https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, August 28, 2013

Kaseba: Naenda kimya kimya ili nisiwape woga wapinzani wangu


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa Ngumi za kulipwa nchini, Japhet Kaseba, amesema kwa sasa anafanya mambo kimya kimya ili ajiweke sawa zaidi katika tasnia ya mchezo huo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Kaseba alisema kwamba mchezo wa masumbwi umekuwa na changamoto nyingi, ukiwamo uhaba wa kupatikanaa mapambano yenye mguso.

Alisema licha ya uhaba huo, kwa upande wake anaendelea na mazoezi makali, japo analazimika kupunguza majigambo kwa kuhofia kuwapaa woga mabondia wengine.

“Nafanya mambo yangu kimya kimya bila hata kupiga       kelele ili nisiwape woga mabondia wanaofikiria kupambana na mimi katika siku za usoni,” alisema Kaseba.

Kwa mujibu wa Kaseba, sasa anasubiria matokeo ya pambano la Thomas Mashali na Mada Maugo, hasa baada ya Maugo aliyekuwa kwenye mipango ya kucheza naye Septemba 7 kukubali kupambana na Mashali Agosti 30 mwaka huu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...