https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Friday, June 14, 2013

Ubaguzi wa wasanii Bongo wadhihirika baada ya kususia mazishi ya Kihiyo yaliyofanyika leo jioni Makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UBAGUZI wa wasanii Tanzania umedhihirika leo baada ya kususia msiba wa msanii mwenzao Hassan Kihiyo aliyezikwa saa kumi za jioni katika makaburi ya Mwinyimkuu, Magomeni.
 Jeneza la marehemu Kihiyo likiwasili eneo la makaburini tayari kwa mazishi yake yaliyofanyika leo jioni makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni.
 Kaburi la marehemu Kihiyo linavyoonekana kwa ndani....
 Jeneza la marehemu Kihiyo likipelekwa kaburini tayari kwa mazishi yake yaliyofanyika leo jioni makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni.

 Mwili wa marehemu Kihiyo ukiwa ndani ya kaburi.....
Jeneza la marehemu Kihiyo likipelekwa kaburini tayari kwa mazishi yake yaliyofanyika leo jioni makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni.

Msiba huo ulihudhuriwa na wasanii wachache, hasa wale wasiokuwa na majina makubwa, licha ya Kihiyo kujitoa mara kwa mara katika matatizo ya wasanii wengine Tanzania.

Kihiyo alifariki jana jioni katika Hospitali ya Wilaya Temeke alipokuwa amelazwa akipata matibabu na kupeleka huzuni kubwa kwa baadhi ya wasanii na mashabiki wanaomuunga mkono.

Mazishi ya msanii huyu hayakuwa na tofauti  na watu wengi, licha ya kucheza filamu kadhaa na kushiriki kutengeneza movie za wasanii wengine kwa namna moja ama nyingine. Kihiyo alicheza filamu zaidi ya nne, ikiwamo ile Mother House, Kaburi Moja, Chanzo ni Mama, Where is God, My Book na nyinginezo.

Wadau na wasanii wachache waliohudhuria msiba huo ni pamoja na Emmanuel Shija, John Mtitu, John Lister, mtunzi wa filamu na maigizo Tanzania, Muddy Kimindu Kulinyangwa ambaye pia ametunga nyimbo mbalimbali za taarabu kama vile Domo la Udaku la T-Moto Taarab, Nani Kama Mama wa Isha Mashauzi na nyinginezo.

Mbali na kususia kwa wakali wa filamu Tanzania, mazishi ya Kihiyo yalifanyika vizuri na kutanguliwa na swala, ambapo msikiti haukuwa mbali na nyumbani ulipokuwapo msiba pamoja na sehemu ya makaburi aliyozikiwa marehemu.

Wasanii wa Tanzania kwa mtindo huo wameonekana kubaguana wenyewe kwa wenyewe, wakiangaliana usoni na wale wenye majina makubwa zaidi ndio wanaoishi kwa kujuliana hali, hasa katika matukio ya misiba wakiamini vyombo vya habari, wadau na mashabiki wataendelea kujazana kwa ajili ya kutaka kuuza sura.


No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...