https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, March 29, 2013

Kuanguka kwa ghorofa Kariakoo, Kamanda Kova apiga mkwara mzito


 Jengo lililo pembeni mwa msikiti wa Shia Ithnaasheri mtaa wa Indira Ghandi katikati ya jiji la Dar es salaam linavyoonekana baada ya kuporomoka asubuhi hii. 

Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es salaam Suleiman Kova kawaambia wanahabari kuwa kila aliyehusika na ujenzi, usimamizi na hata utoaji vibali atawajibishwa endapo kutaonekana kumekuwepo uzembe upande wake hadi kusababisha kadhia hiyo.

Inasemekana kuwa, jengo hilo linakisiwa kuua watu wawili na juhudi za kuwaokoa watu waliokuwa kwenye kifusi hicho zinaendelea.
 Watu wakifuatilia kwa karibu hali ya mambo inavyoendelea mara baada ya jengo hilo kuanguka leo asubuhi na kuzua taharuki kubwa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...