https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, March 16, 2013

Rais Kikwete akiamua atawaokoa wasanii Tanzania



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
NIMEKUWA nikifuatilia na kukoshwa na mwendo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, hasa katika upande wa kuunga mkono sanaa na wasanii hapa nchini.

Mara kwa mara Rais Kikwete amekuwa akitoa kwa moyo wote kuwaunga mkono wasanii, jambo ambalo hakika halitasahauliwa na watu wote, hasa wale wanaofuatilia sanaa Tanzania.


Hapo kipindi cha nyuma, ilikuwa ni ngumu kumuona rais anakuwa kwenye sehemu ya jamii zote, ukizingatia kuwa katika kipindi cha utawala wa marais waliotangulia, akiwamo Benjamin Mkapa, Rais Ali Hassan Mwinyi, sanaa iliitwa ni uhuni.

Si ajabu nao waliogopa kuitwa wahuni, ndio maana uwepo wao haukuwa na tija sana, ingawa wasanii waliendelea kuwa na upendo na nchi yao, hasa kwa kuona wanaendelea kutunga nyimbo nzuri au filamu za kuelimisha jamii kwa ajili ya kukuza uchimi wan chi yao.

Katika kulisema hilo, nachukua fursa hii kushukuru juhudi za Rais Kikwete, huku nikiamini kuwa mwarobaini wa kilio cha wasanii anao yeye, kama amri jeshi mkuu wa Tanzania.

Yeye ndio kila kitu. Hakuna analoweza kusema yeye na likapingwa, hasa kaatika nchi hii inayojiendesha kwa utawala wa sheria. Hivi karibuni, nilipata kuzungumza na Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Ado Novemba.

November alizungumza mengi, lakini kubwa zaidi alionekana kupokea maneno kutoka kwa Rais Kikwete, kuwa anaendelea na juhudi zake kuhakikisha kuwa utawala wake unakuwa na tunu kwa wasanii.

Maneno yake yamekuja huku akisema kuwa ili aweze kufanikisha suala hilo, atawaagiza Shirika la Posta, kulivalia njuga suala la usambazaji wa kazi za wasanii ili zipatikane nchi nzima.

Kabla Posta kupewa jukumu hilo, kazi za wasanii zilikuwa zinapatikana kwa tab u mno katika mikoa mbalimbali ya Tanzania. Leo hii msanii Ahmad Allly Madee, Profesa Jay, Juma Nature kwa upande wa Bongo Fleva, wanaweza kuwa na mashabiki katika wilaya au mikoa husika, lakini wadau hao wasipate fura ya kununua kazi zao.

Hii ni kwasabu zinapatikana kwa ugumu mno. Kubwa shabiki huyo analoweza kufanya ni kuchoma katika vipanda hasa maeneo ya mijini, kama njia za kumuwezesha kusikiliza nyimbo hizo.

Huu ni wizi wa aina yake. Kwa bahati mbaya, wizi huu unachochewa kwa kiasi kikubwa na mfumo mzima wa Taifa letu. Hakuna msambazaji mkubwa zaidi ya hawa ambao kwa miaka mingi wanalalamikiwa.

Waandaaji wa filamu wanalia kila siku. Kazi zao hazisambai kwa wakati, hivyo kuchochea ugumu wa maisha yao. Huu ndio ukweli wa mambo. Na katika kulijua hilo, naamini kuwa Rais Kikwete kwa utashi wake, mapenzi yake kwa wasanii wa Tanzania, hakika anaweza kulipatia ufumbuzi suala hilo.

Na upendo huo wa JK kwa wasanii wa Tanzania, unaweza kuja kwa sababu kuu mbili. Mosi, JK amesaidiwa sana na wasanii wa Tanzania. Kwa mfano, katika kampenzi za mwaka 2005, yeye akiwa mgombea kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wasanii walifanya kazi kubwa mno.

Wasanii kibao walifanya kazi kwa mapenzi mema na Kikwete. Wanaume Family, akiwa Juma Nature na wenzake walifikia kutunga nyimbo na vibwagizo vya aina yake kwa ajili ya kuonyesha mapenzi kwa JK.

Msanii kama Bushoke, wadau wanakumbuka jinsi alivyougeuza wimbo wake wa Mume Bwege na kutaja jina la JK  na CCM kwa nguvu kubwa mno. Pamoja na hao, bado kulikuwa na mtiririko wa safari na ziara za wasanii kwenye kampeni ambazo baadaye alishinda urais kwa kishindo.

Ukiacha kampeni za mwaka 2005, mwaka 2010 pia wasanii lukuki walifanya kazi za maana kwa ziara za CCM. Wasanii kama vile Diamond, Marlaw na wakali wengine walipishana katika barabara wakitaja jina la JK na CCM kwa nguvu zote, hali iliyochangia mafanikio yake.

Hakika kwa kulisema hilo, basi ndio maana hata JK mwenyewe amekuwa na mapenzi na wasanii wa Tanzania, hivyo katika suala kama hili, lazima alivalie njuga kitu chochote kinachohusu sanaa na wasanii.

Sina nia mbaya ya kumshurutisha Rais Kikwete, ila kauli yangu inakuja kwasababu tayari ameonyesha nia ya dhati ya kutetea maisha ya wasanii wanaoendelea kufa kwa njaa licha ya kuwa na kazi nzuri.

Rais Kikwete anajua kuwa ukiacha kujulikana kwa vijana hawa, bado hawana kitu cha kujivunia katika mitaa yao. Wengi wao bado wanaishi kwa virungu, kuomba msaada kutoka kwa wadau wao.

Ni wachache wanaojimudu kimaisha, huku kujimudu huko kukiwa kwa siku chache, kabla ya kupotea kwa muda mrefu. Wapo wasanii ambao miaka ya 2010 walikuwa wanajiweza kiuchumi, lakini leo hii hawana kitu.

Hiyo imesababishwa na mfumo wetu mbovu. Wasanii kuneemeka kwa siku mbili au tatu, hasa pale anapopata shoo zinazolipwa kwa fedha ndogo kutoka kwa wadau wanaoshiba jasho la wasanii.

Huu ndio ukweli. JK anapaswa kulifanyia kazi suala hili kama mwenyewe alivyoonyesha nia hiyo kwa ajili ya maendeleo ya wasanii wa Tanzania, kama njia za kuwabeba na kuwaweka pazuri.

Ndio, Rais Kikwete ametangaza kuwa, katika kipindi cha utawala wake, atahakikisha kuwa maisha ya w asanii yanakuwa juu katika hali ya kuifanya sekta ya sanaa kuwa juu.

Huu ndio ukweli wa mambo. Nauzungumza kama mdau wa sanaa, ambaye muda mwingi nimekuwa nikiangalia kwa karibu sekta ya sanaa na matatizo yake yanayowakabiri kwa namna moja ama nyingine.

JK yeye ndio mwarobaini wa kelele zinazopigwa na wasanii wetu, hasa hizi za kutokuwa na imani na vyombo vya serikali vinavyohusiana na mambo ya sanaa, kikiwamo kile cha COSOTA, ambacho kwa hakika kila msanii anakilalamikia kwa kushindwa kuweka mipango imara.

Ndio hapo sauti ya rais itakavyokuwa na mgusos, atakapoagiza lazima stika za kuwekwa kwenye kazi ziwekewe utaratibu mzuri, zisifanane, kila mmoja iwe na nembo yake kwa ajili ya kuepusha wizi na migogoro.

Pamoja na mambo mengine, lakaini serikali ikifanyia kazi na kulipatia ufumbuzi suala hili, hakika hata mapato ya wasanii yataongezeka pamoja na kutoa fursa ya kodi kuingia serikalini kwa utaratibu maalum.

Hakika, katika hili, napongeza na kutambua juhudi za Rais Kikwete, huku nikiamini kuwa anaweza kufanya palipokuwa na giza kukawa na mwanga, hasa katika suala zima lisilomuhusisha Mwenyezimungu.
0712 053949
0753 806087

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...