https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 17, 2013

Timu ya waandishi wa Habari za Michezo, Taswa FC, chapewa vifaa vya michezo na kinyaji cha Chilly Willy

IMG_0368
Meneja Masoko wa kinywaji cha Chilly Willy kinacho sambazwa na kampuni ya TSN Group, Yohana Manoli  (Kushoto) akimkabidhi jezi mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary (wa kwanza kulia) katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika kwenye mgahawa wa Hadees. Kulia ni Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowah.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Kinywaji maarufu cha kuongeza nguvu, Chilly Willy Energy Drink kimetoa msaada wa jezi  na mipira kwa timu ya soka ya waandishi wa habari za michezo nchini, Taswa FC na timu ya Netiboli, Taswa Queens kwa ajili ya kutumika michezo yake mbali mbali.

Meneja Masoko wa Kampuni ya TSN Group kinachosambaza kinywaji cha Chilly Willy Yohana Manoli alikabidhi vifaa hivyo kwa mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary katika hafla fupi iliyopfanyika kwenye mgahawa wa Hadees uliopo katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Manoli alisema kuwa sababu kubwa ya kukabidhi vifaa hivyo kwa Taswa SC ni kutambua mchango wa waandishi wa habari katika kuendeleza michezo nchini na hasa ukizingatia kuwa kinywaji cha Chilly Willy hakina kilevi na ni maalum kwa wanamichezo.

Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa  TSN Group, Meshack Nzowah alisema kuwa kinywaji chao cha Chilly Willy kina ubora wa kimataifa na wanaamini kuwa wanamichezo na wanajamii wataanza kutumia kinywaji hicho katika shughuli mbalimbali.

“Chilly Willy ni kinywaji ambacho hakina kilevi, kina ubora wa kimataifa na kutokana na hilo, kampuni ya TSN Group ikaamua kukisambaza nchini kwa lengo la kutoa bidhaa iliyobora zaidi, tunaamini wanamichezo wataanza kutumia hiki na vile vile ni maalum kwa waandishi wa habari na wadau wengine nchini,” alisema Nzowah.

Mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary aliipongeza kampuni inayosambaza kinywaji cha Chilly Willy na kuwaomba waandishi wa habari kuanza kutumia kinywaji hicho. Majuto alisema kuwa Chilly Willy imetambua mchango wa Taswa  SC katika kuendeleza michezo na kutoa msaada huo.

“Ni faraja kubwa kuwa na kinywaji hiki hapa nchini na hasa kwa kutujali wana habari, kwa vifaa hivi, Taswa FC na Taswa Queens zitakuwa na nguvu na ubora kama wa Chilly Willy,” alisema Majuto.

Majuto alisema kuwa jezi hizo watazizindua rasmi Jumapili katika mechi dhidi ya timu ya kombaini ya mabondia wa ngumi za kulipwa nchini itakayochezwa kwenye uwanja wa Leaders Club kuanzania saa 5.00 asubuhi.

Alisema kuwa timu ya mabondia itaongozwa na bondia mkongwe nchini, Rashid “Snake Man” Matumla na mabondia wakali wengine kama Francis “SMG” Cheka, Cosmass  Cheka, Mbwana Matumla, Karama Nyilawila, Maliki Kinyogoli, Hassan Matumla, Daudi Mhunzi, Saidi Yazidu, Francis Miyeyusho , Thomas Mashali, Charles Mashali na wengine wengi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...