https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, September 15, 2014

Naibu Waziri wa Nishati na Madini akizungumza

Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mh,Stephen Masele akizungumza kwenye uzinduzi huo uliovuta hisia za wanakijiji wengi. Naibu Waziri wa Nishati na Madini akizungumza na Wananchi Mkurugenzi Mtendaji wa Geita Gold Mine,Michael Van Anen

Monday, September 08, 2014

Tamasha la 'Handeni Kwetu' lapania kuvunja rekodi


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MRATIBU Mkuu wa Tamasha la Utamaduni Handeni, maarufu kama ‘Handeni Kwetu’, Kambi Mbwana, ameapa kuhakikisha kuwa tamasha lao msimu wa 2014 linakuwa la aina yake na kuvunja rekodi ya mwaka jana lilipofanyika kwa mara ya kwanza wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu, Kambi Mbwana, pichani.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mbwana alisema kuwa hiyo ni kutokana na kutamani kushirikisha wasanii wengi kutoka Tanga na Tanzania kwa ujumla.


Alisema kwamba mwaka jana wasanii zaidi ya 200 walionyesha uwezo wao kutoka kwa vikundi mbalimbali vya wilayani Handeni na jijini Dar es Salaam.


“Mwaka jana vikundi zaidi ya 10 vyenye wasanii wasiopungua 15 walipata nafasi ya kupanda jukwaani kuonyesha vipaji vyao, ukiacha wasanii wanaotoka kwenye Kambi ya jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wa Mgambo waliozidi 80.


“Wakati tunajivunia mafanikio haya, tunaamini msimu huu utakuwa mzuri zaidi tukiamini kuwa tutavunja rekodi ya mwaka jana, ambapo tulishuhudia burudani mbalimbali, ikiwamo hadithi zilizohusu watu wa Handeni, bila kusahau vyakula vya asili pamoja na michezo waliyokuwa wakicheza wazee wetu enzi hizo,” alisema Mbwana.


Kwa mujibu wa Mbwana, mipango ya kuboresha tamasha hilo imepamba moto ambapo kwa sasa utafiti wa ubora wa vikundi nje ya wilaya ya Handeni inafanywa ili kuhakikisha kuwa wasanii watakaopanda jukwaani wanakuwa na uwezo wa juu na kufanikisha kwa dhati kukuza sekta ya utamaduni pamoja na uchumi wa Tanzania.

Monday, September 01, 2014

Tamasha la Handeni Kwetu kufanyika Desemba 13 mwaka huu


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

TAMASHA kubwa la umataduni linalojulikana kama 'Handeni Kwetu' limepangwa kufanyika Desemba 13 mwaka huu, katika Uwanja wa Azimio, wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu, Kambi Mbwana, akizungumza jambo katika tamasha la mwaka lililofanyika Desemba 14. Mwaka huu tamasha hilo litafanyika Desemba 13, Siku ya Jumamosi, katika Uwanja wa Azimio, wilayani Handeni, mkoani Tanga. Picha na Maktaba Yetu.
Wasanii wa kundi la ngoma za asili la Mgambo JKT, wilayani Handeni, mkoani Tanga, wakitoa burudani katika tamasha hilo mwaka jana. Mwaka huu litafanyika Desemba 13, Siku ya Jumamosi, katika Uwanja wa Azimio, wilayani Handeni, mkoani Tanga. Picha na Maktaba Yetu.
Mkuu wa Wilaya Handeni, Muhingo Rweyemamu (katikati), akifurahia katika tamasha hilo mwaka jana lililofanyika Desemba 14. Mwaka huu litafanyika Desemba 13, Siku ya Jumamosi, katika Uwanja wa Azimio, wilayani Handeni, mkoani Tanga. Kulia kwake ni Afisa Utawala wa wilaya ya Handeni, Upendo Magashi. Picha na Maktaba Yetu.


Katika tamasha hilo linalofanyika kwa mara pili, burudani mbalimbali za ngoma za asili zinatarajiwa kuonekana jukwaani, ambapo pia vikundi kutoka nje ya Handeni, mkoani Tanga navyo vitaalikwa kwa ajili ya kwenda kutoa burudani wilayani humo.


Akizungumzia hilo, jijini Dar es Salaam, Mratibu Mkuu wa tamasha hilo, Kambi Mbwana, alisema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yanawekwa ili kuliweka katika kilele cha ubora na kuchangia maendeleo ya sanaa na uchumi kwa ujumla.


Alisema kuwa mwaka jana tamasha hilo lilianza kwa mafanikio makubwa, ambapo wageni mbalimbali walifika wilayani humo, jambo lililochangia pia kuitangaza Handeni na mkoa mzima wa Tanga.


“Mwaka huu tumeweka mikakati kabambe ya kuhakikisha kuwa tamasha letu linaendelea kukua kwa kasi baada ya kuanzishwa kwa mafanikio makubwa mwaka jana.


“Naamini kuwa haya ni matunda ya kushirikiana kwa pamoja na wadau wote, ikiwamo serikali kwa kupitia ofisi zote za wilaya ya Handeni, hivyo watu wajiandae mambo mazuri na makubwa kutoka kwenye tamasha hili,” alisema Mbwana.


Tamasha la utamaduni la Handeni, linalojulikana kama Handeni Kwetu, ni miongoni mwa matamasha yenye mchango mkubwa, ambapo kwa mwaka jana Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ndio waliokuwa wadhamini wakuu na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuliweka katika mguso wa aina yake.


LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...