https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 20, 2013

Tegua kitendawili, nani zaidi ya kati ya Diamond na Ommy Dimpozi kwa Bongo Fleva hawa?



KUNA wasanii makini na waofanya vyema mno katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya, maarufu kama Bongo Fleva. Si wengine, ila ni Diamond Platinum na mwenzake Ommy Dimpozi. Hawa vijana wanazua maswali mengi mtaani.

Kila mmoja anasema lake. Wapo wanaosema Diamond ni zaidi na mwingine anamuweka juu Ommy. Jana mitaa ya Kinondoni tulikuta ubishani wa hali ya juu.

Diamond kwa ameachia wimbo wake My Number One, wakati mwenzake Dimpozi anatamba na kibao chake cha Tupogo. Aidha Dimpoz pia ameshatamba na nyimbo kadhaa, ukiwamo ule wa Nai Nai. 

Wakati Diamond yeye alishakuwa na vibao motomoto ukiwamo ule wa Nimpende Nani.

Je, wewe una0na nani ni mkali zaidi ya mwenzake? Najua una mtu unayemkubali sana. Nataka nifahamu nani zaidi kwa upande wako? Binafsi kichwa kinauma. Nikisema Diamond mkali, nikianza kumfuatilia Dimpoz du hataree.

Pia hawa jamaa wamekuwa na mashabiki kadhaa kutokana na life style zao kitaani kwetu. Unajua nini ehee? Ati jamaa hawa ni wazee wa Pamba. Kuna mmoja anajiita yeye ni Rais wa Wasafi.

Weeee. Tena mtindo huo unaacha watu kinywa wazi hataree. Unajua nini ehee? Baadhi yao wanataka sana kujigandisha kwao kutokana na kung’aa kwao. Na ndio maana mmoja wapo hapo anaonekana kiwembe ile mbayaa.
Nataka uniambie nani kwako zaidi?
Tutumie barua pepe au msg ikisema nani zaidi kati yao.
+255712053949

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...