https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, April 30, 2013

Pesa kuduchu zapatikana mechi ya Simba na Polisi Morogoro



MECHI namba 163 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa juzi (Aprili 28 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kuibuka ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi Morogoro imeingiza sh. 18,014,000.
                                          Kipa wa Simba, Juma Kaseja
Watazamaji 3,145 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 3,564,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 2,747,898.31.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 2,841 na kuingiza sh. 14,205,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 36 na kuingiza sh. 720,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 1,812,331.75, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 1,087,399.05, Kamati ya Ligi sh. 1,087,399.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 543,699.53 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 422,877.41.

Ligi ya Tanzania Bara kuendelea kwa timu tano kumenyana uwanjani



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea katika raundi yake ya 25 kesho (Mei Mosi) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi.
                                          Msemaji wa TFF, Boniface Wambura
Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini.

Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa.

Bondia Japhet Kaseba kuzipiga na Mkenya Joseph Magudha Mwezi wa sita

Mwili chuma
                        Taratibu zikiendelea, akiwapo Pendo Njau anayeandika



             Mabondia wakionyeshana ubabe

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BONDIA mwenye uwezo wa kutisha nchini, Japheti Kaseba, anatarajia kuzipiga na bondia kutoka nchini Kenya, Joseph Magudha mwishoni mwa mwezi wa sita huku kila mmoja ikiwa ni njia yake ya kuonyesha umwamba. 
Mdau wa ngumi nchini, Ibrahim Kamwe, alisema kuwa mchezo huo utatoa picha kamili ya ubabe wa mabondia hao.

Monday, April 29, 2013

Picha mbalimbali kuachiwa kwa dhamana kwa Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini na kukusanya nyomi la nguvu sambamba na mabango ya kuinanga Serikali


MH. LEMA AKIWA KIZIMBANI
 
***********
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema, leo amepandishwa kizimbani jijini Arusha na kusomewa shitaka lililokuwa likimkabili na kuachiwa kwa dhamana iliyokuwa na masharti rahisi.

Godless Lema, alikuwa akishikiliwa na polisi mkoani humo kwa tuhuma za uchochezi wa vurugu zilizosababishwa na wanafunzi kwenye chuo cha Uhasibu mwanzoni mwa wiki iliyopita mwenzao kuuwawa huko maeneo ya njiro jijini humo.

Mbunge huyo alikamatwa siku ya Ijumaa na kuwekwa rumande kwa amri ya Mkuu wa Mkoa wa wa Arusha, Magesa Mulongo.

Baada ya kuachiwa mahakamani hapo mbunge huyo ameongozana na wafuasi wake kwa msafara wa maandamano na mapikipiki kuelekea katika Ofisi za Chama hicho.

Picture

Picture
Picture
Picture

Mkuu wa Wilaya Ilala ahamasisha ujasiriamali kwa wananchi ili wajikomboe

no 1
Meneja Miradi wa Shirika la Plan International Wilaya ya Ilala Daniel Kalimbya akiongea katika hafla fupi ya kufunga mkutano wa tathmini ya miradi inayoendeshwa na Shirika hilo kuhusu Ujasiriliamali katika wilaya ya Ilala.Mkutano huo ulishirikisha wadau kutoka Asasi zisizo za kiserikali, Vikundi vya vijana na Maafisa wa Serikali.(Picha na Frank Geofray)
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akiongea katika hafla fupi ya kufunga mkutano wa tathmini ya miradi inayoendeshwa na Shirika hilo kuhusu Ujasiriliamali katika wilaya ya Ilala.Mkutano huo ulishirikisha wadau kutoka Asasi zisizo za kiserikali, Vikundi vya vijana na Maafisa wa Serikali.(Picha na Frank Geofray)
no 3
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa tathmini ya miradi inayoendeshwa na Shirika la Plan International kuhusu Ujasiriliamali wakimsikiliza mgeni rasmi katika hafla ya kufunga mafunzo hayo wilayani ya Ilala.Mkutano huo ulishirikisha wadau kutoka Asasi zisizo za kiserikali, Vikundi vya vijana na Maafisa wa Serikali.(Picha na Frank Geofray)no 4
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa tathmini ya miradi inayoendeshwa na Shirika la Plan International kuhusu Ujasiriliamali wakimsikiliza mgeni rasmi katika hafla ya kufunga mafunzo hayo wilayani ya Ilala.Mkutano huo ulishirikisha wadau kutoka Asasi zisizo za kiserikali, Vikundi vya vijana na Maafisa wa Serikali.(Picha na Frank Geofray)
                                                           ........................................
Na Frank Geofray.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw.Raymond Mushi amevitaka vikundi vya Vijana, Asasi zisizo za Kiserikali na watumishi wa umma waliopata mafunzo ya ujasiriliamali yanayotolewa na Shirika la kimataifa la Plan kuyatumia vizuri katika kuwaletea maendeleo na kuondokana na umaskini.
Bw.Mushi aliyasema hayo wakati alipokuwa akifunga mkutano wa kufanya tathmini ya miradi ya ujasiriliamali iliyokuwa ikiendeshwa na shirika hilo kwa makundi mbalimbali katika kata zote za wilaya ya Ilala Jijini Dar Es Salaam.
Alisema ujasiriliamali ni njia mojawapo ya kuondokana na umaskini na kujikwamua kiuchumi hivyo kutolewa kwa mafunzo hayo kutawasaidia wananchi kutambua fursa zilizopo na kuzitumia vyema.
Aidha aliwaasa washiriki wa mkutano kuwekeza katika elimu kwa watoto ili kujenga taifa lenye uelewa na maarifa hapo baadae kwa kuwa watoto wanapaswa kupewa haki yao ya kupata elimu bora.
“Pamoja na kwamba mtawekeza katika kufanya biashara lakini lazima mhakikishe na suala la elimu kwa watoto wenu mnalitilia mkazo ili kuweza kuwajengea maisha bora hapo badaye”Alisema Bw.Mushi.

Sunday, April 28, 2013

Pitia maoni ya Mwanachama wa CCM, Hussein Bashe juu ya suala la Jimbo la Nzega na kukamatwa kwa Godbless Lema jijini Arusha



                          Mwana CCM Hussein Bashe
Ndg zangu, Awali ya yote niwatakie Juma pili njema na Kwa Ndg zetu wanoenda kanisani siku ya Leo waendelee kuombea Taifa letu na Viongozi wetu kufanya maamuzi ya busara juu ya Hatima ya Maisha ya Watanzania na Taifa kwa Ujumla.

Nimeanza na maneno hiyo hapa juu kufatia matukio miwili,Moja ni Tukio la Arusha na Pili ni Tukio la Maamuzi ya Baraza la Madiwani la wilaya ya Nzega.

Nzega
Halmashauri ya wilaya nzega imepitisha Bajeti na mipango ya Mendeleo ya mwaka wa fedha 2013/4 kilichonisikitisha ni Madiwani kujitengea milioni 82 kwa ajili ya ziara Kwenda mkoa ya Arusha, Dodoma Kama ziara ya kujifunza,Wakati wilaya inakabiliwa na Changamoto za uharibifu wa miundo mbinu kufatia muda Nyingi, makazi ya wananchi wengine yameharibika, shule za msingi na secondaries hazina Madawati, waalimu hawana nyumba, vituo vya Afya having dawa za kutosha, tunakabiliwa na tatizo la Maji Mijini na vijijini.

Baada ya kutwaa Ubingwa wa Bara, Yanga sasa waidhalilisha Simba


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema hauwezi kuifikiria mechi yao dhidi ya Simba, badala yake nguvu zao zote wamezielekeza kwa timu ya Coastal Union ya Tanga, mechi itakayopigwa Mei Mosi, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto

Maneno ya Yanga yanatafsiriwa kama tusi kwa Simba iliyoonekana dhaifu katika mzunguuko wa pili na kushindwa kutetea ubingwa wao ulionyakuliwa na Jangwani wakiwa na mechi mbili mkononi.

Mechi ya Yanga imepangwa kufanyika Mei Mosi, wakati ile ya Simba watacheza Mei 18 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, ambapo pia itakuwa ni hitimisho ya patashika ya Ligi ya Tanzania.

Mambo matatu aliyohojiwa Godbless Lema Polisi jijini Arusha

KWA HISANI YA GAZETI LA MWANANCHI
 
Kushikiliwa kwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema (pichani) kumeendelea kuibua sokomoko baina ya polisi kwa upande mmoja na wafuasi wa Chadema na familia yake kwa upande mwingine.
Godbless Lema
Arusha. Lema aliyekamatwa usiku wa manane kuamkia Ijumaa wiki hii, alihojiwa kwa saa tatu mfululizo katika Kituo Kikuu cha Polisi, Arusha lakini alinyimwa dhamana kwa maelezo kwamba kuachiwa kwake kungehatarisha amani.
 
Akizungumza na gazeti hili kabla ya kujisalimisha kwa askari hao usiku huo wa kuamkia juzi, Lema alithibitisha kuwapo kwa polisi nje ya nyumba yake:
 
“Wapo nje ya nyumba yangu, wanatishia kupiga mabomu kama nisipotoka nje, lakini wanajadiliana na walinzi wangu na mimi nimewataka wanipe hati ya kunikamata,”alisema.

Afariki kwa kukanyagwa na gari mkoani Morogoro baada ya kudondoshwa na mwenzake

 
Mwili wa marehemu, Romanus Masige mkazi wa Kihonda Manispaa ya Morogoro ukiwa umelala chini katika barabara ya Old Dar es Salaam eneo la maktaba ya mkoa wa Morogoro baada ya kudaiwa kusukumwa na wenzake waliokuwa nao wamepakiwa nyuma ya lori wakati wakisafiri kutoka Kihonda kuelekea kituo kikuu cha polisi mjini hapa.(Picha zote kwa hisani ya Jackson Audiface

Shuhuda akieleza tukio zima lililotokea

Handeni Kwetu Blog yadhamini Redds Miss Kibaha 2013


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WADHAMINI kibao wameendelea kumiminika katika Shindano la kumtafuta malkia wa Redds Miss Kibaha 2013 linalotarajiwa kufanyika baadaye mwezi ujao, huku mke wa Mbunge wa Kibaha, mama Celina Koka, Handeni Kwetu Blog na Multichoice nao wakijitokeza kuliwezesha shindano hilo.
Mmiliki wa Handeni Kwetu Blog, Kambi Mbwana

Shindano hilo linaloendelea na maandalizi yake ikiwapo kufanya mazoezi kabambe kwa warembo, pia linadhaminiwa na Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Blog, Handeni Kwetu Blog, The African Stars Entertainment (ASET) na Redds Premium Cold.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mratibu wa shindano hilo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Linda Media Solution (LIMSO), Khadija Kalili, alisema kujitokeza kwa wadhamini hao ni sehemu ya kuliweka shindano lao kwenye kiwango cha juu.

Bondia wa kike nchini Tanzania Pendo asikitika kukosa wapinzani


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa Kick Boxing nchini, Pendo Njau, amesema ukimya wake unatokana na kukosa wapinzani katika mchezo huo kutokana na kukimbiwa na mabondia wake, jambo linaloathiri ngumi za mateke.
Bondia mahiri wa kike nchini Tanzania, Pendo Njau
Akizungumza hivi karibuni kwenye Ukumbi wa mazoezi wa bondia Japhet Kaseba, Pendo alisema kinachoendelea ni mateso kwa mabondia wa kike hasa wale wanaotegemea mchezo huo.

Redds Miss Kibaha wahamishia mazoezi yao Vijana Kinondoni


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WAREMBO wanaotarajiwa kushiriki katika shindano lijalo la Redds Miss Kibaha 2013, wameanza kufanya mazoezi katika Ukumbi wa Vijana Social Hall, Kinondoni.
Baadhi ya warembo wa Miss Kibaha, wakiwa mazoezini

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO), ambaye pia ndio Mratibu wa shindano hilo Khadija Kalili, alisema warembo hao wamekuwa wakijifunza mbinu mbalimbali kwa ajili ya kulifanya shindano lao liwe na msisimko wa aina yake.

Alisema kuwa mwitikio wa warembo ni mkubwa, ndio maana wameamua kuweka mkazo katika suala zima la mazoezi ili mabinti wawe kwenye kiwango cha juu.

“Warembo wanaofanya mazoezi chini ya wakufunzi wao Sweat Ray na Bob Rich ni Nzeran Kitano, Martina Kapaya, Asma Said, Maud Bernad, Flora Mlowola na Nancy James.
 
Wengine ni Esther Albert, Beatrice Bahaya, Jenipher Njabiri na  Rachel John ambao wote kwa pamoja wanafundishwa shoo na mcheza shoo wa Victoria Sound, Bokilo,” alisema Khadija.
 
Kalili anawataja baadhi ya wadhamini waliojitokeza kudhamini shindano hilo ni Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Blog, Handeni Kwetu Blog, The African Stars Entertainment (ASET) na Redds Premium Cold.

Extra Bongo kukamua Garden Breeze leo

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BENDI ya Extra Bongo, leo inafanya shoo ya aina yake katika viwanja vya Garden Breeze Magomeni, jijini Dar es Salaam, huku ikiwa na mipango kabambe ya kuteka nyoyo za wapenzi wao.
         Wacheza shoo wa Extra Bongo
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki alisema kuwa shoo yao itakuwa ya aina yake kutokana na mipango kabambe wanayoendelea kuifanya.

Alisema kwa sasa kiu yao ni kuhakikisha kuwa mashabiki wao wanapata kazi ya aina yake, hivyo wadau na mashabiki wa muziki waende kwa wingi kuangalia vitu vyao.

“Extra Bongo imesheheni wakali kila upande, wakiwamo waimbaji, marepa pamoja na wacheza shoo ambao kwa hakika dhamira yao kubwa ni kuona wadau wao wanaburudika.

“Tunaomba waje kwa wingi katika shoo yetu ya Garden Breeze kwa ajili ya kuangalia namna gani tupo imara katika tasnia ya muziki wa kizazi cha dansi hapa nchini,” alisema Choki.

Safu ya ucheza shoo ya Extra Bongo inaongozwa na Super Nyamwela, wakati waimbaji wanaofanya vyema katika bendi hiyo ni Banza Stone, Khadija Kimobiteli, Athanas, Rogati Hega Katapila, Choki na wengineo wanaotesa katika ramani ya muziki wa dansi.

Saturday, April 27, 2013

Kenya waanza vyema mchezo wa vishale jijini Arusha

 Mgeni Rasmi, Afisa Tawala wa Mkoa wa Arusha, Jackson Saitabahu(wa pili kushoto), Rais wa Shirikisho la Darts Afrika Mashariki, Gesasu Waigama ( aliye katikati), katibu mkuu wa Darts Afrika Mashariki, Gerald Kimetu(wa pili kulia) na Katibu mkuu wa Darts Taifa, Kaale Mgonja katika uzinduzi wa Mashindano ya Darts Safari Lager Afrika Mashariki na kati yaliyoanza jana katika ukumbi wa Appex, Kijenge, jijini Arusha.

 Afisa Tawala wa Mkoa wa Arusha, Jackson Saitabahu akizindua mashindano ya mchezo wa Darts kusaka Bingwa wa Safari Lager Afrika Mashariki na kati , jana katika ukumbi wa Appex, kijenge, jijini Arusha.
Afisa Tawala wa Mkoa wa Arusha, Jackson Saitabahu, akizindua mashindano ya mchezo wa Darts kusaka Bingwa wa Safari Lager Afrika Mashariki na kati , jana katika ukumbi wa Appex, kijenge, jijini Arusha.

MAMBO FULANI MUHIMU

Ukijirahisi, kwenye mapenzi imekula kwako
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
INASHANGAZA kuona msichana anajirahisi katika suala zima la mapenzi, kwa madai eti anaonyesha uhalisia wake wa upendo kwa mwanaume, anayefanya naye kazi, anayeishi mtaani kwao au amekutana naye sehemu Fulani na kuona anafaa kuwa naye.
Pozi la aina yake la wapenda nao
Ni kweli kuwa yoyote anastahili kupenda au kupendwa mahala anapodhani panafaa, ila kuna miiko yake. Kumbuka, unaposhindwa kuzuia hisia zako, tena mahali pasipokuwa muafaka, ni wazi unahitaji kudhalilika kama sio kudhalilishwa na huyo umpendae.
Zipo kanuni zake. Hata shamba, linahitaji maandalizi, yakiwamo ya kulima au kupapaliwa baada ya kupandwa kwa mazao husika, hivyo inapotokea wewe umekurupuka katika suala la mapenzi, jua itakula kwako.

Kwanini nasema hivyo, wapo wasichana ambao wameshindwa kutambua namna ya kufikisha hisia au ujumbe wa mapenzi kwa wanaume wawatakao na kujikuta wakijiachia ovyo ovyo.
Ndio hapo mtu anapofanya vituko, iwe vya kuonyesha nyeti zake kwa mwanaume ambaye anajua kuwa 
akifanya hivyo yule mtu atajua kuwa anampenda.

RC Gama: Ushirikiano unainua maendeleo mkoani Kilimanjaro


Awataka wanasiasa wazuie juhudi za watendaji serikalini
Apania makubwa zaidi kuhakikisha mambo yanasonga


Na Mwandishi Wetu, Moshi
ILI suala ma maendeleo liweze kupatikana, hakika kunahitaji utayari wa kujitolea, uvumilivu na uwajibikaji kutoka kwa jamii yote pamoja na ushirikiano na viongozi wao.
                    Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Leonidas Gama
Juhudi hizo zikifanywa kwa makini bila bila kuwapo kwa muingiliano wa majukumu au msuguano wa kifikra ni rahisi kupatikana maendeleo.
Mlima Kilimanjaro ni miongoni mwa vivutio vya Utalii mkoani humo na Tanzania kwa ujumla.
Katika kulisema hilo, Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa mikoa inayopiga hatua kubwa kimaendeleo kutokana na ushirikiano miongoni mwa viongozi na wananchi wake.

Utekelezaji wa mipango ya ukuaji wa kiuchumi, inatekelezwa kwa kuzingatia fursa mbali mbali zinazopatikana, ikiwemo uwekezaji wa muda mfupi, muda mrefu na muda wa kati, unaoendelea kufanywa na wananchi pamoja na serikali ya mkoa.

Asha Baraka ampiga mkwara mzito Ally Choki


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKURUGENZI wa bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka, amempiga mkwara mzito Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki kwa kumueleza kuwa aache kuwafuatilia wanamuziki wake kwa lengo la kuiangusha bendi yake inayotesa hapa nchini.
 Ally Choki
Asha Baraka
Choki amekuwa kwenye mikakati ya kuimarisha safu ya Extra Bongo, huku akiwatolea macho wanamuziki kadhaa kwa ajili kuiweka sawa bendi yake hiyo ya Wazee wa Kizigo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Asha aliyerejea hivi karibuni akitokea nchini India, alisema kwamba ameambiwa mkakati wa choki kutaka kuibomoa bendi yake hiyo, jambo ambalo analichukulia kwa umakini mkubwa.

Friday, April 26, 2013

Ligi Daraja la Pili Dar es Salaam kumalizika kesho

Na Rahimu Kambi, Dar es Salaam
LIGI Daraja la Pili Mkoa wa Dar es Salaam hatua ya sita bora inamalizika kesho ambapo timu tatu zitakata tiketi ya kucheza hatua ya Kanda ili kupata nafasi ya kucheza Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.

Msemaji wa DRFA, Mohamed Mharizo
Ofisa Habari wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Mohamed Mharizo, amesema leo mchana kuwa ligi hiyo iliyoanza Aprili 15 ndio itapata wawakilishi watatu watakaouwakilisha mkoa huo katika hatua ya Kanda.

Alizitaja mechi zitakazochezwa leo kuwa ni Red Coast itakuwa ikimenyana na Day Break kwenye uwanja wa Kinesi, wakati kwenye Uwanja wa Makurumla, Friends Rangers wao watakuwa wakichuana vikali na Sharif Stars, huku kwenye Uwanja wa Airwing, Boom FC itakuwa ikikabiliana na Abajalo.

Ijuwe Historia ya maadhimisho ya Sikukuu ya Muungano wa Bara na Visiwani


LEO ni Aprili 26. Watanzania wote, ikiwapo Tanzania Bara, iliyokuwa ikiitwa Tanganyika na Zanzibar, wanashiriki kwa pamoja kusherehekea Sikukuu ya Muungano.
Waasisi wa Muungano, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kushoto na Abeid Amani Karume, wote kwa sasa ni marehemu.

Ni siku muhimu kwa Watanzania wote. Baba, mama, mjomba na shangazi kuanzia siku ya kwanza ya Muungano huu hadi leo, wanaikumbuka na kuitilia mkazo.
 Sherehe za Muungano Kitaifa zinafanyika katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, ambapo wananchi na viongozi wanashiriki kwenye maadhimisho hayo.

Pamoja na sherehe hizo, kila Mtanzania na asiyokuwa Mtanzania anapaswa kujua kuwa Mkataba wa Muungano ulitiwa saini na Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume, Aprili 22, 1964, Zanzibar.

Isha Mashauzi alia kwa kudaiwa kuiba Laki 7 dukani kwa watu


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKURUGENZI wa Mashauzi Classic, Isha Ramadhani “Mashauzi” amelalamikia kitendo cha kudaiwa kuiba Laki 7 dukani kwa mtu anayejulikana kwa jina la Halima na kulazimika kusota rumande kwa madai kimepangwa ili kumdhalilisha kwenye fani yake ya uimbaji wa taarabu, huku akimiliki kundi la Mashauzi Classic.
Isha Mashauzi, mwimbaji wa taarabu na Mkurugenzi wa Mashauzi Classic

Isha alifikishwa kituo cha Msimbazi kwa kuhusishwa na upotevu wa shilingi laki saba uliotokea kwenye duka moja la Kariakoo jijini Dar es Salaam.
 
Mmiliki wa duka hilo la nywele, amemfikisha Isha na mwenzake aitwae Halima kituoni hapo akidai alipotelewa na kiasi hicho cha pesa huku msanii huyo akiwa ni wa mwisho kuingia dukani mwake.
 
Handeni Kwetu Blog ilishuhudia pilika pilika za super star huyo kushikiliwa kwa muda saa 5 za usiku juzi huku mwimbaji huyo wa ‘Nani Kama Mama’ akisubiriwa na kamera za waandishi kwa nje.

SHEREHE ZA MUUNGANO



Tukubali ufa wa muungano na tuurekebishe

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KUMEKUWA na maneno makali kutoka kwa baadhi ya wanaojiita wanaharakati, wakitaka kuvunjwa kwa Muungano wa Tanzania Bara na Visiwani.
                       RAIS wa Tanzania, Jakaya Kikwete
Katika kuhaharalisha mahitaji yao, watu hao wamekuwa wakiorodhesha mambo kadhaa, wakionyesha kuwa ndio chanzo cha kuutoa uhai muungano huo ulioingiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambao kwa sasa ni marehemu.

Muungano huo uliingiwa rasmi Aprili 26 mwaka 1964 na kushuhudia Bara na visiwani ikiwa ni nchi moja yenye mpangalio thabiti wa kiutawala.

Hata hivyo, wataalamu wa mambo wanasema kuwa tangu siku ya kwanza ya Muungano huo, kero kadhaa zilianza kujitokeza na kukua hadi leo hii ambapo tunahushudia watu wakiupinga muungano huo.

Thursday, April 25, 2013

Kumekucha kimbembe cha Tuzo za Kili, shuhudia majina ya wakali wanaopambana

WANAO WANIA TUZO ZA KILI MUSIC AWARD 2013 HAWA HAPA

 

Msanii bora wa hiphop
Fid Q,
Joh Makini,
Kala Jeremiah,
Profesa J,
Stamina

Wimbo bora wa Mwaka:
Dear God Kala Jeremiah,
Leka Dutigite Kigoma All Stars,
Mapito - Mwasiti Ft Ally Nipishe,
Me and You -Ommy Dimpoz Ft Vanessa Mdee
Pete - Ben Pol.

Msanii bora wa Kiume
Ben Pol,
Diamond,
Linex,
Mzee Yusuf
Ommy Dimpoz.

TFF yapangua tena ratiba ya Ligi kati ya Simba na Ruvu Shooting iliyopangwa kufanyika leo Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa itafanyika Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.
                         Boniface Wambura, Msemaji wa TFF
Mabadiliko hayo yametokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kupitia msemaji wao Boniface Wambura, linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Ligi hiyo inaendelea kesho (Aprili 26 mwaka huu) kwa mechi kati ya Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Jumapili (Aprili 28 mwaka huu) itakuwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni Simba dhidi ya Polisi Morogoro.

January Makamba azuia watoa uchawi jimboni kwake Bumbuli



Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Bumbuli kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), January Makamba, ameelezea kusikitishwa kwake na masuala ya imani ya kishirikina kupiga hodi kwenye Jimbo lake.

January Makamba, Mbunge wa Bumbuli
Akielezea kwa kina kwenye akaunti yake ya facebook, Makamba alisema kuwa Ijumaa na Jumamosi walikwenda Bumbuli watu wanaodai wana uwezo wa kutoa wachawi na kuamua kuwachangisha watu fedha kwa ajili ya zoezi hilo na kudhalilisha wazee na kina mama wengi na kusababisha  wanyanyaswe na kufanyiwa fujo.
January Makamba kushoto akizungumza na baadhi ya wananchi wake jimboni Bumbuli hivi karibuni.
Alisema kuwa baada ya kuona hivyo, aliamua kuzungumza na viongozi na Mkuu wa Wilaya kwamba watu hao wafukuzwe mara moja na wakamatwe kwasababu zoezi hilo ni kinyume cha Sheria za nchi.

"Vilevile, katika zama hizi mambo ya uchawi na kutafuta wachawi hayana nafasi kabisa. Ni mambo ambayo yametubakiza nyuma kimaendeleo miaka nenda rudi.

Warembo wachangamkia ushiriki wa Miss Kibaha 2013



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WAREMBO wamejitokeza katika kushiriki shindano lijalo la Redds Miss Kibaha 2013.
AKhadija Kalili, Mkurugenzi wa Linda Media Solution
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO), ambaye pia ndio Mratibu wa shindano hilo Khadija Kalili alisema amefurahishwa na mwitikio wa warembo waliojitokeza hadi sasa katika kuwania taji la Miss Kibaha.
 
“Mwitikio wa warembo kwa kweli unatia moyo hivyo kwa kuwa muda wa kufunga milango ya kupokea warembo bado iko wazi, mrembo yoyote anayejiamini kwamba ana vigezo anakaribishwa. Tunataka shindano la mwaka huu liwe na ushindani zaidi,” alisema Kalili.

MGODI UNAOTEMBEA



Ni aibu, thamani ya kura yao imegeuka matusi
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BUNGE la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma, limeleta picha mpya inayochefua kuitazama mara kwa mara. Ni picha isiyofurahisha macho wala hisia za ndani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete
Ni kutokana na baadhi ya wabunge wetu kujiondoa kwenye uwakilishi wa wananchi kwa kutetea maslahi ya wapiga kura wao, badala yake wanaparuana wenyewe pamoja na kupeana maneno ya shombo, kejeli, matusi ya kila aina.
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freemani Mbowe
Katika mfululizo wa makala zangu, nilijaribu kupinga maoni ya Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan aliyechangia kwa kuwataka watu kabla ya kugombea Ubunge, wapitie kwanza jeshi ili wajifunze uzalendo.

Sio kweli, maana uzalendo wa kweli hauwezi kupatikana JKT wanapofundishwa kwa wiki moja au mbili, tena wakiachwa wafanye kila wakipendacho, ikiwapo kupigana picha na kuziingiza kwenye mitandao ya kijamii, hasa wa facebook.

Ally Choki aapa kuwanyakua wa kuipaisha zaidi Extra Bongo



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKURUGENZI wa bendi ya Extra Bongo, Next Level, Ally Choki, amesema kwamba yupo kwenye mikakati ya kuwanyakua na kuwatambulisha waimbaji wasiozidi watatu kwa ajili ya kuimarisha zaidi safu yao.
Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki
Extra Bongo imezidi kuteka nyoyo za wapenzi wao, huku shoo zao zikipendwa na watu wengi katika kumbi mbalimbali za starehe nchini.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Choki alisema kwamba anaamini kufanikiwa kuwapata waimbaji wao mambo yao yatakuwa mazuri katika hali ya kujiweka sawa kiushindani.

Tuesday, April 23, 2013

Kim Poulsen atangaza timu ya pili Stars, Young Taifa Stars

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza timu ya pili ya Taifa (Young Taifa Stars) atakayoitumia kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya wakubwa.
Kocha wa Stars, Kim Poulsen
Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (Aprili 23 mwaka huu) kabla ya kutaja kikosi hicho, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.

Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini atatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.

Ligi Daraja la Pili Mkoa wa Dar es Salaam yaendelea kushika kasi


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
LIGI Darajala la Pili Mkoa wa Dar es Salaam , hatua ya sita bora imezidi kushika kasi ambapo hadi sasa timu ya Red Coast inaongoza ligi hiyo kwa kujikusanyia pointi 7 baada ya kucheza mechi tatu.
Ofisa Habari wa DRFA, Mohamed Mharizo
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam, Mohamed Mharizo, Red Coast imejikusanyia pointi hizo baada ya kuzifunga  Abajalo bao 1-0,  huku ikilazimishwa sare ya bila kufungana na Friends Rangers na jana Jumatatu iliichapa Sharif mabao 3-1, katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Airwing.

Familia yaendelea kushinikiza Wastara aendelee kupumzika nchini Omani



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MJANE wa msanii maarufu wa filamu nchini, Juma Kilowoko (Wastara Juma), ametangaza kuendelea kuishi nchini Omani kwa miezi miwili ijayo kama sehemu yake ya kujipumzisha tangu alipompoteza mume wake aliyempenda kwa dhati.
                                   Wastara kwa sasa yupo nchini Omani kwenye mapumziko
                                              Sajuki enzi za uhai wake
Wastara siku ya msiba wa mume wake
Wastara kwa sasa yupo eda ya mume wake Sajuki, aliyekufa katika Hospitali ya Muhimbili mapema mwaka huu na kushtua wadau wengi wa filamu Tanzania, kutokana na madhira yake ya ugonjwa.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...