https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 30, 2013

Idadi ya vifo yaongezeka ghorofa lililoanguka jana



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
HALI ya uokoaji katika jengo la ghorofa 16 lililoanguka jana mtaa wa Indira ghandi, Kariakoo jijini Dar es Salaam inaendelea, huku hadi sasa watu 18 wakiwa wamekutwa wameshapoteza maisha.
Pichani, uokoaji ikiendelea
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Saidik, alitembelea muda sio mrefu kwa ajili ya kujionea hali ya uokoaji inavyoendelea katika eneo hilo lililoibua taharuki kubwa.

Jana, Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, alitembelea pia katika eneo hilo na kujionea jinsi lilivyoanguka na kusababisha mtafaruku mkubwa kwa watu waliokuwa kwenye kadhia hiyo.

Juhudi za kuokoa watu waliokuwa kwenye ajali hiyo zilipamba moto dakika chache baada ya habari hizo kufika kwa vyombo vya Dola, huku viongozi wa vyama vya siasa na serikali kuwa bega kwa bega katika kufanikisha juhudi za kunusuru roho za watu wao.

Mwili mmoja umeopolewa muda mfupi uliopita, ikiwa ni masaa kadhaa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Sadik kufika, wakati tayari idadi ya watu 17 ilishatangazwa tangu jana.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...