https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, September 01, 2013

Pitia maoni ya Rasimu ya Katiba ya Chama cha siasa NRA

MAONI YA NRA NI KAMA IFUATAVYO;
SURA YA KWANZA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
1(1)Tunakubaliana na SERIKALI TATU .

 
Naibu Katibu Mkuu wa NRA
SASABU:Imekuwa ni kilio cha muda mrefu cha washiriki wa Muungano huu kila mmoja juu ya serikalai yake yenye mamlaka kwa watu wake na hata ukizingatia nchi hizi zilikuwa na historia zake, na kila moja ilikuwa chini ya utawala mwingine wa kikoloni, zilipata Uhuru wao kwa njia tofauti na tarehe tofauti, hivyo ili kuufanya Muungano wenye nguvu na uhalali ni kuwa na serikali hizi tatu zitakazokuwa na mabunge matatu.

NA Ili kuleta maana sahihi ya matumizi wa Maneno, Katika Rasimu hii ya Katiba,Kila panaposomeka ‘TANZANIA BARA’ ,badala yake isomeke ‘JAMHURI YA WATU WA TANGANYIKA’, na Kila panaposomeka ‘TANZANIA ZANZIBAR ’ badala yake isomeka ‘JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR’
Sababu 1:Majina haya mawili ndio yatakayotoa jina la Tanzania, na hivyo kuwa na ‘JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA’
 
Sababu 2:Kuleta maana halisi ya muungano huu ni kuwa kuna wananchi wa pande mbili walioungana na kupata Neno ’JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA’ hivyo maneno ‘WATU WA’ katika upande wa Tanganyika na Zanzibar linawawakilisha wananchi moja kwa moja , kwa kuwa , wao ndio walengwa katika Muungano huu.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha NRA
Pia tunapendekeza ‘KUONGEZWA ANNEX PAGE’ mwisho wa Katiba hii, iweke wazi eneo litakalotiwa saini na viongozi wa nchi hizi mbili.
Sababu:Suala la hati ya Muungano limekuwa ni tatizo,watanzania kwa vipindi tofauti wamekuwa wakihoji suala la makubaliano ya muungano,hivyo kurasa hii ya nyongeza ikionyeshe Nani anawakilisha upande mmoja ,lini wanasaini,na kama kuna makubaliano yoyote yaanishwe katika kurasa hii ili kujenga imani kwa wananchi wa nchi hizi mbili.
KIFUNGU 1(2).Kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni shirikisho la Kidemokrasia na limeridhia ‘MFUMO WA VYAMA VINGI VYA SIASA’ Serikali ya Jamhuri itamke wazi kuwa ‘VYAMA VYA SIASA VITAPATIWA RUZUKU YA KUENDESHEA SHUGHULI ZAO’ kwa ‘USAWA’ huku ikitamka kuwa sheria nyingine itawezesha vyama hivyo kupata ruzuku kutokana na idadi ya Uwakilishi wao katika mabunge yao na Halmashauri.

Sababu 1:Kazi ya Vyama vya Siasa ni kazi inayolenga jamii ndani ya nchi husika,hivyo kuviacha vyama kujitafutia Pesa za kuendesha shughuli zao za msingi bila msaada wa serikali ni ‘HATARI KWA TAIFA’ .Hofu ni kuwa, vyama hivi siku moja kutokana hali ngumu ya kujiendesha vitatafuta wafadhili mamluki wasio na nia njema na nchi yetu ,hivyo ili kusaidia kazi za vyama,kudumisha Uzalendo na kuikuza Demokrasia .Serikali ya Jamhuri isimamie kuhakikisha Vyama vilivyosajiliwa vinapata ‘FLAT RATE GRANT’ malipo yaliyo sawa ya kuendesha shughuli zao.
 
Sababu 2:Ili kuepuka kupata chama kilichopewa pesa za nje kubadili utawala wananchi hii kwa hoja kuwa kilipata pesa kinapojua chenyewe kwa makubaliano ya kurejesha Ufalme,Usultani, wauzaji wa madawa ya kulevya au hata Ukoloni nchini.
 
KIFUNGU CHA 2:ENEO NA MIPAKA YA NCHI WASHIRIKI WA MUUNGANO
 
Kifungu hiki kionyeshe kwa vipimo ukubwa na umbali wa mipaka yetu baina ya Tanganyika na Zanzabar,Yaani
Ni kilometa/maili ngapi kutoka nchi moja na nyingine pande za,
a. Kaskazini
b. Kusini
c. Mashariki na
d. Magharibi
Hii imewekwa katika Katiba ya nchi mojawapo shiriki vipimo vya mipaka yake kwa uwazi.
 
Sababu: Isije siku moja nchi moja ikakosa uhuru wa kutumia eneo Fulani la bahari kwa shughuli zake za kimaendeleo kwa kuwa eneo hili halikuwekwa wazi kuwa lipo upande gani wa nchi hizi mbili.
 
KIFUNGU CHA 3:SIKUKUU ZA KITAIFA.
 
Sikukuu za kitaifa za kiserikali kuwa moja tu kwa Jamhuri ya Muungano, yaani Tarehe ya Muungano 26/April kila mwaka , na kuanisha sikukuu nyingine mbili kubwa za kidini ili kuwa za kitaifa,Nazo ziwe ,
 
1. Iddi fitri(Baada ya Mfungo kulingana na mwandamo wa Mwezi kwa Waislam)
 
2. Krismas (Kila tar.25/Dec kila mwaka kwa Wakristo)
Sikukuu ya Uhuru wa Tanganyika iwe ni kwa Tanganyika tu, na sikukuu ya Uhuru wa Zanzibar iwe ni kwa Zanzibar tu.
 
Sababu:Wananchi kuendelea na kazi za ujenzi wa Taifa lao kwa kipindi hicho na kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali.
 
KIFUNGU CHA 4:LUGHA YA TAIFA
 
Kifungu kidogo cha (2) ,kutamka wazi kuwa iwapo Kiingereza kitatumika sharti pawepo na ‘MKALIMANI WA KUTAFASIRI’
Sababu: Watanzania wengi inajulikana kuwa hawajui lugha hii ya kigeni,na hata wale wanayoijua basi hawaijui kwa ufasaha lugha hii,malalamiko mengi yamekuwa nchi nzima kuwa watu wanakosa kujua haki zao,kuelewa mambo muhimu yanayowahusu hata kushindwa kufuatilia mambo muhimu yanayowahusu ikiwa ni pamoja na kukosa haki katika mahakamani kwa kutojua tu Lugha ya Kiingereza.
 
Kwa kuwa Kiswahili ni moja ya Tunu katika Tunu za Taifa,hivyo Lugha hii itumike katika shughuli zote za serikali kwa sharti hili.Hata mashuleni lugha hii itumike kwa kufundishia na mawasiliano,lugha nyingine ziwe ni ziada kwa anayetaka.

KIFUNGU CHA 5:TUNU ZA TAIFA.
Kiongezwe kifungu kidogo cha 5(h) ‘AMANI’
Sababu:tunaamini kuwa yote yaliyobebwa na kifungu hiki ni zao la Amani,pasipo amani yote haya hayawezi kutekelezeka, hivyo kuifanya Amani ya nchi yetu kuwa tunu itasaidia Watanzania kuona kuwa suala hili ni muhimu sana na litakuwa wazi kwa watu wote.

SURA YA NNE
HAKI ZA BINADAMU
Kiongezwe kifungu cha ;
48.HAKI ZA WAKULIMA NA WAFUGAJI
49.HAKI ZA WAFANYABIASHARA
50.HAKI ZA WANAUME
 
Sababu 1:Makundi haya ni muhimu katika jamii yetu ,Mfano,Wakulima na wafugaji ni asilimia zaidi ya 80% ya Watanzania wote (Kutokana na Takwimu za nchi), ni miongoni mwa makundi yanayopiga kelele kuwa hayapatiwa haki za kutosha.
 
Sababu 2:Pia suala la wafanyabiashara ni suala mtambuka kwa Taifa letu,biashara imekuwa ni sekta inayokuwa kwa kasi na inayotoa ajira na utajiri kwa watanzania,hivyo haki zao wafanyabiashara ni muhimu kutamkwa katika Katiba
 
Sababu 3:Tunapotaja haki za wanawake ni muhimu na haki za wanaume zikatajwa ili kutenda haki kwa jinsia zote na kuondokana na ubaguzi wa kijinsia.
 
SURA YA SABA,SEHEMU YA KWANZA
SERIKALI,RAIS NA MAKAMU WA RAIS
 
( C ).UCHAGUZI WA RAIS
KIFUNGU:75, SIFA ZA RAIS
Kifungu kidogo cha 75(f).kifungu hiki kiondolewe kwani kitawanyika watu haki ,kwani haki za kibinadamu zinatamka kuwa ‘kila mtu anayo haki ya kuchagua na kuchaguliwa’(Universal Declaration Of Human Right,Article 21). hivyo sifa hii inaweza kuwanyima watu wenye uwezo mzuri na busara kuwa Rais.

( D ).MASHARTI MAHUSUSI KUHUSU RAIS
KIFUNGU CHA 83.KINGA DHIDI YA RAIS
Kifungu kidogo cha (2) na (3). Kuhusu mashitaka kwa Rais,tunapendekeza ‘RAIS ASHITAKIWE MARA BAADA YA KUMALIZA MUDA WAKE WA UONGOZI’
 
Sababu 1: Suala la Rais kutokushitakiwa baada ya kuacha madaraka,kutaliingiza Taifa katika majanga makubwa ya Ufisadi,Ulimbikizaji wa mali na utendaji mbovu,usiofuata sheria na haki za kibinadamu , kwa kuwa Rais atakayekuwa na kinga kama hiyo anaweza kuufanya utawala wake kuwa wa dhuluma,unyanyasaji,ukatili na hata usioheshimu watu, akijua kuwa baada ya kumaliza awamu yake hatoshitakiwa.
 
Sababu 2:Raisi asishitakiwe akiwa madarakani ili kuepuka watu wanaoweza kuitumia vibaya nafasi hiyo kwa kumpeleka Rais mahakamani kila kukicha kwa sababu zisizotosha na kumfanya Rais kutokuwa na muda wa kutosha wa kutekeleza majukumu ya Urais kwa wananchi.
SEHEMU YA PILI
 
BARAZA LA MAWAZIRI WA MUUNGANO.
( a ).BARAZA LA MAWAZIRI
 
Tunashauri, ‘Baraza hili la Mawaziri linatakiwa kuwa na idadi sawa ya mawaziri ili kuweka usawa wa kimuungano,na iwapo Waziri atatoka upande mmoja ,Naibu wake atoke upande wa pili wa nchi shiriki wa Muungano’.
KIFUNGU CHA 92(4).
BUNGE na MAHAKAMA , vipewe haki,uwezo na mamlaka kisheria kuchunguza kama ushauri wowote au ushauri wa aina gani ulitolewa na Baraza la Mawaziri kwa Rais.
 
Sababu: Hali hii itaongeza umakini wa Baraza letu la Mawaziri juu ya kumshauri Rais,hofu ni kuwa Baraza hili linaweza kumshauri Rais masuala yasiyo na faida kwa Taiafa hili ama kutoa ushauri utakaoigharimu nchi nakuiletea hasara nchi.Mfano Masuala mengi sana ya Taifa hili yamelalamikiwa juu ya ushauri uliokuwa ukitolewa na Baraza la Mawaziri na kupelekea baadhi ya Mawaziri kujiuzulu huku nchi ikikabiliwa na kesi na madeni yaliyosababishwa na ushauri wa Baraza la Mawaziri,na kama angalizo isije siku moja Taifa hili likaingia katika Vita isiyo na faida na Taifa kutokana na ushauri wa Baraza la Mawaziri.
 
Hivyo mahakama na Bunge vikiwa na haki ya kuhoji na kuchunguza kisheria ushauri wa Baraza la Mawaziri kwa Rais utasaidia kuliondoa Taifa katika misuguano ya ndani kwa ndani.

SURA YA TISA
BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO
SEHEMU YA KWANZA
KUUNDWA KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO.
KIFUNGU CHA 105(1) kuongezwa maneno haya mbele ya sentensi ‘LENYE IDADI SAWA YA WABUNGE KUTOKA PANDE ZOTE ZA MUUNGANO’
105.(2) Wabunge wa Bunge la Jamhuri wasitoknane na majimbo ya uchaguzi,watokane na ‘uchaguzi huru utakaofanywa ndani ya Mabunge ya nchi shiriki’ ili kuleta usawa wa idadi yao katika Bunge la Jamhuri.
 
USHAURI WA JINSI YA KUWAPATA WABUNGE LA JAMHURI
1. Wanaopenda kuwa wabunge wataomba kupitia mabunge ya nchi shiriki,hapo watachaguliwa na kupigiwa kura ,kisha wataletwa katika Bunge la Jamhuri,
2. Hata katika umoja wa Nchi za Afrika mashariki suala la wawakilishi limekuwa likifanyika hivyo na kupeleka idadi sawa ya wawakilisha toka nchi zote washiriki bila kujali idadi ama ukubwa wa eneo la nchi mshiriki.
SABABU:Suala la kutumia majimbo kama eneo la kupata wabunge litatoa idadi tofauti kutokana na ukubwa na idadi ya majimbo ya nchi shiriki,na kufanya sehemu moja nchi shiriki kuwa na idadi kubwa ya uwakilishi zaidi ya upande mwingine .

SEHEMU YA PILI
WABUNGE.
 
(a) Uchaguzi wa Wabunge
117.Sifa za kuwa mbunge.
Kifungu cha 117(5)kifungu kidogo (m) kiondolewa kwa kuwa kitawanyima haki watu haki ambayo inatolewa na Haki ya Kimataifa ya kibinadamu ya kuchagua na kuchaguliwa (Universal Declaration Of Human Right,Article 21).Isipokuwa itamkwe wazi katika Katiba kuwa ,kutatungwa sheria nyingine itakayoelekeza jinsi gani watagombea.
Kigungu cha 118.Kigungu hiki kizima kiondolewe, nacho kinapinga na haki za kibinadamu za Kimataifa.(Universal Declaration of Human Right,Article 21).

118(4).(b).Kifungu hiki kisitaje kuwa sifa ya kuwa M/kiti au makamu wa TUME basi lazima awe Jaji,bali sifa iwe ni ‘Mtu muadilifu, muwajibikaji na mwenye Elimu ya Kutosha. Idadi ya wajumbe wote wa Tume izingatie Muungano na Jinsia.
 
Sababu:Kitendo cha kuweka sifa ya M/kiti na Makmu mwenyekiti lazima awe Jaji itawanyima nafasi watu wenye uwezo na wenye fani nyingine kwa kuwa suala la uchaguzi ni suala la maamuzi,uangalizi na utoaji wa matokeo kwa uwazi , hivyo sio lazima Jaji tu ndio mwenye uwezo wa kufanya hayo,hata mtu mwingine mwenye ujuzi,utaalamu na elimu nyingine anaweza kuyamudu majukumu ya Tume,Pia sifa hii itawahusu viongozi walewale waliokuwa katika mifumo ya serikali zilizopita,waliofanya kazi na kustaafu kwa mujibu wa sheria,hivyo kuwarejesha kazini watu hawa kwa mlango wa Ujaji utaleta matatizo katika utendaji wa kazi za Tume kwa kuwa watu hawa tayari walikuwa katika mtandao wa serikali iliyokuwa Madarakani ,hivyo ni rahisi sana kuendelea kulipa fadhila na kuathiri utendaji wa Tume unaopaswa kuwa huru.
 
Pia sifa hii itawanyima kazi vijana walio na uwezo na utashi wa kufanya kazi .(Lakini si vibaya miongoni mwa wajumbe wakawemo Majaji ili kuzidi kupata fikra na busara zao)

SURA YA KUMI NA MBILI
SEHEMU YA PILI.
TUME HURU YA UCHAGUZI.
181.KUUNDWA KWA TUME.
181(3).Tunashauri kuwa M/kiti na Makamu M/kiti wa Tume Huru,washike madaraka mara baada ya kuthibitishwa na Kamati Maalumu ya Vyama vya Siasa.
 
Sababu:Uchaguzi ni suala la Kisiasa,na washariki wakuu wa shughuli za kisiasa na chaguzi ni vyama vya kisiasa,hivyo tunapendekeza vyama vya kisiasa vihusike katika kuwathibitisha M/kiti na Makamu na wajumbe wa Tume, kwa kuzingatia Uchaguzi na washiriki wa Uchaguzi ni vyama vya siasa kwa kiwango kikubwa,wao ndio wanaopaswa kuthibitisha watu watakaosimamia haki zao katika chaguzi na si mwingine yeyote.
 
SURA YA KUMI NA NNE
 
MASHARTI KUHUSU FEDHA
(B) DENI LA TAIFA NA MIKOPO YA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO.
 
KIFUNGU 213:MAMLAKA YA KUKOPA
213(1)Tunapendekeza kuwa Serikali ya Muungano isiwe na mamlaka ya Kukopa nje ya nchi bali nchi washiriki na serikali zao ndio ziwe na haki hiyo.
Sababu 1:Kwa kuwa serikali ya Muungano itakuwa ikipata pesa toka nchi washirika basi isipewe mamlaka ya kukopa nje.
Sababu 2:Serikali hii kimuundo inaonekana ni ndogo ,pia inaonekana haitakuwa na rasilimali inayomiliki kwani Rasimimali zitakuwa mali ya washiriki wa Muungano ,hivyo kuipa mamlaka ya kukopa haitokuwa na maana yoyote.

( C ).VYANZO VYA MAPATO
215.(b) na (d) kuondolewa kama vyanzo vya mapato
Sababu:Imeelezwa katika kigungu 213(1)

SURA YA KUMI NA TANO
ULINZI NA USALAMA KATIKA TAIFA.
KIFUNGU 220(1):TAASISI ZA ULINZI NA USALAMA.
Tunapendekeza kuwa kuwe na Jeshi moja tu,‘JESHI LA WANANCHI NA LISIWE TAASISI’, kuwepo na kifungu maalumu cha ‘JESHI LA WANANCHI’ na Kifungu kidogo cha ‘JESHI LA AKIBA’ hii itaongeza unyeti wa Jeshi Letu.
Na Taasisi za Ulinzi na Usalama zijitegemee , ikiwa ni pamoja na kubadili Jina la Polisi kuwa ‘USALAMA WA RAIA’
Hivyo kuwa na taasisi za Usalama zifuatazo;
 
1. USALAMA WA RAIA
2. USALAMA WA TAIFA
 
Sababu: Jeshi ni chombo nyeti sana ,chombo amabcho ndicho chenye mamlaka ya kulinda mipaka ya nchi,kufanya ulinzi wa Kimataifa na kuwa na uwezo wa kupigana vita,sio vyema chopma hiki kikawekwa pamoja na vyombo vingine vyenye majukumu ya kulinda Raia na mali zao ndani ya nchi.Kwa kufanya hivi Jeshi litakuwa ni sehemu nyeti zaidi inayohusika na Ulinzi na Usalama wa nchi dhidi ya Nchi nyingine,hata wanajeshi wenyewe katika mafunzo yao hawafundishwi juu ya kuhusika na masuala ya uhalifu mdogo mdogo wa ndani ya nchi,kukamata wezi,kupeleleza uhalifu wa wizi bali hufundishwa juu ya kupigana vita na kulinda mipaka,kutumia silaha kali za vita ,kwa hali hii haitakuwa sawa kuliweka jeshi pomoja na Taasisi nyingine,kufanya hivyo ndio maana tumeshuhudia malalamiko mengi ya wananchi juu ya Jeshi kuingilia kazi za Taasisi nyingine kwa kupiga watu na kukamata (Mifano ipo mingi nchi)
 
Pia Jeshi hili liwekewe na Jeshi la akiba(Hawa ni Askari Waastafu, wenye Ujuzi na Siri mbali mabali za Nchi hii ).Jeshi hili la akiba litatumika kama sehemu ya Ushauri kwa jeshi la wananchi na linaweka kutumiwa wakati wote kwa manufaa ya Taifa.(Majeshi ya Akiba yapo katika nchi nyingi Duniani.
 
NYONGEZA
MAMBO YA MUUNGANO.
(YAMETAJWA KATIKA IBARA YA 60)
YAFUATAYO YAWE MAMBO YA MUUNGANO.
1. Katiba
2. Ulinzi na Usalama
3. Uraia
4. Mambo ya nje
5. Usajili wa Vyama
MENGINE YAWE NI KWA WASHIRIKI WENYEWE.
1. Uhamiaji
2. Sarafu na Benki
3. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo na kodi

MAMBO YA MUUNGANO.
 
Tunapendekeza haya yawe ya Muungano;
A. KATIBA-Ndiyo muungozo wa Jamhuri yetu
B. ULINZI NA USALAMA-Kwa ulinzi wa jamhuri yetu
C. URAIA-Wote tunakuwa watanzania kama ilivyo sasa
D. MAMBO YA NJE-Ili kuleta usawa katika sera za nje masuala haya yanapaswa kuwa ya Muungano, kwa kuwa kutokuwa na umoja katika mambo ya Nje kutapelekea kuwepo kwa kauli mbili tofauti kwa mabalozi wetu nje ya Jamhuri yetu,lakini izingatiwe kuwa suala la uteuzi wa MABALOZI liwe la Muungano kwa kufanya idadi sawa ya mabalozi huku suala la jinsia likizingatiwa.
 
E. USAJILI WA VYAMA-Kwa kuwa chama cha siasa ni Taasisi inayotokana na pande mbili basi suala hili liendelee kama ilivyo sasa kuwa la muungano.
 
MAMBO YASIYO YA MUUNGANO
 
Tunapendekeza haya yasiwe ya Muungano;
A. UHAMIAJI-Kila mshiriki wa Muungano ashughulikie masuala yake ya Uhamiaji mwenyewe
B. SARAFU NA BENKI- Suala la sarafu na benki liwe ni la washirika wenyewe,kama inavyofahamika ili nchi iwe ni nchi kamili suala la sarafu ni Muhimu,nchi isiyo na sarafu yake haiwezi kuwa nchi kamili,na kwa kuwa Muungano huu ni wa nchi Mbili ‘JAMHURI HURU’ ni vyema kila mshirki akawa na Sarafu na Benki yake ili kumwezesha kuwahudumia wananchi wake kwa jinsi anavyoona kwa kuwa na uhuru wa kukopa na kupata misaa,pia suala la mikopo na misaada ya nje liwe ni huru kwa nchi mshiriki wa Muungano . SABABU;Kuondoa malalamiko yaliyozoeleka ya nchi moja kuona kuwa inakosa pato la kotosha katika Muungano huu.

C. USHURU WA BIDHAA NA MAPATO- Kila mwanachama apewe uhuru wa kukusanya mapato yake ili kuendesha serikali yake, hii itaondoa lawama za mapato yanayotokana na bidhaa.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...