https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Wednesday, July 24, 2013

Aliyekufa kwa ajali ya pikipiki azikwa na kuacha simanzi kubwa kijijini kwao



Na Mwandishi Wetu, Handeni
MJASIRIAMALI kijana katika kijiji cha Komsala, wilayani Handeni, mkoani Tanga, Vitalis William, maarufu kama Kihiyo, alizikwa juzi katika makaburi ya kijiji hicho na kuacha simanzi kubwa.
Mmoja wa wanakijiji wa Komsala, wilayani Handeni, mkoani Tanga, Sadiki Mbwana, ambaye ndio chanzo cha habari hii pichani.

Hiyo ni kutokana na aina ya kifo chake pamoja na juhudi za kujikwamua katika lindi la umasikini, akifanikiwa kufanya biashara mbalimbali katika kijiji hicho na Handeni kwa ujumla.

Marehemu alifariki kwa ajali ya pikipiki iliyogongana na baiskeli na kusababisha vifo vya watu wawili huku mmoja akilazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, Magunga.

Akizungumza baada ya mazishi hayo, mkazi wa kijiji cha Komsala, Sadiki Mbwana, alisema kifo cha Kihiyo kimeacha majonzi makubwa kutokana na mchango wake.

Alisema akiwa na umri mdogo usiozidi miaka 29, Kihiyo alifanya juhudi nyingi kujikwamua, ikiwamo kujiingiza katika ujasiriamali na kuvutia wat wote kufuata nyayo zake.

“Tumeguswa sana na msiba wa mwanakijiji mwenzetu huyu, ambaye kwa kiasi kikubwa alikuwa akifanya biashara na maendeleo yake yalikuwa makubwa kupita kiasi.

“Nadhani tuna kila sababu ya kuumia na msiba huu, huku tukitumia nafasi hii kujaribu kushawishiana ili tufuate nyayo zake kwa ajili ya vijana kujikwamua katika lindi la umasikini,” alisema.

Kwa mujibu wa Mbwana, marehemu aliwahi kuja jijini Dar es Salaam, lakini alirudi kijijini kwao baada ya kuona hakuwa na kazi ya kufanya, hivyo kuanza kuwekeza kijijini hapo na hatimae kuanza kutokea peupe, baada ya kufanikiwa kununua vitu mbalimbali pamoja na duka kubwa, huku akiwa na ndoto za kujitanua nje ya wilaya yao.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...