https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Thursday, July 11, 2013

Bondia Mbwana Matumla alilia mapromota wa masumbwi Tanzania


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa ngumi za kulipwa hapa nchini, Mbwana Matumla, amesema kwamba Tanzania bado inaandamwa na ukosefu wa mapromota, hali inayosababisha mchezo wa ngumi usifanye vizuri zaidi.
Bondia Mbwana Matumla, pichani.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Matumla alisema kuwa uhaba huo wa mapromota kunasababisha mabondia wengi washindwe kupata nafasi ya kuonyesha makali yao ulingoni.

Alisema endapo mapromota wangekuwa wengi, hata mwamko katika mchezo huo ungekuwa mkubwa, hivyo kuwafanya mabondia wapya kutamani zaidi tasnia hiyo ya masumbwi.

Matumla aliendelea kusema wapo mabondia ambao kwa mwaka wanapanda ulingoni mara moja au wasipande kabisa katika kuwania mikanda mbalimbali, hivyo kuathiri vipaji vyao.

“Kama bondia anakosa pambano, ina maana kipaji chake kinaweza kupotea, ukizingatia kuwa kabla ya kuangalia nje ya nchi lazima awe na rekodi nzuri katika mapambano ya ndani.

“Hali hii inasababisha wadau wa ngumi waone kuna haja sasa ya kuingia katika mchezo wa masumbwi kwa ajili ya kuuweka juu zaidi kwa kuhakikisha kuwa wanaandaa mapambano,” alisema Matumla.

Matumla anayetokea katika familia wana masumbwi ni miongoni mwa mabondia wenye uwezo wa juu katika mchezo huo, huku akifanikiwa kuibuka na ushindi katika mapambano mengi anayopanda ulingoni.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...