https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, May 03, 2013

Kumekucha Bungeni Dodoma: Tume ya Waziri yatangaza kusahihishwa upya kwa mitihani ya wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 na kufuta yale yaliyotangazwa

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
BUNGE kwa kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu wa Bunge, William Lukuvi, leo ametangaza uamuzi uliochukuliwa na Tume ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kufuatia mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012 watoto wengi kufeli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu wa Bunge, William Lukuvi

Kwa mujibu wa Tume hiyo, imependekeza mtihani wa kidato cha nne kusahihishwa upya huku ikiyafuta yale yaliyotangazwa kwa ajili ya kuweka usahihi na njia ya kuelekea kilele cha ubora wa elimu ya Watanzania wote.

Akizungumza Bungeni leo mjini Dodoma, Lukuvi alisema kuwa mitihani hiyo inapaswa kusahihishwa kwa kufuata kanuni ya mwaka 2011, hivyo uamuzi huo umetolewa na Tume ya Waziri Mkuu Pinda aliyounda baada ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutangaza matokeo ya kidato cha nne huku asilimia 60 ya wanafunzi wote kufeli.

Suala hilo liliibua mtafaruku mkubwa kwa wadau na wanasiasa wa Tanzania, wakililia haki ya mtoto wa Tanzania kusoma, huku wakisema kufeli kwao kutaongeza joto la maisha magumu kwa watoto hao ambao wengi wanatoka kwenye familia masikini.

Taarifa zaidi ya Tume hiyo na uamuzi wako itaendelea kukujia katika blog yako hii, kwa ajili ya kukufikishia habari kamili na namna ya kuwapatia haki ya kupata elimu watoto wa Tanzania.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...