https://tpc.googlesyndication.com/simgad/8045142562622600543


Recent Post

Saturday, June 29, 2013

Serikali yasimamisha shughuli za uchimbaji dhahabu, mgodi wa Magambazi




Na Mwandishi Wetu, Handeni
SERIKALI kwa kupitia Mkurugenzi wa Wilaya ya Handeni, Khalfany Haule, imetangaza kupiga marufuku shughuli zote za uchimbaji au utafiti wa madini, katika Mgodi wa Dhahabu uliopo wilayani Handeni, mkoani Tanga.
  Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu
Mgodi huo unaojulikana kama Magambazi, uliopo Magamba, wilayani Handeni mkoani Tanga, umekuwa ukiibuka kwa matamshi ya kila aina, huku ukikumbukwa pia kuleta mtifuano miongoni mwa wananchi wilayani humo.

Akizungumza mapema wiki hii, Haule alisema kuwa wilaya yao imesimamisha shughuli zote zinazofanyika katika Mgodi huo, zikiwapo zile zinazodaiwa kuwa ni kufanyika kwa utafiti juu ya dhahabu hizo.

Alisema yoyote atakayefanya kazi kinyume, atakuwa amekiuka agizo halali, hivyo atalazimika kufanyiwa kazi, hivyo ni vyema wananchi na watu wote wakafuata maagizo yao.

“Tumesimamisha shughuli zote zinazohusiana na mambo ya dhahabu katika mgodi ule, hivyo kwa sasa hakuna atakayeruhusiwa kufanya jambo lolote lile katika mgodi huo.

“Hata wale waliokuwa wakifanya utafiti hawataruhusiwa kwa namna yoyote hadi hapo itakapotangazwa tena, maana kumekuwa na hila inayofanyika, hasa madai kuwa wapo wanaochimba madini na kudai kuwa wanafanya utafiti, hivyo kuleta mtazamo tofauti.

Kauli hiyo huenda ikazidisha au kupunguza ukakasi wa baadhi ya wawekezaji katika migodi ya Tanzania wanaofanya shughuli hizo na kuliacha Taifa katika mashimo na wao kunufaika.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...