https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, January 26, 2013

Msafara wa Kinana wapokelewa kwa mbwembwe Dodoma

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi (katikati) akiongoza mapokezi ya ujumbe wa Sekretarieti ya CCM,unaoelekea mkoani Kigoma mapema asubuhi hii kwa usafiri wa treni,ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (wa pili kulia) kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM yatakayo adhmishwa mkoani humo.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwa ndani ya treni asubuhi hii akiwapungia mkono WanaCCM wa Mkoani Dodoma waliofika kuwalaki na kuwatakia safari njema Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana akishuka katika treni Mjini Dodoma
Akisalimiana na Baadhi ya Wana CCM akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),  Abdulrahman Kinana akizungumza na Wanachama wa CCM mkoani Dodoma waliokuwa wamefika Stesheni ya Dodoma asubuhi hii kuwalaki Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM. Wajumbe waliondoka jana ni Katibu wa NEC, Siasa na Mahusiano ya Kimataifa, Dkt. Asha-Rose Migiro na kulia kwake ni Katibu wa NEC,Itikaji na Uenezi CCM Nape Nnauye.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiagana na baadhi ya WanaCCM wa Mkoani Dodoma waliofika kuwalaki na kuwatakia safari njema Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM, wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM,Wajumbe wa Sekretarieti ya NEC wameondoka jana jijini Dar kwenda Mkoani Kigoma kuadhimisha miaka 36 ya Chama hicho.
kk1Abdulrahman Kinana katibu Mkuu wa CCM makiwasili mjini Dodoma na wajumbe wa Sekretarieti ya ya CCM waka ti wakielekea mkoani Dodoma kwa Treni kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 36 ya CCM Mkoani Kigoma yatakayofanyika Februari 5 mwaka huu, kushoto ni Katibu wa Halmashauri Itikadi na Uenezi
kk3

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...