https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Tuesday, September 10, 2013

Waziri Mkuu Mizengo Pinda azindua maonyesho ya kibiashara ya Wachina leo jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Diamond Jubilee

Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kulia) akikata utepe leo kuashiria ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo ya siku nne yanalengo la kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini humo ili viwanda na makampuni ya nchi hiyo waweze kufanya biashara na watanzania. Kulia kwa waziri mkuu ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda na kushoto kwake ni Balozi wa China nchini LV Youqing.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alijaribu jembe la kupandia nafaka wakati alipotembelea banda la kiwanda cha Qingyuan Manchu Autonomous County cha nchini China wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.Wanaomtazama ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda (kushoto) na Balozi wa China nchini LV Youqing (kulia).
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia malighafi zinazotumiwa na kampuni ya Beijing New Building Material kutengenezea nyumba alipotembelea banda hilo leo wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Meneja Msaidizi Idara ya Biashara ya Kimataifa wa Kampuni hiyo Alec Lu na wapili kulia ni Makamu Meneja Mkuu Fred Yu.
Mfanyakazi wa kiwanda cha Changzhou Amec Group cha nchini China Yan Xing Long (kulia) akimueleza Waziri Mkuu Mizengo Pinda jinsi mashine ya kuchanganya kokoto iliyotengenezwa na kiwanda hicho inavyofanya kazi wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia mfano wa nyumba zinazojengwa na kampuni ya Beijing New Building Material alipotembelea banda hilo wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda na watatu kushoto ni Meneja Msaidizi Idara ya Biashara ya Kimataifa wa Kampuni Alec Lu.
Baadhi wa watu mbalimbali walioshiriki ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo ya siku nne ambayo yamefunguliwa leo yanalengo la kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini humo ili viwanda na makampuni ya nchi hiyo yaweze kufanya biashara na watanzania.Picha na Anna Nkinda – Maelezo

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...