https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, January 01, 2013

Matokeo ya sensa yamshangaza Rais Kikwete

Rais Jakaya Mrisho Kikwete

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WATANZANIA wamefikia idadi ya 44,929,002 mwaka 2012 kutoka watu 34,443,603 katika sensa ya watu na makazi iliyotangazwa jana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

Idadi hiyo ni kubwa na kumuogopesha Rais Kikwete na kutangaza watu watumie uzazi wa mpango, ikiwa ni kutokana na kugundulika kuwa jumla ya idadi ya watu wote nchini sasa, ni milioni 44,929,002, ikiwa ni ongezeko la watu milioni 10 tangu ilipofanyika Sensa ya mwaka 2002.

Kwa mujibu wa matokeo hayo, upande wa Tanzania Bara kuna Watanzania milioni 43,625,434, wakati Zanzibar  kuna watu milioni 1,303,568.

Akizungumza baada ya kufanya uzinduzi huo, Rais Kikwete jana aliwataka Watanzania wahakikishe kwamba wote wanafuata uzazi wa mpango, akisema kuwa ongezeko hilo ni kubwa na serikali itashindwa kuwahudumia kama inavyotakiwa.

“Sensa ya mwaka 2002 ilionyesha kuwa Watanzania tupo milioni 34, lakini hii ya mwaka huu tumefikia milioni 44 na kuonyesha kuwa ni ongezeko kubwa sana.

“Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Watanzania tutafikia watu milioni 51, ikiwa ni kwasababu ya watu kuzaliana na ndio maana kuna haja ya kupanga uzazi,” alisema Kikwete.

Wakati Taifa linapata Uhuru, inakadiriwa kuwa mwaka 1967, Watanzania Bara walikuwa milioni 12.3 wakati Tanzania Visiwani walikuwa 300,000 ambapo sasa wapo milioni 1,303,568.

 

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...