https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, May 02, 2013

Wizara ya Ujenzi yatoa mafunzo kwa wakandarasi wanawake mkoani Kilimanjaro

Meneja wa TANROAD mkoa wa Kilimanjaro, Marwa Rubirya akizungumza na Washiriki katika ufunguzi wa Semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Kiliamnajro Cranes kutoa mafunzo ya ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za Barabara nchini.


Kaimu katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Martha Ufunguo, akizindua semina ya mafunzo ya siku kumi kwa Washiriki zaidi ya 30 yaliyoandaliwa na Wizara ya Ujenzi kutoa mafunzo ya ushirikishwaji wa wanawake katika kazi barabara, yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Kilimanjaro Cranes, mkoani Kilimanjaro.

 Mratibu wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Mwanaisha Urenge, akizungumza na Washiriki zaidi ya 30 katika semina ya mafunzo ya ushirikishwaji wa wanawake katika kazi barabara, yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Kilimanjaro Cranes, mkoani Kilimanjaro.

Katika picha ya pamoja ni washiriki wa semina ya siku ya mafunzo ya ushirikishwaji wa wakandarasi wanawake katika kazi za barabrani, kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Geita, Manyara, Arusha, Singida, Da es salaam, Katavi na Pemba, yaliyoandaliwa na Wizara ya Ujenzi, katikia ukumbi wa Kilimanjaro Cranes, Mkoani Kilimanjaro.

Katika picha ya pamoja ni washiriki wa semina ya siku ya mafunzo ya ushirikishwaji wa wakandarasi wanawake katika kazi za barabrani, kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Geita, Manyara, Arusha, Singida, Da es salaam, Katavi na Pemba, yaliyoandaliwa na Wizara ya Ujenzi, katikia ukumbi wa Kilimanjaro Cranes, Mkoani Kilimanjaro.



Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro
WIZARA  ya Ujenzi imetoa mafunzo kwa wanawake wakandarasi kuhusu njia ambayo inaweza kuwasaidia kushiriki kikamilifu katika kazi za ujenzi za Barabara ambapo imebainika kwamba wanawake wengi wakandarasi hukumbana na changamoto nyingi katika kazi za ujenzi kutokana na uwepo wa ushindani mkubwa kwa sasa.

Hayo yamebainishwa leo katika semina ya mafunzo ya Wizara ya Ujenzi, Barabara na Nyumba na kutoa uwezo kwa wahandisi wanawake kushiriki kikamilifu katika kazi za barabarani yaliyofanyika katika ukumbi wa Kilimanjaro Cranes na kushirikisha washiriki zaidi ya 30 kutoka katika mikoa zaidi kumi.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...