https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Monday, July 29, 2013

Maonyesho ya Elimu kufanyika Viwanja Vya Posta kuanzia Agosti 30 mwaka huu jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillip Mulugo katikati akizungumzia maonyesho ya elimu yaliyozinduliwa leo Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa Vodacom ambao ndio wadhamini wakuu, Kelvin Twissa, wakati kulia kwake ni muandaaji, Joel Njama. Picha ya juu ni Kelvin Twissa akizungumza jambo linalohusu maonyesho hayo..

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillip Mulugo, jana alizindua rasmi maonyesho ya elimu yaliyopangwa kufanyika kuanzia Agosti 30 mwaka huu katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam ambapo watu mbalimbali wanatarajiwa kushiriki kwa ajili ya kuboresha kiwango cha elimu hapa Tanzania...

Katika maonyesho hayo, watu mbalimbali ikiwamo Kampuni ya Simu za Mikononi ya Vodacom Tanzania, imethitibisha kuwezesha katika maonyesho hayo yanayoandaliwa na Elimu Expo kwa ajili ya kuruhusu muingiliano wa majadiliano kati ya watengenezaji wa sera, wapenda maendeleo, watunzi mbalimbali, wazazi, wanafunzi, na jamii kwa ujumla.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...