https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, August 11, 2013

Kupitishwa kwa madawa ya kulevya Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere kwa kuza balaa na ajira za watu



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
OFISA wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), aliyekuwa zamu siku dawa za kulevya zilipopitishwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam na kukamatwa Afrika Kusini amesimamishwa kazi.

Dawa hizo zilipitishwa na wanawake wawili zikiwa na thamani ya zaidi ya Sh bilioni 6.8 wakitoka nchini ambapo ofisa aliyekuwa sehemu ya kukagua mizigo alihusishwa na kusimamishwa kazi huku uchunguzi ukiendelea.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema alipozungumza na waandishi wa habari na kusema baada ya uchunguzi hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wahusika.

Hata hivyo hakutaja ofisa huyo aliyesimamishwa kazi. Wanawake waliokamatwa na dawa hizo ni Agnes Gerald (25) na Melisa Edward (24) ambao walifunguliwa mashitaka Afrika Kusini.

Walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalikaguliwa na kukutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kwa jina la ‘Tik’ zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya randi milioni 42 sawa na Sh bilioni 6.8.

Kusimamishwa kazi kwa ofisa huyo ni mikakati ya Polisi kuhakikisha kurejeshwa kwa sifa ya kuaminika kwani sasa inatajwa kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kuwa ni moja ya njia kuu za kusafirisha dawa za kulevya.

Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Elieza Feleshi, alisema katika kuhakikisha haki inatendeka, hawezi kuwakingia kifua watendaji wabovu na kuahidi kuwashughulikia kutokana na mashitaka waliyonayo.

Alisema baada ya kuwapo tuhuma kwamba amekuwa akiwakingia kifua watendaji wabovu jambo ambalo alisema si kweli.

Aidha, alisisitiza kuwa si kweli kwamba kuna taarifa za watu kubambikiwa kesi kwani haki inatendeka kwa watuhumiwa wote, jambo lililosaidia kupunguza mlundikano wa wafungwa kutoka 45,000 hadi 33,000 wiki hii. Kwa hisani ya mitandao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...