudumu ya Bunge ya (50) 1 inayomtaka mbunge kwa ruhusa ya Spika kutoa maelezo binafsi yanayomhusu au yanayoigusa jamii moja kwa moja.
 Akiendelea kutoa ya moyoni.

Picha za matukio mbalimbali kwenye sherehe ya wanawake Visi2wani Zanzibar

Zifuatazo ni picha za matukio mbalimbali kwenye red carpet wakati wa sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyowakutanisha wanawake kutoka kila kona ya visiwani Zanzibar ambayo iliandaliwa na Kikundi cha Wanawake cha Zanzibalicious na kufanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya hoteli ya Bwawani.
DSC_0148
DSC_0099
DSC_0095
Mbunifu wa mavazi kutoka bara Mama wa mitindo Asia Idarous (kushoto) akipozi na mbunifu wa mavazi kutoka visiwani Zanzibar Matilda Ishungisa wa Malty design.

Monday, March 23, 2015

SIWEZI KUVUMILIA:Mgambo ingecheza hivi mechi zote ingetwaa ubingwa

Na Kambi Mbwaana, Dar es Salaam
NAJUA kuifunga Simba au Yanga ni ujiko mkubwa. Kila mtu anafahamu hivyo, ndio maana timu ndogo zinapigwa kila mechi wanapokutana wenyewe, ila inapoingia uwanjani kucheza na Simba au Yanga, wanajikaza.

Wanajikaza kiasi kwamba mara kadhaa hushinda au wakishindwa wanalazimishwa sare na timu hizo kongwe na vigogo Tanzania Bara. Hii siwezi kuvumilia. 

Ukiacha matokeo ya mechi ya Yanga na Mgambo iliyochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Mkwakwani, jijni Tanga, Wagosi wa Kaya hao wanaotokea Kabuku, wilayani Handeni, walikuwa na pointi 24 na kushika nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi ya Tanzania Bara.

Katika mechi yao na Simba, Mgambo waliweza kucheza soka safi na la kuvutia kiasi ambacho kiliwapatia ushind wa mabao 2-0. Matokeo hayo yalikuwa machungu kwa mashabiki wa Simba. Hii ni kwa sababu yaliwaweka katika nafasi mbaya kuelekea kutwaa ubingwa wa Bara.

Kama hivi ndivyo, naumiza kichwa kwanini Mgambo isiwe inacheza soka safi la kuvutia hata inapokutana na timu ndogo? Kwanini timu zote zisiwe zinacheza soka lao safi ili ligi izidi kuwa na msisimko?

Sio kama nimeumia kuona Mgambo wameshinda mbele ya Simba, ila ni kuchukizwa na mfumo wa soka letu kuona timu zinajikaza pale wanapokutana na timu kubwa za Simba na Yanga.

Sunday, March 22, 2015

Pitia tamko la Zitto Kabwe alipojiunga na ACT, asema chama chao kipya kitafuata misingi ya mwalimu Nyerere

Maelezo ya Ndugu Zitto Kabwe aliyoyatoa katika Mkutano na Waandishi wa Habari kufuatia Kung’atuka Ubunge na Kujiunga na Chama cha ACT-Wazalendo Jumapili, 22 Machi 2015, Serena Hoteli, Dar es Salaam.

Ndugu Waandishi wa habari, wanachama na wapenzi wa ACT-Wazalendo na wote mliohudhuria mkutano huu, Kama mnavyojua siku ya Ijumaa tarehe 19 Machi 2015 ilikuwa siku yangu ya mwisho kuhudhuria bunge la kumi linaloendelea Mjini Dodoma.
Zitto Kabwe wa pili kutoka kushoto akifuatiwa na Afande Sele mwenye rasta wakionyesha kadi zao za ACT leo jijini Dar es Salaam.

Baada ya kung’atuka ubunge kufuatia kukoma uanachama wangu wa chama nilichotumia kuingia Bungeni, wengi mliniuliza ‘what is next?’.

Sasa ninapenda kuwataarifu, kama ambavyo baadhi yenu tayari mnajua, kwamba jana siku ya Jumamosi tarehe 20 Machi 2015 nilijiunga rasmi na Chama cha ACT - Wazalendo na kukabidhiwa kadi na Mwenyekti wa Tawi la Tegeta. Hii ilikuwa ni moja kati ya siku muhimu kabisa katika maisha yangu ya kisiasa. Na kwa leo kwa kweli nisingependa nizungumzie mgogoro uliokuwepo kati yangu na viongozi wangu wa chama cha zamani wala kile kilichotokea Bungeni. Hayo yote mnayajua, yameandikwa sana na yameshapita. Sasa ni wakati wa kusonga mbele. Rais Kwame Nkrumah alipata kusema "forward ever, backward never". Na kama nilivyosema Bungeni, yaliyopita si ndwele, tugange yajayo. Kwa hiyo leo nitazungumzia uanachama wangu katika chama changu kipya cha ACT - Wazalendo.

Tuna vyama 22 kwa sasa. Na kwa kweli wengi watakuwa wanajiuliza kwa nini nijiunge na chama kipya ambacho kimeanzishwa juzi tu na ambacho pengine wanachama wake bado wanajaa katika kiganja cha mkono?

Nimejiunga na ACT kwa sababu ninaona kwamba huku ndiko kunakoendana na kile ambacho mimi nimekipigania kwa miaka yote tangu nianze siasa, ambacho ni kuweka mbele maslahi ya Taifa dhidi ya kitu kingine chochote. Kwa kifupi nimepigania uzalendo kwa nchi yangu na huu ndiyo msingi mama wa Chama cha ACT - Wazalendo.

Afande Sele amfuata Zitto Kabwe ACT, aitosa Chadema

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWIMBAJI wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Selemani Msindi, Afande Sele, ametangaza kujiunga rasmi na Chama kipya cha siasa cha Alliance for Change and Transparency, ikiwa ni saa chache baada ya Zitto Kabwe kujiunga nacho.
Mwimbaji wa Hip Hop Afande Sele akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati anatangaza kujiunga na ACT leo.

Habari kutoka eneo la tukio zinasema kwamba Sele aliyekuwa mwanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameamua kujiunga na chama hicho ili aweze kutimiza azma yake ya kujihusisha na siasa kwa undani.

Sele alikuwa na lengo la kugombea Ubunge katika jimbo la Morogoro Mjini mwaka huu, hivyo huenda ameamua kuhamia ACT  ili apate nguvu na ushawishi mkubwa wa kuweza kuwatumikia wana Morogoro kwenye uchaguzi huo.

Kuhamia kwa Sele ACT kunaongeza kasi ya joto la watu wanaoanza kukiangalia kwa jicho la matumaini makubwa chama hicho kilichoasisiwa kwa mlengo wenye dhamira ya kupambania sera zenye kuleta mustawi mpana wa maendeleo ya Tanzania.

Zitto ajiunga rasmi na ACT, leo kuwatangazia wananchi kupitia waandishi wa habari leo saa tano

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
ALIYEKUWA Mbunge Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Zitto Kabwe, amejiunga rasmi kwenye Chama chake kipya kinachojulikana kama Alliance for Change and Transparency ( ACT), imefahamika.
Zitto Kabwe kushoto baada ya kusaini kujiunga rasmi kwenye chama cha ACT usiku wa kuamkia leo, jjini Dar es Salaam. Picha kwa hisani yaa mitandao.

Habari zlizoanza kuenea katika mitandao ya kijamii na kwa mtu wa karibu zilisema tamko la kuhamia kwenye chama hicho kipya atazitoa leo saa tano asubuhi, jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo kabla ya kukutana na waandishi wa habari, tayari picha zake zimeanza kuzagaa katika mitandao ya kijamii zikimuonyesha wakati anasaini juu ya kujiunga kwenye chama hicho kinachotarajia kuingia kwenye Uchaguzi wa ndani hivi karibuni.

Duru za siasa zinasema endapo Zitto asingeweza kujiunga na chama hicho kipya jana, basi asingekuwa na sifa ya kugombea uongozi wowote ndani ya ACT, inayotaka mwanachama wake aliyejiunga siku saba kabla ya uchaguzi wao.

Hata hivyo juu ya mwelekeo wake kisiasa na namna gani anaweza kuendelea kuwatumikia Watanzania kwa mambo mbalimbali, Zitto ataongea mengi katikaa mkutano huo na waandishi wa habari, ikiwa ni siku moja baada ya kuachia ngazi rasmi kwa kuaga bungeni.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...