https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, January 01, 2013

Lowassa asifia sera ya vikoba Tanzania




Waziri Mkuu wa zamani na mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa, akitoa hotuba kwa wananchi wa kijiji cha Mswakini, Wilayani Monduli, wakati wa uzinduzi wa Vikoba kijijini hapo.
Wakati Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, ambaye pia ni mbunge wa Monduli mambo yalionekana hivi, akiwa anaingia sambamba na mke wake, Regina Lowassa, katika uzinduzi wa Vikoba katika kijiji cha Mswaki mapema leo.
Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Monduli, aliyejulikana kwa jina laa Judith, akikabidhi hati kwa Edward Lowassa, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Vikoba katika kijiji cha Mswakini


Na Mwandishi Wetu, Monduli
WAZIRI Mkuu wa zamani, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, amesema kuwa ushirika wa Vikoba ni sawa na mshipa wa damu kwa sera ya maisha bora kwa kila Mtanzania.

Lowassa ameyasema hayo leo katika uzinduzi wa Vikoba vya Mswakini, wilayani Monduli, ikiwa ni ishara ya kutambua njia ya kumkomboa Mtanzania.

Akizungumza na wanakikundi hicho, Lowassa alisema kwamba hiyo ni sera aliyoingia nayo madarakani Rais Jakaya Kikwete.

Alisema kuna haja ya kuwa na vikoba nchi nzima kwa ajili ya kuongeza kasi ya maisha bora kwa kila Mtanzania, ukizingatia ni mfumo mzuri kiutendaji wa biashara kwa wote waliokuwa kwenye vikundi hivyo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...