https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Sunday, September 22, 2013

DK. SEIF KHATIB AKUTANA NA KATIBU WA MAMBO YA NJE WA CHAMA CHA ANC CHA AFRIKA KUSINI.

 KATIBU wa NEC, Oganaizesheni Dk. Mohamed Seif Khatib, akimkaribisha Katibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini Billy Masetlha (kushoto) alipowasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, jana, kwa ajili ya mazungumzo na kuwasilisha, Makubaliano ya viongozi wa vyama vya mstari vya ukombozi kusini mwa Afrika,  yaliyofikiwa na viongozi hao katika mkutano wao wa Machi 7, mwaka huu mjini Pretoria, Afrika Kusini.
 KATIBU wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini Billy Masetlha (kushoto) alikimkabidhi Katibu wa NEC ya CCM, Ogamaizesheni, Muhamed Seif Khatib, kabrasha la Makubaliano ya viongozi wa vyama vya mstari vya ukombozi kusini mwa Afrika,  yaliyofikiwa na viongozi hao katika mkutano wao wa Machi 7, mwaka huu mjini Pretoria, Afrika Kusini, jana, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
 KATIBU wa NEC, Oganaizesheni Dk. Mohamed Seif Khatib, akizungumza na Katibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini Billy Masetlha (kushoto) alipowasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya mazungumzo na kuwasilisha, Makubaliano ya viongozi wa vyama vya mstari vya ukombozi kusini mwa Afrika,  yaliyofikiwa na viongozi hao katika mkutano wao wa Machi 7, mwaka huu mjini Pretoria, Afrika Kusini.
 KATIBU wa NEC, Oganaizesheni Dk. Mohamed Seif Khatib, akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini Billy Masetlha (kushoto) alipowasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya mazungumzo na kuwasilisha, Makubaliano ya viongozi wa vyama vya mstari vya ukombozi kusini mwa Afrika,  yaliyofikiwa na viongozi hao katika mkutano wao wa Machi 7, mwaka huu mjini Pretoria, Afrika Kusini. Wengine kushoto ni Ofisa kutoka ANC Lebogang Matshaba na kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida
"KOTE KULEE NILIWAHI KUFIKA..." Katibu wa Mambo ya Nje Chama cha ANC cha Afrika Kusini Billy Masetlha akimwambia Dk. Khatib wakati akiaga nje ya Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, baada ya mazungumzo yao.

Kwa Hisani:Taifa letu.com

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...