https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, January 09, 2013

Meneja Twanga Pepeta amuumbua Dogo Rama



Dogo Rama katika pozi

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MWANAMUZIKI wa bendi ya The African Stars, Dogo Rama, jioni ya jana aliumbuka makao makuu ya bendi yao, baada ya kushindwa kuiona printer iliyokuwa juu ya meza.

Meneja wa Twanga Pepeta, Hassan Rehani

Hatua hiyo, alisababisha kicheko kutoka kwa meneja wake, Hassan Rehani, aliyeanza kumshangaa Dogo Rama.
 
Hata hivyo, kitendo cha kuchekwa katika ofisi hiyo, kilimuumiza na kuanza kuhoji sababu ya kicheko cha bosi wake, ambaye pia hakuwa peke yake ofisini kwake.

Dogo Rama alijitetea, “sio kweli kwamba siijui mashine ya (Printer) kama ulivyoniagiza, ila sijaiona haraka karatasi uliyoniambia nikupe, sasa nashangaa mnacheka.

“Labda mcheke kwa mengine lakini sio hili la printer maana itakuwa ajabu kama sitaijua kitu kama hicho ambacho kila mtu anakijua,” alisema Dogo Rama.

Hata hivyo, kushindwa kujua kitu sio jambo baya kwa mtu yoyote katika Dunia ya leo inayotoa vifaa mbalimbali. Dogo Rama ni miongoni mwa vijana imara wanaoipaisha bendi ya Twanga Pepeta, akijulikana pia kwa jina la Kilomita 10,000.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...