https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, July 27, 2013

Picha mbalimbali za kusisimua, Dar es Salaam na wilayani Handeni



Ukifika wilayani Handeni, mkoani Tanga, lazima ukutane na bango hilo hapo linaloelimisha masuala ya afya na Ugonjwa wa Ukimwi. Eneo hili lipo karibu kabisa na Ofisi ya Mkuu wa wilaya Handeni pamoja na ofisi nyingi za serikali wilayani humo. Picha na Kambi Mbwana, aliyekuwa wilayani Handeni.



Maeneo ya katikati ya jiji la Dar es Salaam hali hii ni kawaida kabisa. Pichani gari la taka likiwa limesheheni uchafu maeneo ya jiji. Mara kadhaa gari hili linapopita watu wengi hujikuta wameziba pua zao kwa harufu kali kutokana na takataka hizo. Picha na Kambi Mbwana.



Raha ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani Kujisitiri kwa mavazi yenye heshima na kuziba sehemu yote ya mwili, kikiwamo kichwa, kama alivyokutwa dada huyu Grace Misango, maeneo ya Kimara, jijini Dar es Salaam leo. Akina dada wengi katika kipindi cha mwezi huu wa Ramadhani unaoendelea wamekuwa wakivaa nguo za heshima zaidi jambo linalowatofautisha kabisa na kipindi chote cha maisha, hivyo kuna ulazima wa mwezi huu kuendelea? Picha na Mpiga Picha Wetu.



Mfanyabiashara huyu alikutwa hivi karibuni kijiji cha Sindeni, wilayani Handeni mkoani Tanga, akipandisha mbuzi wake kwenye gari, halipo pichani akiwasafirisha wilayani Korogwe mkoani Tanga. Picha na Kambi Mbwana, aliyekuwa Handeni.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...