https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, March 03, 2013

Wacheza gofu waonyesha uwezo wao GYMKHANA

Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Mishack Ugulo, pichani.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WANAMICHEZO mbalimbali wa mchezo wa gofu, jana walionyeshana uwezo katika mashindano yaliyodhaminiwa na benki ya BankABC, yakihudhuriwa pia na viongozi wa juu ya benki hiyo yenye matawi yake Dar es Salaam na Arusha.

Mashindano hayo yalivutia wachezaji wengi, wakiwamo wafanyabiashara na wateja wa BankABC, huku dhamira ikiwa ni kuendeleza juhudi za kuuweka mchezo wa gofu katika kiwango cha juu.

Akizungumza katika ufunguzi wa shindano hilo la siku moja katika Viwanja vya Gymkhana, yaliyoanza asuhubi hadi jioni, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya BankABC, Misheck Ugalo, alisema kuwa wameamua kudhamini shindano hilo ili kushiriki juhudi za kuuletea mafanikio mchezo huo.

Alisema benki yao ina haki ya kushiriki pamoja na wateja wao katika sekta ya michezo, ukiwamo gofu unaopendwa na watu wengi.

“Leo (jana) tumeamua kuwa na wateja wetu katika kudhamini gofu ambayo hakika ni mchezo mzuri unaohitaji umakini katika uchezaji wake.

“Shindano hili la siku moja nadhani litakuwa na tija hasa kama washiriki wote waliojiandikisha kushindana wataonyesha uwezo wao halisi,” alisema.

Benki ya BankABC sio mara yake ya kwanza kujiingiza kwenye michezo, hasa baada ya mwaka jana kudhamini michuano ya ‘BankABC SUP8R 2012.

.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...