https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, April 06, 2018

Wazanzibar waaswa kuwa wazalendo na nchi yao

Na Mwandishiwetu, Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dkt. Ali Mohamed Shein  amewaasa vijana wa Zanzibar kuwa Wazalendo na nchi yao  kwa kuisoma na kuijua historia ya Zanzibar ikiwa ni pamoja na kuenzi mchango wa Mwasisi wa Taifa hilo Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Dkt. Shein  ameyasema hayo wakati akitoa hotuba ya ufunguzi katika  kongamano la kwanza la kumbukumbu ya Rais wa kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa kwanza wa Baraza la mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume,  lililofanyika katika Chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere   katika kampasi ya Zanzibar, iliyopo Bububu  mjini Magharibi siku ya Alhamis tarehe 5 April, 2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dkt. Ali Mohamed Shein akitoa hotuba ya ufunguzi wakati wa kongamono la kumbukumbu ya hayati sheikh abeid amani karume lililoandaliwa na chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere kampasi ya zanzibar.


“Hayati Sheikh Abeid Amani Karume,   alikuwa ni mtu mvumilivu na mstahimilivu, aliyeipenda Zanzibar na wananchi wake, hivyo ni vyema mchango wake katika kuleta maendeleo ya Zanzibar ukakumbukwa na kuenziwa.

Rais Karume ametumia fursa hiyo pia kukipongeza Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa kuona umuhimu wa kuandaa Kongamano hilo ambalo ni la kwanza kufanyika visiwani Zanzibar.

Mikoa na wilaya zaagizwa kutenga maeneo ya hifadhi

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri wakipanda mti wa kumbukumbu wakati wa kilele cha kuadhimisha siku ya upandaji miti kitaifa iliyofanyika jana katika kijiji cha Mhunze wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.

Na Hamza Temba, WMU, Kishapu, Shinyanga

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amewaagiza Wakuu wa Mikoa nchini kuhakikisha Halmashauri zote nchini zinatenga maeneo katika kila kijiji kwa ajili ya uhifadhi wa misitu ikiwa ni pamoja na vijiji hivyo kuunda kanuni na taratibu zao wenyewe za kusimamia maeneo hayo.

Ametoa agizo hilo jana katika kijiji cha Mhunze wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wakati wa kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Upandaji Miti Kitaifa yaliyofanyika mkoani humo kuanzia Aprili 03 mwaka huu.

Muriya: Makazi yetu Oman ni fursa za kiuchumi kwa watu wote

Makazi ya Jebel Sifah nchini Oman ni fursa za kiuchumi kwa watu wote

Balozi Mdogo wa Oman Visiwani Zanzibar, Ahmad Mohamed Al Muzaini wa nne kutoka kulia akiwa amesimama baada ya kumaliza kuzungumza kwenye maonyesho ya makazi ya Oman Visiwani Zanzibar yakiandaliwa na Kampuni ya Muriya yenye maskani yake nchini Oman. Maonyesho hayo yamefanyika katika Hoteli ya The Park Hyatt, Zanzibar. Wengine ni wadau wa ardhi na makazi waliohudhuria kwenye maonyesho hayo. Picha na Mpiga picha wetu.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
HUKU maonyesho ya makazi ya Jebel Sifah yanayoonyeshwa na Kampuni ya Muriya yenye maskani yake nchini Oman yakiendelea visiwani Zanzibar katika Hotel ya The Park Hyatt, baada ya kumalizika jijini Dar es Salaam, wafanyabiashara wa visiwani hapa wametakiwa kupanua wigo wao wa kibiashara kwa kununua makazi yao nchini Oman ili wajiwekee vitega uchumi kwa ajili ya maendeleo yao.

Ushauri huo umetolewa leo na Meneja Mauzo wa Muriya, Ghizlane El Gouchi, wakati wa kuelimisha wakazi na wananchi wa Zanzibar juu ya utendaji kazi wao katika sekta ya ardhi na makazi waliyojikita nchini Oman, huku wakijivunia maendeleo makubwa kwenye sekta hiyo muhimu dunian kote.

Tuesday, April 03, 2018

Watanzania waaswa kuchangamkia makazi nchini Oman

Meneja Mauzo Mwandamizi wa  Kampuni ya Ujenzi wa Makazi ya Muriya, Ghizlane El Gouchi (wa pili kushoto) akiwaonyesha wageni waliohudhuria hafla ya kuitambulisha kampuni hiyo kuelekea maonyesho ya biashara yaliyoanza leo jijini Dar es Salaam hadi Aprili 5 na Zanzibar Aprili 6. Kushoto ni Mshauri wa Mradi Mona Abel Malak, mshauri mwandamizi, Faisal Alzakwani,Mshauri Hamad Al Balushi na mshauri mwingine Omar Saleh. 

NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
Watanzania wameaswa kuchangamkia nyumba zinazouzwa na Kampuni ya Muriya yenye maskani yake Muscat nchini Oman, ili kujiweka katika kundi sahihi la kibiashara sanjari na kujipatia maendeleo makubwa kutoka kwa nchi ya Tanzania na Oman.

Hayo yamesemwa leo na Meneja Masoko na Kampuni ya Muriya Ghizlane El Gouchi, wakati anazungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya nyumba zinazouzwa na kampuni yao huku maonyesho hayo yakifanyika jana katika Hotel ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam na kuhudhuliwa na watu mbalimbali wenye ndoto za uwekezaji wa majengo.

Saturday, January 13, 2018

Watanzania wanaoishi Saudi Arabia washerehekea Sikukuu ya Mapinduzi Riyadh Palace Hotel na Balozi Mgaza

Baadhi ya Watanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mgaza katikati mwenye suti.

Na mwandishi maalum, Riyadh - Saudi Arabia
Wanadiaspora na Watanzania waishio Riyadh nchini Saudi Arabia walisherehekea na kuandhimisha miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar  siku ya ijumaa tarehe 12 Januari, 2018 katika ukumbi wa Riyadh Palace Hotel. 

Sherehe hizo zilindaliwa na jumuiya ya Watanzania 'Tanzania Walfare Society' ambapo waalikwa mbalimbali kutoka miji ya Riyadh, Qasim na maeneo ya karibu walihudhuria. Mgeni rasmi katika sherehe hiyo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. 

Hemedi Mgaza. Miongoni mwa walihudhuria sherehe hizo pia walikuwa wanafunzi wa vyuo vikuu, wafanyakazi wapya wa kampuni ya ufugaji ng'ombe wa Maziwa ya Al Marai na wengine kutoka kampuni ya ufugaji kuku ya Al Watania.  Kwa picha na habari zaidi angalia kupitia you tube 'Prince eddycool'
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania ya Riyadh, Bw. Fuad Mabruk akitoa hotuba mbele ya Watanzania na wanadiaspora wa mji wa Riyadh huku nyuma yake walioketi kwenye meza kuu kuanzia kulia ni Makamu wa Mwenyekiti wa Jumuiya Dkt. Mahmoud Tuli, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Mgaza, Afisa Mkuu wa Utawala wa Ubalozi Bw. Ahmada Sufiani, Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Bw. Saeed Al Jabry na wa kwanza kushoto ni Mweka Hazina wa Jumuiya Bw. Mohamed Saeed.
 Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, H.E Hemed Mgaza, akizungumza na Watanzania.
Baadhi ya Watanzania na wanadiaspora wakisikiliza hotuba zilizokuwa zikitolewa na baadaye walipata fursa ya kuuliza maswali na kutoa maoni.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...