https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, September 20, 2013

Mdoe: Tumekusudia kumthamini Gurumo



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KATIBU wa Kamati ya Gurumo 53 iliyoandaliwa kwa ajili ya kumuandalia shoo maalum ya kumuaga Muhdini Gurumo, Said Mdoe, amesema kuwa lengo lao ni kuhakikisha kuwa mwanamuziki huyo mkongwe anapata tumaini jipya baada ya kustaafu muziki.
Kamati ya Gurumo 53 ikizungumza na waandishi wa Habari wiki iliyopita jijini Dar es Salaam. Kulia ni Said Mdoe, Katibu wa Kamati hiyo.
Shoo ya Gurumo imepangwa kufanyika Oktoba 11 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, wakati ile ya pili itafanyika Novemba Mosi, TCC Sigara Chang’ombe, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mdoe alisema kuwa kwa sasa kila kitu kinaendelea vizuri kwa ajili ya kuhakikisha kuwa shoo hiyo inakuwa ya aina yake.

Alisema kuwa lengo lao ni kuthamini mchango wa mwanamuziki huyo aliyetangaza kuachana na muziki, hali ya kuwa hana kitu cha maana alichokipata.

"Kamati yetu inaendelea vizuri katika maandalizi ya shoo hizi mbili za mkongwe wa muziki, Gurumo ambaye kwa sasa umri wake unamfanya ashindwe kupanda jukwaani.

"Lengo letu ni kuona mwanamuziki huyo anaagwa kwa heshima kutokana na mchango wake katika tasnia ya muziki wa dansi hapa nchini,” alisema Mdoe.

Kamati hiyo ipo chini ya mwenyekiti wake Asha Baraka, ambaye pia ni Mkurugenzi wa The African Stars, Twanga Pepeta inayotesa katika tasnia ya muziki wa dansi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...