https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, May 16, 2013

Kuelekea mechi ya Simba na Yanga Jumamosi, vituo 9 Dar es Salaam kuuza tiketi za mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka Tanzania

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
TIKETI kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Yanga litakalochezwa keshokutwa (Jumamosi) kwenye Uwanja wa Taifa zitaanza kuuzwa kesho (Ijumaa) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
 
            Boniface Wambura, Msemaji wa TFF
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Boniface Wambura, vituo vitakavyouza tiketi hizo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live Mbagala na Sokoni Kariakoo.

Tiketi hizo zitakuwa zikiuzwa katika magari maalumu yaliyoegeshwa katika vituo hivyo. Viingilio katika mechi hiyo ya kufunga msimu ni sh. 5,000 kwa viti vya kijani, sh. 7,000 viti vya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 VIP B n ash. 30,000 kwa VIP A.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...