https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, August 31, 2013

MAMBO FULANI MUHIMU:Umegundua nini kwa umpendae, chukua hatua

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KUNA watu ambao wanaendelea kuingia kwenye wasiwasi mkubwa kwasababu ya kutofurahia uhusiano wao au ndoa yao kwa wale waliofanikiwa.
Mambo Fulani Muhimu kwa watu muhimu.
Hawa ni wale wanaoshi bila hata kugundua namna gani ya kuwafurahisha watu wao.

Ni wale ambao licha ya kutarajia makubwa kutoka kwa wapenzi wao, ila wametumbukia katika wasiwasi wa aina yake.

Ndugu msomaji wangu, katika uhusiano wa kimapenzi, kuna wale ambao wapo pamoja lakini wanapokuwa kwenye tendo la ndoa, mmoja wapo haridhiki.

Matokeo hayo yanamfanya mmoja wapo kuishi kwa mashaka, akiamini kuwa uhusiano wake utaingia kwenye utata, pale mwenzake atakapobaini mapungufu yake.

Nasema haya kwa kuamini kuwa mambo haya yapo kwenye jamii yetu. Sio kila mmoja anaishi kwa raha na mwenzake. Wale ambao tangu waanze uhusiano wao wamekuwa na furaha, hasa kwasababu ya wote kuridhishana katika hatua mbalimbali, wengine hilo ni ndoto kwao.

Pamoja na yote hayo, ikiwa wewe ndio muathirika katika suala hilo, hupaswi kubaki kimya. Unatakiwa uliweke wazi suala hilo kwa mwenzako.

Kuna watu wanaofanya makosa, pale anapogundua kuwa kila siku uwezo wa mwenzake, hasa katika suala la tendo la ndoa unazidi kushuka chini.

Kuna mengi yanayoweza kuchangia suala hilo, hasa kuathirika kisaikolojia, ila mwisho wa siku bado wawili hao wanaweza kukaa chini na kuliangalia kwa mapana.

Ni bora ukamuelezea mwenzako tofauti zake zote ili iwe njia ya kufika mbali kwenye uhusiano wenu. Ni jambo baya kubaki kimya hali ya kuwa unajua una tatizo katika mwili wako.

Huu ndio ukweli, maana mambo kama hayo yasipoangaliwa kwa kina, huzalisha mihemko katika uhusiano.

Ikiwa wewe ni mmoja wa wale waliokuwa kwenye uhusiano na mtu ambaye ana tatizo linalomkabiri, likiwapo hili la kushindwa kumfikisha mwenzako kileleni, basi badala ya kubaki kimya, chukua hatua.

Ninaposema kuchukua hatua, sina maana ya mtu huyo kutoka nje ya ndoa yake au kuwa na mpenzi wa pembeni. Unaweza kumuelezea mwenzako tatizo lako na kujadili njia ya kupita.

Mengi yatakuja katika kikao hicho wewe na mwenzako. Lakini baadaye majibu halisi yatapatikana. Kama una ugonjwa ulioanza kunyemelea, pia mtagundua.

Lakini kubaki kimya ni kulifanya tatizo hilo lizidi kuota mizizi na baadaye huwa ni sababu ya kwanza ya kuongeza usaliti kwa kiwango kikubwa mno.

Uhusiano una changamoto nyingi mno. Moja wapo ni pale mmoja wpao anaposhindwa kumkabiri mwenzake na kumfikisha pale anapohitaji.

Ni pale mmoja wapo anapogundua yupo kwenye uhusiano na mtu ambaye anaweza kumfanya akasahau shida zake kwa kupewa raha anazohitaji.

Najua si wote ni wajuzi na hakuna anayejua yote, ila ni bora tukafahamu changamoto hizo kwa ajili ya kumaliza tatizo.

Unapaswa kujiuliza maswali haya. Kwanini mpenzi wako au mke wako haridhiki. Je, unahisi una matatizo ya kiafya yanayosababisha nguvu zako za kiume zipunguwe kama sio kwisha kabisa?

Je, mtu wako ameanza kuligundua hilo na kumsababishia msongo wa mawazo? Baada ya kuwaza haya, unapaswa kukaa chini ili ubaini tatizo.

Kwa bahati nzuri, kwa wale wanaowapenda kwa moyo wote watu wao, hatua hiyo haitakuwa kuongeza tatizo bali kulitatua, ukizingatia kuwa ndio njia nzuri ya kuhakikisha kuwa wawili hao wanakuwa kwenye upendo wao.

Msipoweza kulitatua jambo hilo, ni wazi mwelekeo wake ni mbaya, maana wengi wao wameachana kwasababu suala hilo linaweza kuzalisha usaliti, hasa pale mmoja wapo anapoamua kutafuta furaha kwa mtu mwingine.

+255 712053949

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...