https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, January 19, 2013

Serikali yapunguza tatizo la njaa wilayani Handeni


Mkuu wa Wilaya Handeni, Muhingo Rweyemamu

Na Rahimu Kambi, Handeni
SERIKALI imeleta tani 150 za mahindi ambazo zimeanza kusagwa kwa ajili ya kuwauzia wananchi kwa bei nafuu isiyozidi Sh 900 kwa kilo moja, kitendo kitakachoweza kupunguza tatizo la njaa wilayani hapa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, alipozungumza na Handeni Kwetu juu ya kupambana na njaa wilayani kwake.

Akizungumza zaidi, Muhingo alisema kwamba chakula hicho kitauzwa zaidi kwa kata na vijiji vilivyoathiriwa sana na tatizo la njaa wilayani humo.

Alisema kwa kufikishiwa chakula hicho, wananchi wake watapata unafuu wa kiasi fulani, hasa kwa kununua kwa bei nafuu tifautisha na bei ya sasa.

"Chakula kimeshafika na sasa kimeanza kusagwa ili unga uuzwe kwa bei nafuu kwa ajili ya kuwapa unafuu wananchi katika baadhi ya kata zilizoathiriwa zaidi na tatizo la njaa.

"Naamini sehemu kama vile Sindeni, Kwamsisi, Kwedikabu, Kwasunga na kwingineko kulikokumbwa na tatizo hilo chakula hicho kitafika, ikiwa ni mipango mizuri ya serikali juu ya kukabiriana na tatizo la njaa," alisema Rweyemamu.

Wilaya ya Handeni ni miongoni mwa maeneo yanayotajwa kuwa na njaa inayosababisha baadhi ya wananchi wake kukosa chakula, hivyo kuhangaika hasa kwa kula mboga mboga na matunda mengine, yakiwamo maembe.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...