https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, May 06, 2013

Mama Asha Bilal aadhimisha sherehe za miaka 10 ya taasisi ya Maznat

 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana jioni kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, kama Mgeni rasmi sambamba ya kuzindua Shule ya Taasisi hiyo inayofundisha masuala ya urembo.
 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akishiriki kukata Keki na Maza Sinare, ambaye ni mmiliki wa Saluni ya Maznat, ikiwa ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana Mei 5, 2013, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo. 
 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
 Mama Asha, akipongezwa na wageni waalikwa baada ya kusoma hotuba yake ukumbini hapo.
 Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria sherehe hizo.
 Mmiliki wa Saluni na Taasisi ya Maznat, Maza Sinare, akiwalisha keki baadhi ya wageni waalikwa wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam jana, sambamba na sherehe hizo pia Mgeni rasmi mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal (kulia) akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi shule ya masuala ya Urembo, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana. Shule hiyo inasimamiwa na Taasisi hiyo.luni na Taasisi hiyo ya Maznat, Maza Sinare. 

 Kwa amani na furaha ya kutimiza miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, wageni waalikwa waligonganisha glasi zao.
miaka kumi ya kampuni ya Maznat Bridal Care. Picha zote kwa hisani ya Lukaza Blog...

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...