https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 20, 2013

Jumuiya ya wazazi CCM mkoani Tanga yatema cheche



Wana CCM, pichani. Picha na maktaba yetu.
Na Ray Said, Lushoto
VIONGOZI wa  Jumuiya  ya  wazazi  wilayani  Lushoto,  mkoani  Tanga, wameshauriwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye juhudi kwasababu siasa  za wakati huu zimejaa ushindani na kunahitajika utekelezaji  wa  sera  zilizowekwa  ili kuweza  kukipatia Chama cha Mapinduzi (CCM) ushindi  wa  kishindo mwaka  2015.

Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti  wa  Wazazi  Mkoani  Tanga  Dkt Edmund Mndolwa, alisema hayo katika ziara ya  kuwashukuru kwa kumchagua kwa  kishindo katika  nafasi  hiyo ya  kuwa  mwenyekiti  wa Jumuiya hiyo na kutembelea wilaya zote 9 za Mkoa wa Tanga.

Alisema imekuwa ni jambo la kawaida kwa wenyeviti na Makatibu kufanya kazi kimazoea kwa kufanya kazi zisizo eleweka kwa kigezo cha kuwa Chama Cha Mapinduzi tayari ni chama kikubwa na kinapendwa na kuza hofu kwa mustakabali wa siasa za Tanzania.

Mwenyekiti  huyo  ambae pia  ni   Mjumbe  wa  Halmashauri  kuu  ya  CCM  Taifa {NEC}aliwataka Viongozi hao kushuka chini kwa wanachama ambapo huko ndio kuna watu ambao wengi wao ni wakereketwa na ambao wanahitaji kuona maendeleo yao, kwa kupitia utekelezaji wa serikali wa Ilani ya uchaguzi ya Chama chao.

“Makatibu acheni  kuwa kama  miungu  watu  kutoa maagizo kwa simu bali nendeni  hadi katika ngazi za kata na kuona utekelezaji wa Ilani yetu inavyosimamiwa na viongozi ngazi ya tawi,” alisema.
Mndolwa nakuongeza  kuwa  kwa  kufanya  hivyo  Jumuia  yetu  itakuwa  imara  kwenye  ngazi  zote.

Kwa upande  mwingine  Dkt Mndolwa  aliwataka  wana CCM  kutosikiliza propaganda  zinazoenezwa  na  wapinzani, huku akiwaaasa wajibu mapigo kwa kuwakumbusha wapinzani maendeleo yaliyotekelezwa na serikali ya CCM kwenye nyanja za Elimu, Afya, miundombinu na mengineyo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...