https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, February 23, 2017

Jumia yazindua huduma za ndege

 Ofisa Habari wa Kampuni ya Jumia Travel, Geofrey Kijangwa (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu kampuni hiyo kuzindua huduma za ndege. Kushoto ni Meneja Mkazi wa Kampuni hiyo, Fatema Dharsee. 

Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI ya Jumia Travel imetangaza kuwa imezindua huduma za ndege kwa ajili ya wasafiri, hatua ambayo itapelekea kutanua wigo wa huduma zake. 

Uzinduzi huu unakuja kipindi ambacho Kilele cha Mkutano wa Pili wa Masuala ya Anga Afrika ukifanyika nchini Rwanda. 

Kwa sasa mtandao huo nambari moja kwa huduma za hoteli barani Afrika unatoa huduma za ndani na nje ya nchi kwa kushirikiana na mashirika makubwa ya ndege yakiwemo Precision Air, Kenya Airways, Rwandair Express, Qatar Airways, Emirates, Ethiopian Airlines, South African Airways, KLM, Fly Dubai, Turkish Airlines, Air Arabia, Air Seychelles miongoni mwa nyinginezo.
 Meneja Mkazi wa Kampuni hiyo, Fatema Dharsee akizungumza na wanahabari.

TAYODEA yapongezwa kuinua uchumi wa vijana jijini Tanga

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa uzinduzi wa akibadhi vifaa vya vijana wa mradi wa WEKEZA (Wezesha Ustawi Endelevu kiwango cha Elimu Kuzuia Ajira kwa watoto) kulia ni Mkurugenzi wa Tayodea, David Chanyegea na kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga,Faidha Salim

 Mkurugenzi wa Tayodea, David Chanyege akizungumza wakati wa halfa hiyo kushoto kwake ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza.

Wednesday, February 22, 2017

Semina yakutanisha vijana mbalimbali kujadili changamoto zao


Bwana Jackson Oganga akiwa anatoa maelezo kwa vijana jinsi ya kupata 'Scholarship' katika zinazotolewa sehemu mbalimbali.
Mwakilishi wa Asasi ya Kiraia  Global Peace Foundation (GPF) Tanzania aliyewakilisha katika Semina hiyo Bi. Anna Mwalongo akielezea kwa kifupi kuhusu Asasi hiyo.

Wajasiriamali watembelewa katika maeneo yao nchini Tanzania

Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Ubwa Ibrahim akiwa katika moja ya mikoa kukagua na kuimarisha shughuli za Wajasiriamali wanachama wa kampuni hiyo katika mikoa mbalimbali nchini. Tayari hadi leo ameshafanya ziara katika mikoa ya Iringa, Tabora, Kigoma, Manyara, Arusha na Kilimanjaro.

Mafunzo yanayotolewa na kampuni hiyo kwa wajasiriamali zaidi ya 400,000 nchini ni. ufugaji wa kuku wa chotara, sungura, samaki pamoja na kilimo bishara cha mbogamboga na matunda.

Pia husaidia kupatika kwa masoko ya bidhaa hizo, pamoja na kuwaunganisha katika taasisi mbalimbali za kifedha ili kupata mikopo kirahisi. Imeandaliwa na Richard Mwaikenda.

Tuesday, February 21, 2017

Bayport yatoa kompyuta nne kwa shule za Msingi Dodoma Mjini

Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mvunde (kulia) akipokea msaada wa Kompyuta Nne kwa Meneja Masoko na Mawasiliano wa Taasisi ya Kifedha Bayport Tanzania, Ngula Cheyo mjini Dodoma leo asubuhi. Kushoto ni Meneja wa Kanda ya Kati wa taasisi hiyo, Kushoto ni Meneja wa Kanda ya Kati wa taasisi hiyo, Christopher Kihwele. 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
TAASISI ya Kifedha ya Bayport Financial Services, jana imemkabidhi kompyuta nne Naibu Waziri wa Vijana, Kazi na Ajira, Mheshimiwa Anthon Mavunde kwa ajili ya shule za Msingi za Majengo, Chigonge, Mahomanyika na Uhuru zilizopo mjini Dodoma.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Majengo, wakinyoosha mikono juu katika tukio la kukabidhiwa kompyuta nne za Bayport Financial Services, zikipokewa na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde.

Makabidhiano hayo yalifanyika katika shule ya Msingi Majengo, ambapo kompyuta hizo zina lengo la kuongeza kiwango cha elimu mkoani Dodoma. Akizungumza leo mjini Dodoma, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, alisema kwamba msaada huo wa kompyuta umetokana na dhamira yao ya kusaidia jamii kwenye sekta ya elimu kama njia ya kuikomboa jamii.

Alisema kwamba si mara ya kwanza kusaidia sekta ya elimu kutokana na kujitokeza mara kadhaa kujenga madarasa, kununua thamani za shule pamoja na kudhamini mikopo ya elimu ya juu na vitabu. 
Baadhi ya walimu wa Shule ya Msingi Majengo, wakisoma shairi mahususi kwa ajili ya Naibu Waziri wa Kazi, Ajira, Vijana, Anthony Mavunde wakati anakabidhiwa kompyuta nne kutoka kwenye taasisi ya Bayport Financial Services.

“Bayport tuna lengo la kuikwamua jamii katika maendeleo kwa kuhakikisha kwamba tunakuza kiwango cha elimu, hivyo kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali kuhamia Dodoma, tumeamua kutoa kompyuta nne kwa kuboresha miundo mbinu ya elimu ili nchi yetu isonge mbele.

Monday, February 20, 2017

Mkuu wa wilaya Muheza ajionea zoezi la upasuaji wa macho Kituo cha Afya Ubwari

MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo katika akiingia kwenye kituo cha Afya Cha Ubwari leo wakati alipokwenda kuangalia zoezi la upasuaji wa macho kwa wakazi wa wilaya hiyo wanaokabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo ya mtoto wa Jicho iliyoendeshwa na Taasisi ya Medewell Charitable Health Centre kulia ni Mganga Mkuu wa wilaya hiyo,Mathew Mganga na kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Luiza Mlelwa.



Baadhi ya wazee waliofanyiwa upasuaji wakisubiri zoezi la kupatiwa dawa na miwani
Baadhi ya wananchi waliofanyiwa upasuaji wakisubiri zoezi la kupatiwa dawa na miwani.

Mbunge wa Mkuranga aongoza tukio la kuchangia damu Dar es Salaam

Mgeni rasmi wa kongamano la kuchangia damu lililoandaliwa na Tanzania Yemen Professional Foundation (TYPF), Abdallah Ulega ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mkuranga akizungumza umuhimu wa kila Mtanzania kujitolea damu ili kuinusuru jamii yake. Picha zote na Mpiga Picha Wetu.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MBUNGE wa Mkuranga, Mheshimiwa Abdallah Ulega, mwishoni mwa wiki aliongozana na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jasem Al Najem, katika tukio la uchangiaji wa damu lililoandaliwa na Taasisi ya Tanzania Yemen Professional Foundation (TYPF), lililofanyika katika Ukumbi wa City Garden, jijini Dar es Salaam. Katika tukio hilo, watu mbalimbali walishiriki katika uchangiaji damu kama sehemu ya kutatua changamoto ya upungufu wa damu kwa wenye uhitaji, wakiwamo akina mama wajawazito, ajali za barabarani na majanga mengine.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, H.E Jasem Al Najem akitolewa damu katika tukio la kuchangia damu lililofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa City Garden, jijini Dar es Salaam.


Akizungumza katika uchangiaji huo, Mbunge Ulega alisema kwamba jukumu la kuchangia damu linamuhusu kila Mtanzania, huku akiwataka watu kujenga mazoea ya kujitolea damu ili kuondoa upungufu wa damu.

Alisema kwamba mahitaji ya damu kwa nchi yetu ni makubwa, hivyo amefarijika kwa kupata mwaliko wa kuwa mgeni rasmi sambamba na kuongoza tukio hilo la uchangiaji wa damu, akiamini amejitolea jambo la msingi na la lazima.

Monday, February 13, 2017

Mke wa Rais Magufuli atembelea wasiojiweza mkoani Singida

NA MWANDISHI MAALUM, SINGIDA
MKE wa Rais Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wametoa rai kwa Wanzania kujenga tabia ya kusaidia watu wasiojiweza na wenye mahitaji maalumu.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wakilakiwa kwa furaha walipowasili katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo.
Wake hao wa viongozi pia wamewatahadharisha watumishi wanaofanya kazi katika vituo vya kulelea wazee wasiojiweza wahakikishe misaada inayotolewa na wadau mbalimbali inawafikia walengwa bila ya kuchakachuliwa.

Wameyasema hayo leo (Jumatatu, Februari 13, 2017) wakati walipotembelea Makazi ya Wazee wasiojiweza na walemavu watokanao na ugonjwa wa ukoma ya Sukamahela wilayani Manyoni Mkoani Singida. Katika kituo hicho wamekabidhi tani 7.5 za vyakula mbalimbali ukiwemo mchele, unga wa sembe na maharage, ambapo Mama Janeth amewataka viongozi wa kituo kuhakikisha chakula hicho hakichakachuliwi.

Akizungumza na wazee wa makaazi hayo, viongozi mbalimbali na wananchi wanaozunguka eneo hilo Mama Janeth amesema “Naomba chakula hiki kitunzwe vizuri na hakikisheni kinawafikia walengwa na kisichakachuliwe hii ni sadaka,”.

Kwa upande wake Mama Mary amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza na kuwasaidia wazee wanaoishi katika makaazi ya kulelea walemavu na wasiojiweza nchini kwa sababu wanakabiliwa na changamoto nyingi. “Watanzania wote popote mlipo tukumbuke kutembelea vituo vya kulelea wazee kikiwepo na hiki tulichokitembelea leo cha Sukamahela na kutoa misaada mbalimbali kkwa kadri tutakavyojaaliwa,” amesema.

DC Muwango ataka ardhi iliyovamiwa irejeshwe

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango akisisitiza umuhimu wa kufanya mazoezi.

Na Mathias Canal, Lindi
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango ameitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo irejeshe maeneo yote ya wazi yaliyo vamiwa na kutumika kinyume cha matumizi yaliyolengwa.

Dc Muwango ametoa agizo hilo mjini Nachingwea kwenye uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayoweza kuzuilika kupitia mazoezi na michezo.

Uzinduzi huo uliofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine ambapo Alisema kuwa yeye kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo anatambua na anazotaarifa za kutosha kuwa maeneo mengi ambayo yalitengwa kwa ajili michezo na shuguli nyingine za umma yamevamiwa na kubadilishwa matumizi.
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango akionyesha mfano wa ufanayaji mazoezi
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya hiyo Mhe Rukia Muwango akifanya mazoezi katika uzinduzi huo.

Maonyesho ya utalii nchini Saudi Arabia yaipaisha Tanzania

Baaadhi ya watu mbalimbali wakitembelea banda la Tanzania, nchini Saudi Arabia, katika maonyesho ya utalii ya '(Travel and Tourism Pioneers Forum - 2017).

Na Mwandishi Maalum, Saudi Arabia
Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia mwishoni mwa juma hili ulishiriki katika maonyesho ya Safari na Utalii yajulikanayo kama '(Travel and Tourism Pioneers Forum - 2017).

Maonyesho ya TPF 2017 ambayo hufanyika kila mwaka kwa uandalizi Al Awsat Expo chini ya uhisani wa Mwana Mfalme HRH Prince Dr. Seif al Islam bin Saud bin Abdulaziz, yamefanyika kwa mafanikio huku ubalozi wa Tanzania ukifanikiwa kwa kiasi kikubwa kutangaza utalii wa Tanzania.

Akizungumza katika maonyesho hayo, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, H.E Hemed Mgaza, alisema kwamba maonesho hayo yalikuwa maalumu kwa wafanya maamuzi na viongozi wa asasi za utalii (decision makers and leaders and tourisma leaders) nchini Saudi Arabia.
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, H.E Hemed Mgaza, mwenye suti nyeusi akizungumza jambo na wageni waliotembelea katika banda la Tanzania kwenye maonyesho hayo.

Alisema kwamba kuwa banda la Tanzania lilifanikiwa kuonesha vivutio vya utalii vya Tanzania ikiwemo mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, hifadhi za taifa, maeneo ya kihistoria ya Zanzibar, kilwa na Bagamoyo. 

Saturday, February 11, 2017

Makamu wa Rais Tanzania aendeleza kasi ya mazoezi ya viungo mjini Dodoma


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa kukabidhi matembezi ya Uzinduzi wa Kitaifa wa Mazoezi ya Viungo kwa wananchi wote ya kupambana na magonjwa yasioambukiza, Makao Makuu ya nchi Dodoma.

Makamu wa Rais Mh.Samia Suluhu Hassan akishiriki mazoezi mapema leo asubuhi mjini Dodoma ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa katika Uzinduzi wa Kitaifa wa Mazoezi ya Viungo kwa wananchi wote ya kupambana na magonjwa yasioambukiza, mjini Dodoma.Pichani kushoto ni Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Mh.Nape Nnauye.

Khadija Kopa ataka wanawake wajikwamue kiuchumi



Baadhi ya nguo za maharusi zinavyoonekana katika duka la urembo na mitindo lililozinduliwa rasmi jana, huku mgeni rasmi akiwa ni mwimbaji wa muziki wa taarabu nchini Tanzania, Bi Khadija Kopa.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWIMBAJI wa muziki wa taarab nchini Tanzania, Bi Khadija Kopa, amewataka wanawake kuendelea kujikwamua kiuchumi wao wenyewe bila kusubiri kuwezeshwa na wanaume.
Khadija aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa duka kubwa la kisasa la urembo na nguo za wanawake linalojihusisha pia na kupamba maharusi, kukodisha na kuuza nguo za maharusi, linalojulikana kama Taiba Beauty, linalomilikiwa na mjasiriamali Twaiba Ahmed Ally.
Mwimbaji mkongwe wa muziki wa taarabu nchini, Bi Khadija Kopa, akizungumza na waandishi hawapo pichani katika uzinduzi wa duka la nguo za wanawake na za harusi linalomilikiwa na mwanamama Twaiba Ahmed Ally.

Alisema kwamba wapo wanawake wanaoamini kuwa hawawezi kuendelea hadi wawezeshwe, jambo linalohitaji kupingwa vikali ili wanawake waweze kupiga hatua kiuchumi na kujikomboa wao wenyewe.
Mmiliki wa duka la nguo za maharusi lililopo mtaa wa Livingstone na Mkunguni, Bi Twaiba Ahmed Ally, katikati akikata keki ya uzinduzi wa duka hilo jana. Kulia ni mwimbaji wa taarabu nchini, Khadija Kopa akilishwa keki kama mgeni rasmi. Kushoto ni mtangazaji wa kipindi cha Ng'ari Ng'ari kutoka Clouds Tv, Sakina Lyoka.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...