https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, August 31, 2013

Francis Cheka amtandika Mmarekani Phil Williams Ukumbi wa Diamond Jubilee na kuwapa raha Watanzania


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa Tanzania, Francis Cheka, ameendeleza ubabe wake baada ya kumtandika mpinzani wake Phil Williams katika pambano lao lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.
Bondia wa Tanzania, Francis Cheka, pichani
Ushindi huo wa Cheka ni furaha kubwa kwa Watanzania wote, hususan wale wanaotokea mkoani Morogoro ambapo mkali huyo ndipo anapotokea kwenye mji huo.
Cheka na Phil Williams wakimenyana ulingoni.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara akimvisha mkanda wa Ubingwa wa Dunia wa WBF, Francis Cheka, baada ya kumpiga mpinzani wake Phil Williams katika Ukumbi wa Diamond Jubuilee.

Cheka alipata ushindi huo na kunyakua ubingwa wa Dunia wa WBF, baada ya kumpiga Williams kwa pointi kuonyesha kuwa yeye ni mkali na hana mpinzani hapa Tanzania.

Mbali na kufanikiwa kumchapa Mmarekani huyo, mara kwa mara Cheka amekuwa akiibuka na ushindi kila anapoingia ulingoni kupambana na mabondia wa Tanzania.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...