https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 03, 2013

Leaders Club yasukiwa zengwe ili ifungwe kwa madai inapigia kelele wakubwa wanaoishi kwenye maeneo hayo



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
HALI ya hatari imeanza kuonekana baada ya kigogo mmoja serikali kutoka jiji la Dar es Salaam kupendekeza Viwanja vya Leaders Club kuachwa kutumiwa katika masuala ya kiburudani kwa madai kuwa yanabugudhi watu wanaoishi kwenye maeneo hayo.
Hawa ni baadhi ya wadau wakijadiliana mambo baada ya kufikishiwa habari za kusimamisha bonanza la michezo lililofanyika juzi katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni.
 
Sakata hili limejitokeza katika siku za hivi karibuni, baada ya kutokea mvutano kwa baadhi ya wadau wa burudani na Ofisi ya Utamaduni Kinondoni, kuvamia katika viwanja hivyo na kuzuia mambo yanayofanyika hapo mara kwa mara.

Kwa wasiofika Leaders Club, viwanja hivyo hutumika zaidi katika siku za Jumapili, ambapo bendi ya Twanga Pepeta  hufanya shoo ya mwisho wa wiki, katika bonanza lake, wakati pia bendi za Msondo Ngoma na kujumuisha pia matukio mbalimbali.

Aidha, Kampuni ya Prime Time Promotion ya jijini Dar es Salaam sambamba na Clouds Media Group inafanya shoo ya kila mwaka ya Fiesta inayofanyika pia katika viwanja hivyo.

Juzi, Clouds waliandaa bonanza la michezo lililojumuisha pia Kampuni mbalimbali na wafanyakazi wao kuonyesha uwezo wao.

Habari kutoka ndani ya Ofisi ya Utamaduni Kinondoni zinasema kuwa kuna kigogo mmoja anayeishi katika maeneo hayo, hivyo amepiga marufuku kwasababu hataki kelele.

“Suala la Leaders Club lazima liende na mtu, maana bosi hataki kufanyike shughuli yoyote inayohusu mziki katika eneo hili, wakati anajua fika Kinondoni hakuna viwanja vya wazi.

“Kwakweli naogopa, hivyo tunapofuatilia suala hili lazima ijulikane kuwa sisi ni watu wadogo na maagizo kama haya hutolewa na watu wazito na kuibua mgogoro mkubwa,” alisema mpashaji huyo ambaye naye anatoka katika ofisi za serikali.

Viwanja vya Leaders Club ni sehemu pekee tulivu ambavyo vinaweza kukusanya watu wengi katika matukio mbalimbali na kujadiliana mambo ya kimaisha, yakiwamo yale ya kiburudani.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...