https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, September 21, 2013

Kuachiwa kwa Masogange kwavuta hisia za wengi, nguvu na harakati za Mwakyembe sasa zajadiliwa na kuzua maswali lukuki



Na Timu ya Handeni Kwetu Blog
TUKIO la kuachiwa huru kwa msanii Agness Gerald Masogange na Melisa Edward nchini Afrika Kusini, limepokelewa kwa shingo upande na Watanzania wengi wanaofuatilia kasi ya dawa za kulevya.
Dawa za kulevya
Katika hilo, wapo wanaochukizwa na uamuzi huo wakisema kuwa ni njia ya kumdhalilisha Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyemba, aliyepania pia kulivalia njuga suala hilo.

Masogange amepigwa faini ya shilingi za Tanzania Milioni tano, kwasababu ya madai kuwa walizokutwa nazo si dawa za kulevya.



Masogange akiwa katika pozi kama unavyomuona hapo. Chezea Masogange wewe.
Katika mitandao ya kijamii na mitaani, kila mmoja anasema lake, huku wengineo wakifika mbali zaidi kupekua na kuorodhesha vifungu vya maswali vya kuangalia sakata hilo.

Masogange ametiwa hatiani na kalipa faini. Melisa ameachiwa huru. Kesi yao imekuwa rahisi baada ya kubainika kwamba yale waliyobeba yalikuwa si madawa ya kulevya bali mali ghafi mojawapo ya kutengenezea madawa ya kulevya.

Waziri wa Uchukuzi, Harrison Makyembe, pichani.
Mtanzania mmoja, anayejulikana kwa jina la Ibrahim Mkamba, aliandika mambo mengi kwenye wall yake facebook. Na haya ndiyo aliyoandika na sisi tumeyachukua kama yalivyo kama ishara ya kupanua wigo wa kufikiri juu ya vita ya dawa za kulevya Tanzania kama tulivyoweka mengine hapo chini ili kupata la kujadili juu ya vita hii.
Melisa Edward pichani, aliyeachiwa sambamba na Masogange, nchini Afrika Kusini, baada ya kuonekana hana hatia.

"Tungekuwa serious na kama watu wanaokubalika na watu hawahusiki na sula hilo, tungefanya upelelezi wetu wa kina ili usaidie kuziba mianya yote ya suala hilo kwa kupata kutoka kwa Masogange na Mellisa fact:-
1. kwamba walisafirisha mali hiyo wakijua kwamba ni mali ghafi ya madawa ya kulevya?

2. kwamba waliitoa wapi mali ghafi hiyo na walikuwa wanampelekea nani au taasisi gani Afrika Kusini?

3. kwamba walijiamini vipi kusafiri na mzigo huo yaani nani alisimamia mambo yaliyohusu safari yao?

4. kwamba walisafiri vipi kwenda JNIA, kwa gari la kukodi au la mtu binafsi? Kama la binafsi nani aliwapeleka hapo uwanjani?
5. kwamba safari na mzigo huo ilianzia wapi, wanakoishi au pengine? Ni wapi hapo?

6.kwamba walienda Afrika Kusini kwa madhumuni ya kupeleka mzigo huo tu au na madhumuni mengine? 7. kwambafaini ya rand 30 ambayo ni milioni 4 za bongo Masogange alilipa mwenyewe au alilipiwa? Kama alilipiwa, nani alimlipia? 8. kwamba wakiwa mahabusu Afrika Kusini waliwakuta watanzania wengine wa kesi za unga?

9. Kwamba zaidi ya usanii wanafanya shughuli gani za kimaisha?
10. Kwamba wana nini kingine chochote cha kueleza kuhusu tukio hilo kitakachoisaidia jamii?

Tutapongezana kwa kushinda kesi ya uchafu lakini ni vizuri tujulishane kwamba kwa yanayozungumzwa uswahilini, kesi hii imeweka doa kubwa na imeshusha hadhi vibaya sana kwa mamlaka zilizokuwa zikiheshimika sana. Tuone yatakayofuata baada ya kina Masogange kurudi kama yatachafua zaidi au yatapunguza uchafu," mwisho wa andiko la Mkamba.
 

Naye Bernard Bakuza, aliandika hivi, “Hatimaye agnes gerald aka masogange na melissa edward waachiwa huru nchini afrika kusini walichokamatwa nacho si madawa ya kulevya....
Nisaidieni inakuwaje na wale watumishi wa Uwanja wa ndege waliofukuzwa wanarejeshwa kazini ama....Mwakyembeeeeeeeee.
Naye Olivia Sanare aliandika hivi “Kwa mtaji huu vita dhidi ya madawa ya kulevya haiwezi kuisha.
Kina masogange wameachiwaje?wanadai hazikuwa dawa za kulevya zilikuwa zilikuwa dawa za kemikali nchi ya drama.
Ni vyema basi hata wale waliosimamishwa kazi na Mh.Mwakyembe warudishwe kazini sababu hawana hatia kama mambo yenyewe ndo haya,” mwisho wa status yake na kuchangiwa na watu wengi mno katika group la Tanuru la Fikra.
Katika kuliangalia suala hilo, kuna mengi yanaweza kupatikana, ikiwa ni pamoja na udhaifu wa sheria zetu au vitendo vya kupindua pindua mambo.
Wataalamu wa mambo ya kisiasa wanachukulia suala hilo kama tusi lingine kwa Makyembe, kutokana na watu hao kuachiwa wakati alifikia kutimua wafanyakazi kadhaa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere akisema kuwa walichangia kupitishwa kwa dawa za kulevya na Masogange.
Je, Mwakyembe kama Waziri wa Uchukuzi ataendeleza moto wake kupambana na usafirishaji wa dawa za kulevya Tanzania au atazima moto wake na kuacha wafanye wanavyotaka?
Nini kinafuata baada ya Masogange kuachiwa? Tusubiri tuone.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...