https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, September 21, 2013

Al Shabaab watingisha nchini Kenya leo na kuua kadhaa na kuzua taharuki ya aina yake



Na Mwandishi Wetu, Kenya
HALI ya hatari imezidi kutingisha viunga vya Kenya baada ya watu zaidi 22 kufariki Dunia baada ya watu kuvamia Westgate nchini humo na kuzua taharuki ya aina yake.
Hali ilivyokuwa nchini Kenya leo. Picha kwa hisani ya Reuters...
Wakati vifo hivyo vikitokea huku wengineo wakisema waliokufa ni zaidi ya watu 30, kundi la wanamgambo wa kiisilamu la Al shabaab nchini Somalia limedai kutekeleza mauaji hayo.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari nchini Kenya, kikundi hicho kimekiri kuhusika na kadhia hiyo, ikiwa ni ishara ya kuonyesha kuwa bado wana nguvu za kutingisha wanavyotaka.

Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mtu mmoja 
anayeshukiwa kuhusika na tukio hilo amekamatwa na sasa yupo chini katika matibabau hospitalini.

Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...