https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, May 26, 2013

Yanga yatamba Simba itaishia kunawa msimu huu wa usajili


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UONGOZI wa klabu ya Yanga, umetamba kuwa watani zao wa jadi Simba, wataishia kunawa kama wana ndoto au lengo la kuchukua mchezaji wao yoyote wanayemuhitaji abaki kwenye kikosi chao.
                    Baraka Kizuguto, Msemaji wa Yanga
Yanga na Simba wapo kwenye vita ya kuwasainisha nyota wao, huku Yanga wakifanikiwa kupata saini ya Mrisho Ngassa kutoka Simba, hiku juzi Haruna Niyonzima naye akitia saini ya kubaki jangwani kwa misimu mwili zaidi.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, alisema kuwa hakuna nyota wanayemtaka akasajiliwa na Simba, hivyo benchi la ufundi na usajili linafanya kazi muda wote.

Alisema anaamini kila mchezaji imara na hodari mwenye uwezo atabaki Yanga pamoja na kuongeza wengine kulingana na mahitaji ya benchi lao la ufundi, linaloongozwa na Ernest Brandit.

“Tunasikia mengi kutoka kwa watani wetu, ila juu ya kupata saini za mchezaji wetu kutoka Yanga, labda awe ahitajiki kulingana na mtazamo wa benchi la ufundi, maana hawatapata hiyo nafasi.

“Tumeshafanikiwa kuipataa saini ya Niyonzima, kinachofuata sasa ni kuwaangalia wengine, akiwamo Hamis Kiiza, Nurdin Bakari, ambao nao mikataba yao imekwisha na Yanga inawahitaji,” alisema Kizuguto.

Yanga inaingia kwenye vita vya usajili huku ikijivunia kunyakua ubingwa wa Ligi ya Tanzania Bara, sambamba na kumtandika mtani wake wa jadi, Simba kwa mabao 2-0 na kuwafurahisha mashabiki wao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...