https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 09, 2013

Yanga, Toto African hapatoshi leo uwanja wa Taifa



Baadhi ya wachezaji wa Yanga wakiwa mazoezini.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MABINGWA wa zamani wa Tanzania Bara, Yanga SC, leo inaingia uwanjani kumenyana na timu ya Toto African ya jijini Mwanza, mechi itakayopigwa katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Mbali na Yanga na Toto African, mechi nyingine itakayochezwa leo itahusisha timu ya Polisi Morogoro dhidi ya Azam, itakayochezwa katika Uwanja wa Chamazi, jijini Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo kati ya Yanga na Toto, mwamuzi atakuwa ni
Andrew Shamba kutoka Pwani, akisaidiwa na Abdallah Mkomwa pamoja na Abdallah Rashid wote kutoka mkoani Pwani, wakati Kamishna ni Salim Singano kutoka Tanga, wakati Mtathmini wa waamuzi amepangwa kuwa Alfred Lwiza.

Kocha wa timu ya Yanga, Ernest Brandit, ametangaza hali ya hatari kwa timu ya Toto African, akisema kuwa amejipanga imara kuhakikisha kuwa wanatoka na pointi tatu na kutwaa ubingwa wa Bara.

Yanga inaingia uwanjani huku wakiwa na pointi 42, akifuatiwa na Azam yenye pointi 36, timu ambayo nayo ipo kwenye nafasi nzuri ya kuweza kutwaa ubingwa huo.

Nayo Azam ikiwa chini ya kocha wao Stewart Hall, yenyewe imepania vilivyo kuhakikisha kuwa wanaibuka na ushindi kwa ajili ya kujipatia pointi 29, wakiamini kuwa watazidi kusumbuana na vinara wa ligi hiyo, ingawa Hall hatakuwa kwenye benchi la timu yake kwasababu ya kufungiwa mechi tatu na Kamati ya Ligi kwa kitendo chake cha utovu wa nidhamu.

Mwamuzi wa mchezo wa Azam na Polisi amepangwa kuwa Charles Komba kutoka mkoani Dodoma, wakati Simon Mberwa kutoka mkoani Pwani, atakuwa Kamishina.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...