https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, September 21, 2013

Waziri Muhongo azindua hafla ya udhibiti wa vihatarishi katika usimamizi wa fedha

Mkurugenzi Mtendaji wa Banki ya Barclay's Tanzania Kihara Maina akitoa hotuba ya kumkaribisha  Mgeni Rasmi Waziri wa Wizara ya Fedha na Uchumi  Dkt. William Mgimwa katika hafla ya uzinduzi wa udhibiti wa vihatarishi katika  usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions).Uzinduzi huo uliyofanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi Waziri wa Wizara ya Fedha na Uchumi Dkt. William Mgimwa akiongea na viongozi, wawezeshaji na wateja wa  Benki ya Barclays Tanzania  wakati wa  hafla ya uzinduzi wa udhibiti wa vihatarishi katika  usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions)  iliyofanyika leo kwenye  hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam
Mjumbe wa bodi ya benki ya Barclays Tanzania Fatma Karume (kulia) akisisitiza na kufurahia jambo alipokuwa anaongea na Mgeni Rasmi (hayupo kwenye picha) wakati wa hafla ya uzinduzi wa udhibiti wa vihatarishi katika usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions) iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mjumbe wa bodi ya benki hiyo Suleiman Mohamed.
Baadhi ya washiriki wa semina ya udhibiti wa vihatarishi katika usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions) wa Benki ya Barclays wakihudhuria  hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye  hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Eleuteri Mangi-Maelezo)

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...