https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, September 08, 2013

Unga wa sembe sasa washuka bei na kuwapa nafuu walaji jijini Dar es Salaam



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BAADA ya kusota kwa miezi kadhaa, sasa wakazi wengi jijini Dar es Salaam, wameanza kupumua kutokana na bei ya unga wa sembe kushuka kutoka kwenye Kilo sh 1300 hadi 1400 na kufikia kilo moja sh 1000.
Hali hiyo imesababishwa na maeneo mengi ya vijijini kuanza kuvuna mahindi yao, hivyo kupunguza kasi ya bei hiyo maeneo ya mijini, hasa jijini Dar es Salaam.

Handeni Kwetu Blog ilitembelea maduka kadhaa yaliyopo Kimara, jijini Dar es Salaam na kukuta wafanyabiashara wa maduka wakiuza unga huo kwa sh 1000.

Juhudi zinafanywa ili kupatikana kwa bei zote za bidhaa za chakula jijini Dar es Salaam, kama vile mchele, unga wa dona, sukari, maharage na nyinginezo.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...