https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, March 21, 2013

Naidjala na Sekotswe watoka sare pambano la masumbwi la kukata na shoka


MPAMBANO uliokuwa unangojewa kwa hamu na watu wengi wa kumpata Mfalme wa uzito wa bantam wa kimataifa kati ya mabondia Immenuel Naidjala a.k.a Prince kutoka Namibia na Lesley Sekotswe kutoka Botswana haukuweza kutoa mshindi baada ya matokeo ya majaji wawili kumpa kila mmoja ushindi wan a jaji wa tatu kutoa droo.

Pambano hili lilikuwa limeandaliwa na kampuni ya Sunshine Promotions ya bwana Nestor Tobias na lilikuwa na kila aina ya hamasa baada ya mabondia wote wawili kuonyesha ufundi wa kurusha makonde. 
 

Rais wa IBF kutoka Afrika, Ghuba ya Uajemi na mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi ambeye alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa mpambani huu alitangaza kuwa mabondia wote wawili watakutana tena baada ya kipindi cha mapumziko ya mwezi mmoja ili kuweza kumpata mshindi wa mkanda huo ambaoni watatu kwa umaarufu katika mukanda ya ngumi. 

Mkanda wa kwanza kwa umaarufu ni wa ubingwa wa dunia. Mkanda wa tatu ni wa ubingwa wa mabara na mkanda wa tatu ni wa ubingwa wa kimataifa ambao ndio uliokuwa unagombewa na mabanodia hao. 

Wakazi wengi wa jiji la Widhoek na miji mingine ya jirani pamoja nan chi za jirani walijazana katika hotel ya Widhoek Country Club and Casino kuushughudia mpambani huo ambao ulikuwa na kila aina ya hamasa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...