https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, June 07, 2013

Diwani wa CCM na mume wa Khadija Kopa kuzikwa leo saa tisa mjini Bagamoyo



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KADA wa Chama Cha Mapinduzi na Diwani wa Kata ya Magomeni, Bagamoyo mkoani Pwani ambaye pia ni mume wa Khadija Kopa, Jafary Ally anazikwa leo saa tisa mjini Bagamoyo.


Khadija Kopa akimlilia mumewe jana.
Kwa sasa msiba upo kwa wazazi wake Tandale, lakini muda mchache ujao watu wataanza kuelekea Bagamoyo kwa ajili ya mazishi. Jana kulikuwa na mvutano, baada ya baadhi ya watu, wakiwamo viongozi wa CCM kutaka Ally akazikwe Bagamoyo.

Taarifa zaidi ya mazishi ya mume wa Kopa zitaendelea kukujia katika blog yako ya Handeni Kwetu.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...