https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, January 03, 2013

Mtanga asema Mungu anawapa kadi nyekundu

Dada huyu akishuka kwenye gari huku analia
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MSANII wa Vichekesho hapa nchini, Hamis Changale, maarufu kama Mtanga, ameshangazwa na kadi nyekundu zinazoendelea kwa wasanii na kusababisha vifo vyao, hali inayoogopesha.
Wadau na wasanii wakijadili jambo kwenye msiba wa Sajuki

Mtanga aliyasema hayo mapema leo, akisema kadi hizo nyekundu zinatolewa kwa wasanii nyota, akiwamo Steven Kanumba, Sharomillionea, Mropelo, John Maganga na sasa ameondoka Juma Kilowoko, maarufu kama Sajuki.

Thea akijadili jambo msibani kwa Sajuki
Mtanga alisema vifo hivyo ni kama kadi nyekundu kwa wasanii Tanzania, jambo linalomnyima raha kwa kusikia au kuona nyota wanaendelea kupukutika kila siku kwa sababu za kushangaza.

 Hali inavyoendelea msiba wa Sajuki Tabata Bima

“Alipokufa Kanumba, watu wengi tuliogopa kutokana na kifo chake, lakini bado ikaja tena kwa wasanii zaidi ya watano, akiwamo Sharomillionea aliyekufa mwishoni mwa mwaka jana na kuzikwa kwao Lusanga.
Msanii wa vichekesho, Mtanga

“Na leo tena mwenzetu Sajuki anafungua pazia la vifom kwa wasanii wa Tanzxasnia kwa mwaka huu kuonyesha kuwa bado Mungu anaendelea kutoa kadi nyekundu kwa wasanii kila siku ya Mungu,” alisema Mtanga.
Sajuki enzi za uhai, wakati ni mgonjwa akiwa na mke wake, Wastara

Kwa mujibu wa Mtanga, kadi nyekundu katika mchezo wa soka ni tukio linalotokea kati ya mchezaji uwanjani na mwamuzi kwa ajili ya kumtoa nje ya uwanja mchezaji aliyefanya kitendo ambacho si cha kiungwana.

Taarifa za kifo cha Sajuki kimeendelea kuwagusa Watanzania na viongozi wa Serikali, baada ya Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba kuwa miongoni mwa waombolezaji waliofika msibani Tabata Bima kwa ajili ya kuungana katika msiba wa Sajuki.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, aliwata Watanzania kutumia fursa ya kifo kwa ajili ya kumuombea marehemu pamoja na kuwataka wasanii wawe kitu kimoja.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...